Swahili: New Testament

American Standard Version

John

8

1lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
1but Jesus went unto the mount of Olives.
2Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
2And early in the morning he came again into the temple, and all the people came unto him; and he sat down, and taught them.
3Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
3And the scribes and the Pharisees bring a woman taken in adultery; and having set her in the midst,
4Kisha wakamwuliza Yesu, "Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
4they say unto him, Teacher, this woman hath been taken in adultery, in the very act.
5Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?"
5Now in the law Moses commanded us to stone such: what then sayest thou of her?
6Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
6And this they said, trying him, that they might have [whereof] to accuse him. But Jesus stooped down, and with his finger wrote on the ground.
7Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, "Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe."
7But when they continued asking him, he lifted up himself, and said unto them, He that is without sin among you, let him first cast a stone at her.
8Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
8And again he stooped down, and with his finger wrote on the ground.
9Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
9And they, when they heard it, went out one by one, beginning from the eldest, [even] unto the last: and Jesus was left alone, and the woman, where she was, in the midst.
10Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, "Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?"
10And Jesus lifted up himself, and said unto her, Woman, where are they? did no man condemn thee?
11Huyo mwanamke akamjibu, "Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!" Naye Yesu akamwambia, "Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena."
11And she said, No man, Lord. And Jesus said, Neither do I condemn thee: go thy way; from henceforth sin no more.
12Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, "Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima."
12Again therefore Jesus spake unto them, saying, I am the light of the world: he that followeth me shall not walk in the darkness, but shall have the light of life.
13Basi, Mafarisayo wakamwambia, "Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali."
13The Pharisees therefore said unto him, Thou bearest witness of thyself; thy witness is not true.
14Yesu akawajibu, "Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
14Jesus answered and said unto them, Even if I bear witness of myself, my witness is true; for I know whence I came, and whither I go; but ye know not whence I come, or whither I go.
15Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
15Ye judge after the flesh; I judge no man.
16Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
16Yea and if I judge, my judgment is true; for I am not alone, but I and the Father that sent me.
17Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
17Yea and in your law it is written, that the witness of two men is true.
18Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia."
18I am he that beareth witness of myself, and the Father that sent me beareth witness of me.
19Hapo wakamwuliza, "Baba yako yuko wapi?" Yesu akawajibu "Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia."
19They said therefore unto him, Where is thy Father? Jesus answered, Ye know neither me, nor my Father: if ye knew me, ye would know my Father also.
20Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
20These words spake he in the treasury, as he taught in the temple: and no man took him; because his hour was not yet come.
21Yesu akawaambia tena, "Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika."
21He said therefore again unto them, I go away, and ye shall seek me, and shall die in your sin: whither I go, ye cannot come.
22Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, "Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?"
22The Jews therefore said, Will he kill himself, that he saith, Whither I go, ye cannot come?
23Yesu akawaambia, "Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
23And he said unto them, Ye are from beneath; I am from above: ye are of this world; I am not of this world.
24Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu."
24I said therefore unto you, that ye shall die in your sins: for except ye believe that I am [he], ye shall die in your sins.
25Nao wakamwuliza, "Wewe ni nani?" Yesu akawajibu, "Nimewaambieni tangu mwanzo!
25They said therefore unto him, Who art thou? Jesus said unto them, Even that which I have also spoken unto you from the beginning.
26Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake."
26I have many things to speak and to judge concerning you: howbeit he that sent me is true; and the things which I heard from him, these speak I unto the world.
27Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
27They perceived not that he spake to them of the Father.
28Basi, Yesu akawaambia, "Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
28Jesus therefore said, When ye have lifted up the Son of man, then shall ye know that I am [he], and [that] I do nothing of myself, but as the Father taught me, I speak these things.
29Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza."
29And he that sent me is with me; he hath not left me alone; for I do always the things that are pleasing to him.
30Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
30As he spake these things, many believed on him.
31Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, "Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
31Jesus therefore said to those Jews that had believed him, If ye abide in my word, [then] are ye truly my disciples;
32Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru."
32and ye shall know the truth, and the truth shall make you free.
33Nao wakamjibu, "Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?"
33They answered unto him, We are Abraham's seed, and have never yet been in bondage to any man: how sayest thou, Ye shall be made free?
34Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
34Jesus answered them, Verily, verily, I say unto you, Every one that committeth sin is the bondservant of sin.
35Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu.
35And the bondservant abideth not in the house for ever: the son abideth for ever.
36Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
36If therefore the Son shall make you free, ye shall be free indeed.
37Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
37I know that ye are Abraham's seed: yet ye seek to kill me, because my word hath not free course in you.
38Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu."
38I speak the things which I have seen with [my] Father: and ye also do the things which ye heard from [your] father.
39Wao wakamjibu, "Baba yetu ni Abrahamu!" Yesu akawaambia, "Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
39They answered and said unto him, Our father is Abraham. Jesus saith unto them, If ye were Abraham's children, ye would do the works of Abraham.
40Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
40But now ye seek to kill me, a man that hath told you the truth, which I heard from God: this did not Abraham.
41Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu." Wao wakamwambia, "Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu."
41Ye do the works of your father. They said unto him, We were not born of fornication; we have one Father, [even] God.
42Yesu akawaambia, "Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
42Jesus said unto them, If God were your Father, ye would love me: for I came forth and am come from God; for neither have I come of myself, but he sent me.
43Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
43Why do ye not understand my speech? [Even] because ye cannot hear my word.
44Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
44Ye are of [your] father the devil, and the lusts of your father it is your will to do. He was a murderer from the beginning, and standeth not in the truth, because there is no truth in him. When he speaketh a lie, he speaketh of his own: for he is a liar, and the father thereof.
45Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
45But because I say the truth, ye believe me not.
46Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
46Which of you convicteth me of sin? If I say truth, why do ye not believe me?
47Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu."
47He that is of God heareth the words of God: for this cause ye hear [them] not, because ye are not of God.
48Wayahudi wakamwambia, "Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?"
48The Jews answered and said unto him, Say we not well that thou art a Samaritan, and hast a demon?
49Yesu akajibu, "Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
49Jesus answered, I have not a demon; but I honor my Father, and ye dishonor me.
50Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
50But I seek not mine own glory: there is one that seeketh and judgeth.
51Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele."
51Verily, verily, I say unto you, If a man keep my word, he shall never see death.
52Basi, Wayahudi wakasema, "Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele!
52The Jews said unto him, Now we know that thou hast a demon. Abraham died, and the prophets; and thou sayest, If a man keep my word, he shall never taste of death.
53Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?"
53Art thou greater than our father Abraham, who died? and the prophets died: whom makest thou thyself?
54Yesu akawajibu, "Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
54Jesus answered, If I glorify myself, my glory is nothing: it is my Father that glorifieth me; of whom ye say, that he is your God;
55Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
55and ye have not known him: but I know him; and if I should say, I know him not, I shall be like unto you, a liar: but I know him, and keep his word.
56Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi."
56Your father Abraham rejoiced to see my day; and he saw it, and was glad.
57Basi, Wayahudi wakamwambia, "Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?"
57The Jews therefore said unto him, Thou art not yet fifty years old, and hast thou seen Abraham?
58Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko."
58Jesus said unto them, Verily, verily, I say unto you, Before Abraham was born, I am.
59Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.
59They took up stones therefore to cast at him: but Jesus hid himself, and went out of the temple.