Swahili: New Testament

American Standard Version

2 Thessalonians

3

1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
1Finally, brethren, pray for us, that the word of the Lord may run and be glorified, even as also [it is] with you;
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
2and that we may be delivered from unreasonable and evil men; for all have not faith.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
3But the Lord is faithful, who shall establish you, and guard you from the evil [one].
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
4And we have confidence in the Lord touching you, that ye both do and will do the things which we command.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
5And the Lord direct your hearts into the love of God, and into the patience of Christ.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
6Now we command you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, that ye withdraw yourselves from every brother that walketh disorderly, and not after the tradition which they received of us.
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
7For yourselves know how ye ought to imitate us: for we behaved not ourselves disorderly among you;
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
8neither did we eat bread for nought at any man's hand, but in labor and travail, working night and day, that we might not burden any of you:
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
9not because we have not the right, but to make ourselves and ensample unto you, that ye should imitate us.
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
10For even when we were with you, this we commanded you, If any will not work, neither let him eat.
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
11For we hear of some that walk among you disorderly, that work not at all, but are busybodies.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
12Now them that are such we command and exhort in the Lord Jesus Christ, that with quietness they work, and eat their own bread.
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
13But ye, brethren, be not weary in well-doing.
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
14And if any man obeyeth not our word by this epistle, note that man, that ye have no company with him, to the end that he may be ashamed.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
15And [yet] count him not as an enemy, but admonish him as a brother.
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
16Now the Lord of peace himself give you peace at all times in all ways. The Lord be with you all.
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
17The salutation of me Paul with mine own hand, which is the token in every epistle: so I write.
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
18The grace of our Lord Jesus Christ be with you all.