1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
1Now concerning the collection for the saints, as I gave order to the churches of Galatia, so also do ye.
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
2Upon the first day of the week let each one of you lay by him in store, as he may prosper, that no collections be made when I come.
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
3And when I arrive, whomsoever ye shall approve, them will I send with letters to carry your bounty unto Jerusalem:
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
4and if it be meet for me to go also, they shall go with me.
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
5But I will come unto you, when I shall have passed through Macedonia; for I pass through Macedonia;
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
6but with you it may be that I shall abide, or even winter, that ye may set me forward on my journey whithersoever I go.
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
7For I do not wish to see you now by the way; for I hope to tarry a while with you, if the Lord permit.
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
8But I will tarry at Ephesus until Pentecost;
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
9for a great door and effectual is opened unto me, and there are many adversaries.
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
10Now if Timothy come, see that he be with you without fear; for he worketh the work of the Lord, as I also do:
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
11let no man therefore despise him. But set him forward on his journey in peace, that he may come unto me: for I expect him with the brethren.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
12But as touching Apollos the brother, I besought him much to come unto you with the brethren: and it was not all [his] will to come now; but he will come when he shall have opportunity.
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
13Watch ye, stand fast in the faith, quit you like men, be strong.
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
14Let all that ye do be done in love.
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
15Now I beseech you, brethren (ye know the house of Stephanas, that it is the firstfruits of Achaia, and that they have set themselves to minister unto the saints),
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
16that ye also be in subjection unto such, and to every one that helpeth in the work and laboreth.
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
17And I rejoice at the coming of Stephanas and Fortunatus and Achaicus: for that which was lacking on your part they supplied.
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
18For they refreshed my spirit and yours: acknowledge ye therefore them that are such.
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
19The churches of Asia salute you. Aquila and Prisca salute you much in the Lord, with the church that is in their house.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
20All the brethren salute you. Salute one another with a holy kiss.
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
21The salutation of me Paul with mine own hand.
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
22If any man loveth not the Lord, let him be anathema. Maranatha.
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
23The grace of the Lord Jesus Christ be with you.
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.
24My love be with you all in Christ Jesus. Amen.