Swahili: New Testament

American Standard Version

John

6

1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
1After these things Jesus went away to the other side of the sea of Galilee, which is [the sea] of Tiberias.
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
2And a great multitude followed him, because they beheld the signs which he did on them that were sick.
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
3And Jesus went up into the mountain, and there he sat with his disciples.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
4Now the passover, the feast of the Jews, was at hand.
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
5Jesus therefore lifting up his eyes, and seeing that a great multitude cometh unto him, saith unto Philip, Whence are we to buy bread, that these may eat?
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
6And this he said to prove him: for he himself knew what he would do.
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
7Philip answered him, Two hundred shillings' worth of bread is not sufficient for them, that every one may take a little.
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
8One of his disciples, Andrew, Simon Peter's brother, saith unto him,
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
9There is a lad here, who hath five barley loaves, and two fishes: but what are these among so many?
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
10Jesus said, Make the people sit down. Now there was much grass in the place. So the men sat down, in number about five thousand.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
11Jesus therefore took the loaves; and having given thanks, he distributed to them that were set down; likewise also of the fishes as much as they would.
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
12And when they were filled, he saith unto his disciples, Gather up the broken pieces which remain over, that nothing be lost.
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
13So they gathered them up, and filled twelve baskets with broken pieces from the five barley loaves, which remained over unto them that had eaten.
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
14When therefore the people saw the sign which he did, they said, This is of a truth the prophet that cometh into the world.
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
15Jesus therefore perceiving that they were about to come and take him by force, to make him king, withdrew again into the mountain himself alone.
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
16And when evening came, his disciples went down unto the sea;
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
17and they entered into a boat, and were going over the sea unto Capernaum. And it was now dark, and Jesus had not yet come to them.
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
18And the sea was rising by reason of a great wind that blew.
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
19When therefore they had rowed about five and twenty or thirty furlongs, they behold Jesus walking on the sea, and drawing nigh unto the boat: and they were afraid.
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
20But he saith unto them, It is I; be not afraid.
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
21They were willing therefore to receive him into the boat: and straightway the boat was at the land whither they were going.
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
22On the morrow the multitude that stood on the other side of the sea saw that there was no other boat there, save one, and that Jesus entered not with his disciples into the boat, but [that] his disciples went away alone
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
23(howbeit there came boats from Tiberias nigh unto the place where they ate the bread after the Lord had given thanks):
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
24when the multitude therefore saw that Jesus was not there, neither his disciples, they themselves got into the boats, and came to Capernaum, seeking Jesus.
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
25And when they found him on the other side of the sea, they said unto him, Rabbi, when camest thou hither?
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
26Jesus answered them and said, Verily, verily, I say unto you, Ye seek me, not because ye saw signs, but because ye ate of the loaves, and were filled.
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
27Work not for the food which perisheth, but for the food which abideth unto eternal life, which the Son of man shall give unto you: for him the Father, even God, hath sealed.
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
28They said therefore unto him, What must we do, that we may work the works of God?
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
29Jesus answered and said unto them, This is the work of God, that ye believe on him whom he hath sent.
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
30They said therefore unto him, What then doest thou for a sign, that we may see, and believe thee? what workest thou?
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
31Our fathers ate the manna in the wilderness; as it is written, He gave them bread out of heaven to eat.
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
32Jesus therefore said unto them, Verily, verily, I say unto you, It was not Moses that gave you the bread out of heaven; but my Father giveth you the true bread out of heaven.
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
33For the bread of God is that which cometh down out of heaven, and giveth life unto the world.
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
34They said therefore unto him, Lord, evermore give us this bread.
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
35Jesus said unto them. I am the bread of life: he that cometh to me shall not hunger, and he that believeth on me shall never thirst.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
36But I said unto you, that ye have seen me, and yet believe not.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
37All that which the Father giveth me shall come unto me; and him that cometh to me I will in no wise cast out.
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
38For I am come down from heaven, not to do mine own will, but the will of him that sent me.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
39And this is the will of him that sent me, that of all that which he hath given me I should lose nothing, but should raise it up at the last day.
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
40For this is the will of my Father, that every one that beholdeth the Son, and believeth on him, should have eternal life; and I will raise him up at the last day.
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
41The Jews therefore murmured concerning him, because he said, I am the bread which came down out of heaven.
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
42And they said, Is not this Jesus, the son of Joseph, whose father and mother we know? how doth he now say, I am come down out of heaven?
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
43Jesus answered and said unto them, Murmur not among yourselves.
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
44No man can come to me, except the Father that sent me draw him: and I will raise him up in the last day.
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
45It is written in the prophets, And they shall all be taught of God. Every one that hath heard from the Father, and hath learned, cometh unto me.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
46Not that any man hath seen the Father, save he that is from God, he hath seen the Father.
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
47Verily, verily, I say unto you, He that believeth hath eternal life.
48Mimi ni mkate wa uzima.
48I am the bread of life.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
49Your fathers ate the manna in the wilderness, and they died.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
50This is the bread which cometh down out of heaven, that a man may eat thereof, and not die.
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
51I am the living bread which came down out of heaven: if any man eat of this bread, he shall live for ever: yea and the bread which I will give is my flesh, for the life of the world.
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
52The Jews therefore strove one with another, saying, How can this man give us his flesh to eat?
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
53Jesus therefore said unto them, Verily, verily, I say unto you, Except ye eat the flesh of the Son of man and drink his blood, ye have not life in yourselves.
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
54He that eateth my flesh and drinketh my blood hath eternal life: and I will raise him up at the last day.
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
55For my flesh is meat indeed, and my blood is drink indeed.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
56He that eateth my flesh and drinketh my blood abideth in me, and I in him.
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
57As the living Father sent me, and I live because of the Father; so he that eateth me, he also shall live because of me.
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
58This is the bread which came down out of heaven: not as the fathers ate, and died; he that eateth this bread shall live for ever.
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
59These things said he in the synagogue, as he taught in Capernaum.
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
60Many therefore of his disciples, when the heard [this], said, This is a hard saying; who can hear it?
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
61But Jesus knowing in himself that his disciples murmured at this, said unto them, Doth this cause you to stumble?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
62[What] then if ye should behold the Son of man ascending where he was before?
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
63It is the spirit that giveth life; the flesh profiteth nothing: the words that I have spoken unto you are spirit, are are life.
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
64But there are some of you that believe not. For Jesus knew from the beginning who they were that believed not, and who it was that should betray him.
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
65And he said, For this cause have I said unto you, that no man can come unto me, except it be given unto him of the Father.
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
66Upon this many of his disciples went back, and walked no more with him.
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
67Jesus said therefore unto the twelve, Would ye also go away?
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
68Simon Peter answered him, Lord, to whom shall we go? thou hast the words of eternal life.
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
69And we have believed and know that thou art the Holy One of God.
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
70Jesus answered them, Did not I choose you the twelve, and one of you is a devil?
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.
71Now he spake of Judas [the son] of Simon Iscariot, for he it was that should betray him, [being] one of the twelve.