Swahili: New Testament

American Standard Version

Acts

2

1Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
1And when the day of Pentecost was now come, they were all together in one place.
2Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
2And suddenly there came from heaven a sound as of the rushing of a mighty wind, and it filled all the house where they were sitting.
3Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
3And there appeared unto them tongues parting asunder, like as of fire; and it sat upon each one of them.
4Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
4And they were all filled with the Holy Spirit, and began to speak with other tongues, as the Spirit gave them utterance.
5Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
5Now there were dwelling at Jerusalem Jews, devout men, from every nation under heaven.
6Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
6And when this sound was heard, the multitude came together, and were confounded, because that every man heard them speaking in his own language.
7Walistaajabu na kushangaa, wakisema, "Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
7And they were all amazed and marvelled, saying, Behold, are not all these that speak Galilaeans?
8Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
8And how hear we, every man in our own language wherein we were born?
9Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
9Parthians and Medes and Elamites, and the dwellers in Mesopotamia, in Judaea and Cappadocia, in Pontus and Asia,
10Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
10in Phrygia and Pamphylia, in Egypt and the parts of Libya about Cyrene, and sojourners from Rome, both Jews and proselytes,
11Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu."
11Cretans and Arabians, we hear them speaking in our tongues the mighty works of God.
12Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, "Hii ina maana gani?"
12And they were all amazed, and were perplexed, saying one to another, What meaneth this?
13Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, "Watu hawa wamelewa divai mpya!"
13But others mocking said, They are filled with new wine.
14Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: "Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
14But Peter, standing up with the eleven, lifted up his voice, and spake forth unto them, [saying], Ye men of Judaea, and all ye that dwell at Jerusalem, be this known unto you, and give ear unto my words.
15Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
15For these are not drunken, as ye suppose; seeing it is [but] the third hour of the day.
16Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
16but this is that which hath been spoken through the prophet Joel:
17Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
17And it shall be in the last days, saith God, I will pour forth of my Spirit upon all flesh: And your sons and your daughters shall prophesy, And your young men shall see visions, And your old men shall dream dreams:
18Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
18Yea and on my servants and on my handmaidens in those days Will I pour forth of my Spirit; and they shall prophesy.
19Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
19And I will show wonders in the heaven above, And signs on the earth beneath; Blood, and fire, and vapor of smoke:
20jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
20The sun shall be turned into darkness, And the moon into blood, Before the day of the Lord come, That great and notable [day].
21Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
21And it shall be, that whosoever shall call on the name of the Lord shall be saved.
22"Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
22Ye men of Israel, hear these words: Jesus of Nazareth, a man approved of God unto you by mighty works and wonders and signs which God did by him in the midst of you, even as ye yourselves know;
23Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
23him, being delivered up by the determinate counsel and foreknowledge of God, ye by the hand of lawless men did crucify and slay:
24Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
24whom God raised up, having loosed the pangs of death: because it was not possible that he should be holden of it.
25Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
25For David saith concerning him, I beheld the Lord always before my face; For he is on my right hand, that I should not be moved:
26Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
26Therefore my heart was glad, and my tongue rejoiced; Moreover my flesh also shall dwell in hope:
27kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.
27Because thou wilt not leave my soul unto Hades, Neither wilt thou give thy Holy One to see corruption.
28Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
28Thou madest known unto me the ways of life; Thou shalt make me full of gladness with thy countenance.
29"Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
29Brethren, I may say unto you freely of the patriarch David, that he both died and was buried, and his tomb is with us unto this day.
30Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
30Being therefore a prophet, and knowing that God had sworn with an oath to him, that of the fruit of his loins he would set [one] upon his throne;
31Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza.
31he foreseeing [this] spake of the resurrection of the Christ, that neither was he left unto Hades, nor did his flesh see corruption.
32Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
32This Jesus did God raise up, whereof we all are witnesses.
33Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
33Being therefore by the right hand of God exalted, and having received of the Father the promise of the Holy Spirit, he hath poured forth this, which ye see and hear.
34Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
34For David ascended not into the heavens: but he saith himself, The Lord said unto my Lord, Sit thou on my right hand,
35hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
35Till I make thine enemies the footstool of thy feet.
36"Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo."
36Let all the house of Israel therefore know assuredly, that God hath made him both Lord and Christ, this Jesus whom ye crucified.
37Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: "Ndugu zetu, tufanye nini?"
37Now when they heard [this,] they were pricked in their heart, and said unto Peter and the rest of the apostles, Brethren, what shall we do?
38Petro akajibu, "Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
38And Peter [said] unto them, Repent ye, and be baptized every one of you in the name of Jesus Christ unto the remission of your sins; and ye shall receive the gift of the Holy Spirit.
39Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake."
39For to you is the promise, and to your children, and to all that are afar off, [even] as many as the Lord our God shall call unto him.
40Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, "Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu."
40And with many other words he testified, and exhorted them, saying, Save yourselves from this crooked generation.
41Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
41They then that received his word were baptized: and there were added [unto them] in that day about three thousand souls.
42Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
42And they continued stedfastly in the apostles' teaching and fellowship, in the breaking of bread and the prayers.
43Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
43And fear came upon every soul: and many wonders and signs were done through the apostles.
44Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
44And all that believed were together, and had all things common;
45Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
45and they sold their possessions and goods, and parted them to all, according as any man had need.
46Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
46And day by day, continuing stedfastly with one accord in the temple, and breaking bread at home, they took their food with gladness and singleness of heart,
47Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.
47praising God, and having favor with all the people. And the Lord added to them day by day those that were saved.