1"Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
1I am the true vine, and my Father is the husbandman.
2Yeye huliondoa ndani yangu kila tawi lisilozaa matunda, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.
2Every branch in me that beareth not fruit, he taketh it away: and every [branch] that beareth fruit, he cleanseth it, that it may bear more fruit.
3Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni.
3Already ye are clean because of the word which I have spoken unto you.
4Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipokaa katika mzabibu hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu.
4Abide in me, and I in you. As the branch cannot bear fruit of itself, except it abide in the vine; so neither can ye, except ye abide in me.
5"Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi yake. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo atazaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.
5I am the vine, ye are the branches: He that abideth in me, and I in him, the same beareth much fruit: for apart from me ye can do nothing.
6Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.
6If a man abide not in me, he is cast forth as a branch, and is withered; and they gather them, and cast them into the fire, and they are burned.
7Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.
7If ye abide in me, and my words abide in you, ask whatsoever ye will, and it shall be done unto you.
8Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.
8Herein is my Father glorified, that ye bear much fruit; and [so] shall ye be my disciples.
9Mimi nimewapenda ninyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu.
9Even as the Father hath loved me, I also have loved you: abide ye in my love.
10Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
10If ye keep my commandments, ye shall abide in my love; even as I have kept my Father's commandments, and abide in his love.
11Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.
11These things have I spoken unto you, that my joy may be in you, and [that] your joy may be made full.
12Hii ndiyo amri yangu: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
12This is my commandment, that ye love one another, even as I have loved you.
13Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
13Greater love hath no man than this, that a man lay down his life for his friends.
14Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.
14Ye are my friends, if ye do the things which I command you.
15Ninyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita ninyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.
15No longer do I call you servants; for the servant knoweth not what his lord doeth: but I have called you friends; for all things that I heard from my Father, I have made known unto you.
16Ninyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapa ninyi chochote mumwombacho kwa jina langu.
16Ye did not choose me, but I chose you, and appointed you, that ye should go and bear fruit, and [that] your fruit should abide: that whatsoever ye shall ask of the Father in my name, he may give it you.
17Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: pendaneni.
17These things I command you, that ye may love one another.
18"Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
18If the world hateth you, ye know that it hath hated me before [it hated] you.
19Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi kama watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.
19If ye were of the world, the world would love its own: but because ye are not of the world, but I chose you out of the world, therefore the world hateth you.
20Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.
20Remember the word that I said unto you, A servant is not greater than his lord. If they persecuted me, they will also persecute you; if they kept my word, they will keep yours also.
21Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.
21But all these things will they do unto you for my name's sake, because they know not him that sent me.
22Kama nisingalikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia; lakini sasa hawawezi kujitetea kwamba hawana dhambi.
22If I had not come and spoken unto them, they had not had sin: but now they have no excuse for their sin.
23Anayenichukia mimi, anamchukia na Baba yangu pia.
23He that hateth me hateth my Father also.
24Kama nisingalifanya kwao mambo ambayo hakuna mtu mwingine amekwisha yafanya wasingalikuwa na hatia; lakini sasa wameona niliyoyafanya wakinichukia mimi, wakamchukia na Baba yangu pia.
24If I had not done among them the works which none other did, they had not had sin: but now have they both seen and hated both me and my Father.
25Na hivi ni lazima yatimie yale yaliyoandikwa katika Sheria yao: Wamenichukia bure!
25But [this cometh to pass], that the word may be fulfilled that is written in their law, They hated me without a cause.
26"Atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.
26But when the Comforter is come, whom I will send unto you from the Father, [even] the Spirit of truth, which proceedeth from the Father, he shall bear witness of me:
27Nanyi pia mtanishuhudia kwa kuwa mmekuwa nami tangu mwanzo.
27and ye also bear witness, because ye have been with me from the beginning.