Swahili: New Testament

American Standard Version

2 Timothy

4

1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
1I charge [thee] in the sight of God, and of Christ Jesus, who shall judge the living and the dead, and by his appearing and his kingdom:
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
2preach the word; be urgent in season, out of season; reprove, rebuke, exhort, with all longsuffering and teaching.
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
3For the time will come when they will not endure the sound doctrine; but, having itching ears, will heap to themselves teachers after their own lusts;
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
4and will turn away their ears from the truth, and turn aside unto fables.
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
5But be thou sober in all things, suffer hardship, do the work of an evangelist, fulfil thy ministry.
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
6For I am already being offered, and the time of my departure is come.
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
7I have fought the good fight, I have finished the course, I have kept the faith:
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
8henceforth there is laid up for me the crown of righteousness, which the Lord, the righteous judge, shall give to me at that day; and not to me only, but also to all them that have loved his appearing.
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
9Give diligence to come shortly unto me:
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
10for Demas forsook me, having loved this present world, and went to Thessalonica; Crescens to Galatia, Titus to Dalmatia.
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
11Only Luke is with me. Take Mark, and bring him with thee; for he is useful to me for ministering.
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
12But Tychicus I sent to Ephesus.
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
13The cloak that I left at Troas with Carpus, bring when thou comest, and the books, especially the parchments.
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
14Alexander the coppersmith did me much evil: the Lord will render to him according to his works:
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
15of whom do thou also beware; for he greatly withstood our words.
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
16At my first defence no one took my part, but all forsook me: may it not be laid to their account.
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
17But the Lord stood by me, and strengthened me; that through me the message might me fully proclaimed, and that all the Gentiles might hear: and I was delivered out of the mouth of the lion.
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
18The Lord will deliver me from every evil work, and will save me unto his heavenly kingdom: to whom [be] the glory forever and ever. Amen.
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
19Salute Prisca and Aquila, and the house of Onesiphorus.
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
20Erastus remained at Corinth: but Trophimus I left at Miletus sick.
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
21Give diligence to come before winter. Eubulus saluteth thee, and Pudens, and Linus, and Claudia, and all the brethren.
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.
22The Lord be with thy spirit. Grace be with you.