Swahili: New Testament

American Standard Version

James

4

1Mapigano na magombano yote kati yenu yanatoka wapi? Hutoka katika tamaa zenu mbaya ambazo hupigana daima ndani yenu.
1Whence [come] wars and whence [come] fightings among you? [come they] not hence, [even] of your pleasures that war in your members?
2Mnatamani vitu na kwa vile hamvipati mko tayari kuua; mwatamani sana kupata vitu, lakini hamvipati, hivyo mnagombana na kupigana. Hampati kile mnachotaka kwa sababu hamkiombi kwa Mungu.
2Ye lust, and have not: ye kill, and covet, and cannot obtain: ye fight and war; ye have not, because ye ask not.
3Tena, mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya; mnaomba ili mpate kutosheleza tamaa zenu.
3Ye ask, and receive not, because ye ask amiss, that ye may spend [it] in your pleasures.
4Ninyi ni watu msio na uaminifu kama wazinzi. Je, hamjui kwamba kuwa rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu? Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu.
4Ye adulteresses, know ye not that the friendship of the world is enmity with God? Whosoever therefore would be a friend of the world maketh himself an enemy of God.
5Msifikiri kwamba Maandiko Matakatifu yamesema maneno ya bure, yanaposema: "Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu ana wivu mkubwa."
5Or think ye that the scripture speaketh in vain? Doth the spirit which he made to dwell in us long unto envying?
6Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: "Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu."
6But he giveth more grace. Wherefore [the scripture] saith, God resisteth the proud, but giveth grace to the humble.
7Basi, jiwekeni chini ya Mungu; mpingeni Ibilisi naye atawakimbieni.
7Be subject therefore unto God; but resist the devil, and he will flee from you.
8Mkaribieni Mungu, naye atakuja karibu nanyi. Osheni mikono yenu enyi wakosefu! Safisheni mioyo yenu enyi wanafiki!
8Draw nigh to God, and he will draw nigh to you. Cleanse your hands, ye sinners; and purify your hearts, ye doubleminded.
9Oneni huzuni, lieni na kuomboleza; kicheko chenu na kiwe kilio; na furaha yenu iwe huzuni kubwa.
9Be afflicted, and mourn, and weep: let your laughter be turned to mourning, and your joy to heaviness.
10Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.
10Humble yourselves in the sight of the Lord, and he shall exalt you.
11Ndugu, msilaumiane ninyi kwa ninyi. Anayemlaumu ndugu yake na kumhukumu, huyo huilaumu na kuihukumu Sheria. Kama ukiihukumu Sheria, basi, wewe huitii Sheria, bali waihukumu.
11Speak not one against another, brethren. He that speaketh against a brother, or judgeth his brother, speaketh against the law, and judgeth the law: but if thou judgest the law, thou art not a doer of the law, but a judge.
12Mungu peke yake ndiye mwenye kuweka Sheria na kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi, wewe ni nani hata umhukumu binadamu mwenzako?
12One [only] is the lawgiver and judge, [even] he who is able to save and to destroy: but who art thou that judgest thy neighbor?
13Basi, sasa sikilizeni ninyi mnaosema: "Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani na kukaa huko mwaka mzima tukifanya biashara na kupata faida."
13Come now, ye that say, To-day or to-morrow we will go into this city, and spend a year there, and trade, and get gain:
14Ninyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Ninyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.
14whereas ye know not what shall be on the morrow. What is your life? For ye are a vapor, that appeareth for a little time, and then vanisheth away.
15Mngalipaswa kusema: "Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile."
15For that ye ought to say, If the Lord will, we shall both live, and do this or that.
16Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.
16But now ye glory in your vauntings: all such glorying is evil.
17Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.
17To him therefore that knoweth to do good, and doeth it not, to him it is sin.