Swahili: New Testament

American Standard Version

Galatians

1

1Mimi Paulo mtume,
1Paul, an apostle (not from men, neither through man, but through Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead),
2na ndugu wote walio pamoja nami, tunayaandikia makanisa yaliyoko Galatia. Mimi nimepata kuwa mtume si kutokana na mamlaka ya binadamu, wala si kwa nguvu ya mtu, bali kwa uwezo wa Yesu Kristo na wa Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka wafu.
2and all the brethren that are with me, unto the churches of Galatia:
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
3Grace to you and peace from God the Father, and our Lord Jesus Christ,
4Kristo alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba, ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu mbaya wa sasa.
4who gave himself for our sins, that he might deliver us out of this present evil world, according to the will of our God and Father:
5Kwake yeye uwe utukufu milele! Amina.
5to whom [be] the glory for ever and ever. Amen.
6Nashangaa kwamba muda mfupi tu umepita, nanyi mnamwasi yule aliyewaita kwa neema ya Kristo, mkafuata Habari Njema ya namna nyingine.
6I marvel that ye are so quickly removing from him that called you in the grace of Christ unto a different gospel;
7Lakini hakuna "Habari Njema" nyingine. Ukweli ni kwamba wako watu wanaowavurugeni, watu wanaotaka kuipotosha Habari Njema ya Kristo.
7which is not another [gospel] only there are some that trouble you, and would pervert the gospel of Christ.
8Lakini, hata kama mmoja wetu au malaika kutoka mbinguni, atawahubirieni Habari Njema tofauti na ile tuliyowahubirieni sisi, basi huyo na alaaniwe!
8But though we, or an angel from heaven, should preach unto you any gospel other than that which we preached unto you, let him be anathema.
9Tulikwisha sema, na sasa nasema tena: kama mtu yeyote anawahubirieni Habari Njema ya aina nyingine, tofauti na ile mliyokwisha pokea, huyo na alaaniwe!
9As we have said before, so say I now again, if any man preacheth unto you any gospel other than that which ye received, let him be anathema.
10Sasa nataka kibali cha nani: cha binadamu, ama cha Mungu? Au je, nataka kuwapendeza watu? Kama ningefanya hivyo, mimi singekuwa kamwe mtumishi wa Kristo.
10For am I now seeking the favor of men, or of God? or am I striving to please men? if I were still pleasing men, I should not be a servant of Christ.
11Ndugu, napenda mfahamu kwamba ile Habari Njema niliyoihubiri si ujumbe wa kibinadamu.
11For I make known to you, brethren, as touching the gospel which was preached by me, that it is not after man.
12Wala mimi sikuipokea kutoka kwa binadamu, wala sikufundishwa na mtu. Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyenifunulia.
12For neither did I receive it from man, nor was I taught it, but [it came to me] through revelation of Jesus Christ.
13Bila shaka mlikwisha sikia jinsi nilivyokuwa ninaishi zamani kwa kuzingatia dini ya Kiyahudi, na jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kupita kiasi na kutaka kuliharibu kabisa.
13For ye have heard of my manner of life in time past in the Jews' religion, how that beyond measure I persecuted the church of God, and made havoc of it:
14Naam, mimi niliwashinda wengi wa wananchi wenzangu wa rika langu katika kuizingatia dini ya Kiyahudi, nikajitahidi sana kuyashika mapokeo ya wazee wetu.
14and I advanced in the Jews' religion beyond many of mine own age among my countrymen, being more exceedingly zealous for the traditions of my fathers.
15Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.
15But when it was the good pleasure of God, who separated me, [even] from my mother's womb, and called me through his grace,
16Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanae kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,
16to reveal his Son in me, that I might preach him among the Gentiles; straightway I conferred not with flesh and blood:
17na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.
17neither went I up to Jerusalem to them that were apostles before me: but I went away into Arabia; and again I returned unto Damascus.
18Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.
18Then after three years I went up to Jerusalem to visit Cephas, and tarried with him fifteen days.
19Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
19But other of the apostles saw I none, save James the Lord's brother.
20Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.
20Now touching the things which I write unto you, behold, before God, I lie not.
21Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.
21Then I came unto the regions of Syria and Cilicia.
22Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.
22And I was still unknown by face unto the churches of Judaea which were in Christ:
23Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: "Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza."
23but they only heard say, He that once persecuted us now preacheth the faith of which he once made havoc;
24Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
24and they glorified God in me.