Swahili: New Testament

American Standard Version

1 Thessalonians

3

1Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
1Wherefore when we could no longer forbear, we thought it good to be left behind at Athens alone;
2na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
2and sent Timothy, our brother and God's minister in the gospel of Christ, to establish you, and to comfort [you] concerning your faith;
3kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
3that no man be moved by these afflictions; for yourselves know that hereunto we are appointed.
4Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
4For verily, when we were with you, we told you beforehand that we are to suffer affliction; even as it came to pass, and ye know.
5Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
5For this cause I also, when I could no longer forbear, sent that I might know your faith, lest by any means the tempter had tempted you, and our labor should be in vain.
6Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
6But when Timothy came even now unto us from you, and brought us glad tidings of your faith and love, and that ye have good remembrance of us always, longing to see us, even as we also [to see] you;
7Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
7for this cause, brethren, we were comforted over you in all our distress and affliction through your faith:
8kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
8for now we live, if ye stand fast in the Lord.
9Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
9For what thanksgiving can we render again unto God for you, for all the joy wherewith we joy for your sakes before our God;
10Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
10night and day praying exceedingly that we may see your face, and may perfect that which is lacking in your faith?
11Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
11Now may our God and Father himself, and our Lord Jesus, direct our way unto you:
12Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
12and the Lord make you to increase and abound in love one toward another, and toward all men, even as we also [do] toward you;
13Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.
13to the end he may establish your hearts unblameable in holiness before our God and Father, at the coming of our Lord Jesus with all his saints.