Swahili: New Testament

American Standard Version

John

4

1Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
1When therefore the Lord knew that the Pharisees had heard that Jesus was making and baptizing more disciples than John
2(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
2(although Jesus himself baptized not, but his disciples),
3Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
3he left Judea, and departed again into Galilee.
4na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
4And he must needs pass through Samaria.
5Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
5So he cometh to a city of Samaria, called Sychar, near to the parcel of ground that Jacob gave to his son Joseph:
6Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
6and Jacob's well was there. Jesus therefore, being wearied with his journey, sat thus by the well. It was about the sixth hour.
7Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."
7There cometh a woman of Samaria to draw water: Jesus saith unto her, Give me to drink.
8(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
8For his disciples were gone away into the city to buy food.
9Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
9The Samaritan woman therefore saith unto him, How is it that thou, being a Jew, askest drink of me, who am a Samaritan woman? (For Jews have no dealings with Samaritans.)
10Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."
10Jesus answered and said unto unto her, If thou knewest the gift of God, and who it is that saith to thee, Give me to drink; thou wouldest have asked of him, and he would have given thee living water.
11Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
11The woman saith unto him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: whence then hast thou that living water?
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."
12Art thou greater than our father Jacob, who gave us the well, and drank thereof himself, and his sons, and his cattle?
13Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
13Jesus answered and said unto her, Every one that drinketh of this water shall thirst again:
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."
14but whosoever drinketh of the water that I shall give him shall never thirst; but the water that I shall give him shall become in him a well of water springing up unto eternal life.
15Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."
15The woman saith unto him, Sir, give me this water, that I thirst not, neither come all the way hither to draw.
16Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."
16Jesus saith unto her, Go, call thy husband, and come hither.
17Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.
17The woman answered and said unto him, I have no husband. Jesus saith unto her, Thou saidst well, I have no husband:
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."
18for thou hast had five husbands; and he whom thou now hast is not thy husband: this hast thou said truly.
19Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
19The woman saith unto him, Sir, I perceive that thou art a prophet.
20Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."
20Our fathers worshipped in this mountain; and ye say, that in Jerusalem is the place where men ought to worship.
21Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
21Jesus saith unto her, Woman, believe me, the hour cometh, when neither in this mountain, nor in Jerusalem, shall ye worship the Father.
22Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
22Ye worship that which ye know not: we worship that which we know; for salvation is from the Jews.
23Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
23But the hour cometh, and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and truth: for such doth the Father seek to be his worshippers.
24Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."
24God is a Spirit: and they that worship him must worship in spirit and truth.
25Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."
25The woman saith unto him, I know that Messiah cometh (he that is called Christ): when he is come, he will declare unto us all things.
26Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."
26Jesus saith unto her, I that speak unto thee am [he].
27Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"
27And upon this came his disciples; and they marvelled that he was speaking with a woman; yet no man said, What seekest thou? or, Why speakest thou with her?
28Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
28So the woman left her waterpot, and went away into the city, and saith to the people,
29"Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"
29Come, see a man, who told me all things that [ever] I did: can this be the Christ?
30Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
30They went out of the city, and were coming to him.
31Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."
31In the mean while the disciples prayed him, saying, Rabbi, eat.
32Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."
32But he said unto them, I have meat to eat that ye know not.
33Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"
33The disciples therefore said one to another, Hath any man brought him [aught] to eat?
34Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
34Jesus saith unto them, My meat is to do the will of him that sent me, and to accomplish his work.
35Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
35Say not ye, There are yet four months, and [then] cometh the harvest? behold, I say unto you, Lift up your eyes, and look on the fields, that they are white already unto harvest.
36Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
36He that reapeth receiveth wages, and gathereth fruit unto life eternal; that he that soweth and he that reapeth may rejoice together.
37Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
37For herein is the saying true, One soweth, and another reapeth.
38Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."
38I sent you to reap that whereon ye have not labored: others have labored, and ye are entered into their labor.
39Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."
39And from that city many of the Samaritans believed on him because of the word of the woman, who testified, He told me all things that [ever] I did.
40Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
40So when the Samaritans came unto him, they besought him to abide with them: and he abode there two days.
41Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
41And many more believed because of his word;
42Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."
42and they said to the woman, Now we believe, not because of thy speaking: for we have heard for ourselves, and know that this is indeed the Saviour of the world.
43Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
43And after the two days he went forth from thence into Galilee.
44Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."
44For Jesus himself testified, that a prophet hath no honor in his own country.
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
45So when he came into Galilee, the Galilaeans received him, having seen all the things that he did in Jerusalem at the feast: for they also went unto the feast.
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
46He came therefore again unto Cana of Galilee, where he made the water wine. And there was a certain nobleman, whose son was sick at Capernaum.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
47When he heard that Jesus was come out of Judaea into Galilee, he went unto him, and besought [him] that he would come down, and heal his son; for he was at the point of death.
48Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
48Jesus therefore said unto him, Except ye see signs and wonders, ye will in no wise believe.
49Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."
49The nobleman saith unto him, Sir, come down ere my child die.
50Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
50Jesus saith unto him, Go thy way; thy son liveth. The man believed the word that Jesus spake unto him, and he went his way.
51Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
51And as he was now going down, his servants met him, saying, that his son lived.
52Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."
52So he inquired of them the hour when he began to amend. They said therefore unto him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
53Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
53So the father knew that [it was] at that hour in which Jesus said unto him, Thy son liveth: and himself believed, and his whole house.
54Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.
54This is again the second sign that Jesus did, having come out of Judaea into Galilee.