1Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
1But I determined this for myself, that I would not come again to you with sorrow.
2Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
2For if I make you sorry, who then is he that maketh me glad but he that is made sorry by me?
3Ndiyo maana niliwaandikia--sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
3And I wrote this very thing, lest, when I came, I should have sorrow from them of whom I ought to rejoice; having confidence in you all, that my joy is [the joy] of you all.
4Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
4For out of much affliction and anguish of heart I wrote unto you with many tears; not that ye should be made sorry, but that ye might know the love that I have more abundantly unto you.
5Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi--ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
5But if any hath caused sorrow, he hath caused sorrow, not to me, but in part (that I press not too heavily) to you all.
6Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
6Sufficient to such a one is this punishment which was [inflicted] by the many;
7Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
7so that contrariwise ye should rather forgive him and comfort him, lest by any means such a one should be swallowed up with his overmuch sorrow.
8Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
8Wherefore I beseech you to confirm [your] love toward him.
9Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
9For to this end also did I write, that I might know the proof of you, whether ye are obedient in all things.
10Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe--kama kweli ninacho cha kusamehe--nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
10But to whom ye forgive anything, I [forgive] also: for what I also have forgiven, if I have forgiven anything, for your sakes [have I forgiven it] in the presence of Christ;
11ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
11that no advantage may be gained over us by Satan: for we are not ignorant of his devices.
12Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
12Now when I came to Troas for the gospel of Christ, and when a door was opened unto me in the Lord,
13Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
13I had no relief for my spirit, because I found not Titus my brother: but taking my leave of them, I went forth into Macedonia.
14Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
14But thanks be unto God, who always leadeth us in triumph in Christ, and maketh manifest through us the savor of his knowledge in every place.
15Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
15For we are a sweet savor of Christ unto God, in them that are saved, and in them that perish;
16Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
16to the one a savor from death unto death; to the other a savor from life unto life. And who is sufficient for these things?
17Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.
17For we are not as the many, corrupting the word of God: but as of sincerity, but as of God, in the sight of God, speak we in Christ.