Swahili: New Testament

American Standard Version

Colossians

4

1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
1Masters, render unto your servants that which is just and equal; knowing that ye also have a Master in heaven.
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
2Continue stedfastly in prayer, watching therein with thanksgiving;
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
3withal praying for us also, that God may open unto us a door for the word, to speak the mystery of Christ, for which I am also in bonds;
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
4that I may make it manifest, as I ought to speak.
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
5Walk in wisdom toward them that are without, redeeming the time.
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
6Let your speech be always with grace, seasoned with salt, that ye may know how ye ought to answer each one.
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
7All my affairs shall Tychicus make known unto you, the beloved brother and faithful minister and fellow-servant in the Lord:
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
8whom I have sent you for this very purpose, that ye may know our state, and that he may comfort your hearts;
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
9together with Onesimus, the faithful and beloved brother, who is one of you. They shall make known unto you all things that [are done] here.
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
10Aristarchus my fellow-prisoner saluteth you, and Mark, the cousin of Barnabas (touching whom ye received commandments; if he come unto you, receive him),
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
11and Jesus that is called Justus, who are of the circumcision: these only [are my] fellow-workers unto the kingdom of God, men that have been a comfort unto me.
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
12Epaphras, who is one of you, a servant of Christ Jesus, saluteth you, always striving for you in his prayers, that ye may stand perfect and fully assured in all the will of God.
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
13For I bear him witness, that he hath much labor for you, and for them in Laodicea, and for them in Hierapolis.
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
14Luke, the beloved physician, and Demas salute you.
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
15Salute the brethren that are in Laodicea, and Nymphas, and the church that is in their house.
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
16And when this epistle hath been read among you, cause that it be read also in the church of the Laodiceans; and that ye also read the epistle from Laodicea.
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
17And say to Archippus, Take heed to the ministry which thou hast received in the Lord, that thou fulfil it.
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.
18The salutation of me Paul with mine own hand. Remember my bonds. Grace be with you.