Swahili: New Testament

American Standard Version

John

2

1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
1And the third day there was a marriage in Cana of Galilee; and the mother of Jesus was there:
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
2and Jesus also was bidden, and his disciples, to the marriage.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
3And when the wine failed, the mother of Jesus saith unto him, They have no wine.
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
4And Jesus saith unto her, Woman, what have I to do with thee? mine hour is not yet come.
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
5His mother saith unto the servants, Whatsoever he saith unto you, do it.
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
6Now there were six waterpots of stone set there after the Jews' manner of purifying, containing two or three firkins apiece.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
7Jesus saith unto them, Fill the waterpots with water. And they filled them up to the brim.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
8And he saith unto them, Draw out now, and bear unto the ruler of the feast. And they bare it.
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
9And when the ruler of the feast tasted the water now become wine, and knew not whence it was (but the servants that had drawn the water knew), the ruler of the feast calleth the bridegroom,
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
10and saith unto him, Every man setteth on first the good wine; and when [men] have drunk freely, [then] that which is worse: thou hast kept the good wine until now.
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
11This beginning of his signs did Jesus in Cana of Galilee, and manifested his glory; and his disciples believed on him.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
12After this he went down to Capernaum, he, and his mother, and [his] brethren, and his disciples; and there they abode not many days.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
13And the passover of the Jews was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
14And he found in the temple those that sold oxen and sheep and doves, and the changers of money sitting:
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
15and he made a scourge of cords, and cast all out of the temple, both the sheep and the oxen; and he poured out the changers' money, and overthrew their tables;
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
16and to them that sold the doves he said, Take these things hence; make not my Father's house a house of merchandise.
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
17His disciples remembered that it was written, Zeal for thy house shall eat me up.
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
18The Jews therefore answered and said unto him, What sign showest thou unto us, seeing that thou doest these things?
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
19Jesus answered and said unto them, Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
20The Jews therefore said, Forty and six years was this temple in building, and wilt thou raise it up in three days?
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
21But he spake of the temple of his body.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
22When therefore he was raised from the dead, his disciples remembered that he spake this; and they believed the scripture, and the word which Jesus had said.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
23Now when he was in Jerusalem at the passover, during the feast, many believed on his name, beholding his signs which he did.
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
24But Jesus did not trust himself unto them, for that he knew all men,
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
25and because he needed not that any one should bear witness concerning man; for he himself knew what was in man.