Swahili: New Testament

American Standard Version

2 Corinthians

8

1Ndugu, tunapenda kuwapa habari juu ya neema ambazo Mungu ameyajalia makanisa ya Makedonia.
1Moreover, brethren, we make known to you the grace of God which hath been given in the churches of Macedonia;
2Waumini wa huko walijaribiwa sana kwa taabu; lakini furaha yao ilikuwa kubwa hivi hata wakawa wakarimu kupita kiasi, ingawaje walikuwa maskini sana.
2how that in much proof of affliction the abundance of their joy and their deep poverty abounded unto the riches of their liberality.
3Naweza kushuhudia kwamba walikuwa wakarimu kadiri ya nguvu zao na hata zaidi. Kwa hiari yao wenyewe,
3For according to their power, I bear witness, yea and beyond their power, [they gave] of their own accord,
4walitusihi sana wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu.
4beseeching us with much entreaty in regard of this grace and the fellowship in the ministering to the saints:
5Hilo lilikuwa jambo ambalo hatukulitazamia kabisa! Kwanza walijitolea wao wenyewe kwa Bwana, kisha wakajitolea wenyewe kwetu pia, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
5and [this], not as we had hoped, but first they gave their own selves to the Lord, and to us through the will of God.
6Kwa sababu hiyo, tulimsihi Tito aliyeianza kazi hiyo awasaidieni pia muitekeleze huduma hii ya upendo miongoni mwenu.
6Insomuch that we exhorted Titus, that as he made a beginning before, so he would also complete in you this grace also.
7Ninyi mna kila kitu: imani, uwezo wa kusema, elimu; bidii yote ya kutenda mema, na upendo wenu kwetu. Hivyo, tunatazamia muwe wakarimu katika huduma hii ya upendo.
7But as ye abound in everything, [in] faith, and utterance, and knowledge, and [in] all earnestness, and [in] your love to us, [see] that ye abound in this grace also.
8Siwapi ninyi amri, lakini nataka tu kuonyesha jinsi wengine walivyo na bidii ya kusaidia ili nipate kujua jinsi upendo wenu ulivyo wa kweli.
8I speak not by way of commandment, but as proving through the earnestness of others the sincerity also of your love.
9Maana, ninyi mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo: yeye, ingawa alikuwa na kila kitu, alijifanya maskini kwa ajili yenu, ili kutokana na umaskini wake, awatajirishe.
9For ye know the grace of our Lord Jesus Christ, that, though he was rich, yet for your sakes he became poor, that ye through his poverty might become rich.
10Kuhusu jambo hili, basi, nawapeni shauri hili: inafaa kwenu kutekeleza sasa yale mliyoanza mwaka jana. Ninyi mlikuwa wa kwanza kuchukua hatua na kuamua kufanya hivyo.
10And herein I give [my] judgment: for this is expedient for you, who were the first to make a beginning a year ago, not only to do, but also to will.
11Basi, kamilisheni shughuli hiyo; na kama vile mlivyokuwa na hamu kubwa ya kusaidia, basi, fanyeni bidii vivyo hivyo, kadiri ya uwezo wenu, kuikamilisha.
11But now complete the doing also; that as [there was] the readiness to will, so [there may be] the completion also out of your ability.
12Maana ikiwa mtu ana moyo wa kusaidia, Mungu hupokea kila anachoweza kutoa: hadai zaidi.
12For if the readiness is there, [it is] acceptable according as [a man] hath, not according as [he] hath not.
13Ninyi hampaswi kuongezewa taabu kusudi wengine wapunguziwe mzigo wao; sivyo, ila ni lazima tujali usawa na haki.
13For [I say] not [this] that others may be eased [and] ye distressed;
14Kila mlicho nacho sasa cha ziada kiwasaidie wale wanaohitaji, ili nao wakati watakapokuwa na ziada, wawasaidie ninyi katika mahitaji yenu, na hivyo kuwe na usawa.
14but by equality: your abundance [being a supply] at this present time for their want, that their abundance also may become [a supply] for your want; that there may be equality:
15Kama Maandiko yasemavyo: "Aliyekusanya kwa wingi hakuwa na ziada, na yule aliyekusanya kidogo hakupungukiwa."
15as it is written, He that [gathered] much had nothing over; and he that [gathered] little had no lack.
16Namshukuru Mungu aliyeweka ndani ya moyo wa Tito hamu hiyo niliyo nayo mimi ya kuwasaidia.
16But thanks be to God, who putteth the same earnest care for you into the heart of Titus.
17Si tu kwamba alikubali ombi letu, ila pia alikuwa na hamu kubwa ya kusaidia, hata akaamua kwa hiari yake mwenyewe kuja kwenu.
17For he accepted indeed our exhortation; but being himself very earnest, he went forth unto you of his own accord.
18Pamoja naye, tunamtuma ndugu mmoja ambaye sifa zake katika kueneza Habari Njema zimeenea katika makanisa yote.
18And we have sent together with him the brother whose praise in the gospel [is spread] through all the churches;
19Zaidi ya hayo, yeye amechaguliwa na makanisa awe mwenzetu safarini wakati tunapopeleka huduma hii yetu ya upendo, huduma tunayoifanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana na uthibitisho wa nia yetu njema.
19and not only so, but who was also appointed by the churches to travel with us in [the matter of] this grace, which is ministered by us to the glory of the Lord, and [to show] our readiness:
20Tunataka kuepa lawama zinazoweza kutokea kuhusu usimamizi wetu juu ya zawadi hii karimu.
20Avoiding this, that any man should blame us in [the matter of] this bounty which is ministered by us:
21Nia yetu ni kufanya vema, si tu mbele ya Bwana, lakini pia mbele ya watu.
21for we take thought for things honorable, not only in the sight of the Lord, but also in the sight of men.
22Basi, pamoja na ndugu hao, tumemtuma ndugu yetu mwingine ambaye mara nyingi tumempa majaribio mbalimbali, tukamwona kuwa ni mwenye hamu kubwa ya kusaidia; hata sasa amekuwa na moyo zaidi kwa sababu ana imani sana nanyi.
22and we have sent with them our brother, whom we have many times proved earnest in many things, but now much more earnest, by reason of the great confidence which [he hath] in you.
23Tito ni mwenzangu; tunafanya kazi pamoja kwa ajili yenu; lakini kuhusu hawa ndugu zetu wengine, wanaokuja pamoja nao, hao ni wajumbe wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
23Whether [any inquire] about Titus, [he is] my partner and [my] fellow-worker to you-ward, or our brethren, [they are] the messengers of the churches, [they are] the glory of Christ.
24Basi, waonyesheni uthabiti wa upendo wenu, makanisa yapate kuona kweli kwamba fahari ninayoona juu yenu ni ya halali.
24Show ye therefore unto them in the face of the churches the proof of your love, and of our glorying on your behalf.