1Endeleeni kupendana kidugu.
1Let love of the brethren continue.
2Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
2Forget not to show love unto strangers: for thereby some have entertained angels unawares.
3Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
3Remember them that are in bonds, as bound with them; them that are illtreated, as being yourselves also in the body.
4Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
4[Let] marriage [be] had in honor among all, and [let] the bed [be] undefiled: for fornicators and adulterers God will judge.
5Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa."
5Be ye free from the love of money; content with such things as ye have: for himself hath said, I will in no wise fail thee, neither will I in any wise forsake thee.
6Ndiyo maana tunathubutu kusema: "Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?"
6So that with good courage we say, The Lord is my helper; I will not fear: What shall man do unto me?
7wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
7Remember them that had the rule over you, men that spake unto you the word of God; and considering the issue of their life, imitate their faith.
8Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele.
8Jesus Christ [is] the same yesterday and to-day, [yea] and for ever.
9Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
9Be not carried away by divers and strange teachings: for it is good that the heart be established by grace; not by meats, wherein they that occupied themselves were not profited.
10Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
10We have an altar, whereof they have no right to eat that serve the tabernacle.
11Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
11For the bodies of those beasts whose blood is brought into the holy place by the high priest [as an offering] for sin, are burned without the camp.
12Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
12Wherefore Jesus also, that he might sanctify the people through his own blood, suffered without the gate.
13Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
13Let us therefore go forth unto him without the camp, bearing his reproach.
14Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
14For we have not here an abiding city, but we seek after [the city] which is to come.
15Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
15Through him then let us offer up a sacrifice of praise to God continually, that is, the fruit of lips which make confession to his name.
16Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
16But to do good and to communicate forget not: for with such sacrifices God is well pleased.
17Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
17Obey them that have the rule over you, and submit [to them]: for they watch in behalf of your souls, as they that shall give account; that they may do this with joy, and not with grief: for this [were] unprofitable for you.
18Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
18Pray for us: for we are persuaded that we have a good conscience, desiring to live honorably in all things.
19Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
19And I exhort [you] the more exceedingly to do this, that I may be restored to you the sooner.
20Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele.
20Now the God of peace, who brought again from the dead the great shepherd of the sheep with the blood of an eternal covenant, [even] our Lord Jesus,
21Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.
21make you perfect in every good thing to do his will, working in us that which is well-pleasing in his sight, through Jesus Christ; to whom [be] the glory for ever and ever. Amen.
22Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
22But I exhort you, brethren, bear with the word of exhortation, for I have written unto you in few words.
23Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
23Know ye that our brother Timothy hath been set at liberty; with whom, if he come shortly, I will see you.
24Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
24Salute all them that have the rule over you, and all the saints. They of Italy salute you.
25Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.
25Grace be with you all. Amen.