Swahili: New Testament

American Standard Version

1 Corinthians

12

1Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
1Now concerning spiritual [gifts], brethren, I would not have you ignorant.
2Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
2Ye know that when ye were Gentiles [ye were] led away unto those dumb idols, howsoever ye might led.
3Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
3Wherefore I make known unto you, that no man speaking in the Spirit of God saith, Jesus is anathema; and no man can say, Jesus is Lord, but in the Holy Spirit.
4Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
4Now there are diversities of gifts, but the same Spirit.
5Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
5And there are diversities of ministrations, and the same Lord.
6Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
6And there are diversities of workings, but the same God, who worketh all things in all.
7Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
7But to each one is given the manifestation of the Spirit to profit withal.
8Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
8For to one is given through the Spirit the word of wisdom; and to another the word of knowledge, according to the same Spirit:
9Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
9to another faith, in the same Spirit; and to another gifts of healings, in the one Spirit;
10humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
10and to another workings of miracles; and to another prophecy; and to another discernings of spirits; to another [divers] kinds of tongues; and to another the interpretation of tongues:
11Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
11but all these worketh the one and the same Spirit, dividing to each one severally even as he will.
12Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
12For as the body is one, and hath many members, and all the members of the body, being many, are one body; so also is Christ.
13Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
13For in one Spirit were we all baptized into one body, whether Jews or Greeks, whether bond or free; and were all made to drink of one Spirit.
14Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
14For the body is not one member, but many.
15Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
15If the foot shall say, Because I am not the hand, I am not of the body; it is not therefore not of the body.
16Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
16And if the ear shall say, Because I am not the eye, I am not of the body; it is not therefore not of the body.
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
17If the whole body were an eye, where were the hearing? If the whole were hearing, where were the smelling?
18Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
18But now hath God set the members each one of them in the body, even as it pleased him.
19Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
19And if they were all one member, where were the body?
20Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
20But now they are many members, but one body.
21Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."
21And the eye cannot say to the hand, I have no need of thee: or again the head to the feet, I have no need of you.
22Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
22Nay, much rather, those members of the body which seem to be more feeble are necessary:
23Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
23and those [parts] of the body, which we think to be less honorable, upon these we bestow more abundant honor; and our uncomely [parts] have more abundant comeliness;
24ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
24whereas our comely [parts] have no need: but God tempered the body together, giving more abundant honor to that [part] which lacked;
25ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
25that there should be no schism in the body; but [that] the members should have the same care one for another.
26Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
26And whether one member suffereth, all the members suffer with it; or [one] member is honored, all the members rejoice with it.
27Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
27Now ye are the body of Christ, and severally members thereof.
28Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
28And God hath set some in the church, first apostles, secondly prophets, thirdly teachers, then miracles, then gifts of healings, helps, governments, [divers] kinds of tongues.
29Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
29Are all apostles? are all prophets? are all teachers? are all [workers of] miracles?
30Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
30have all gifts of healings? do all speak with tongues? do all interpret?
31Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.
31But desire earnestly the greater gifts. And moreover a most excellent way show I unto you.