Swahili: New Testament

American Standard Version

Luke

19

1Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
1And he entered and was passing through Jericho.
2Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
2And behold, a man called by name Zacchaeus; and he was a chief publican, and he was rich.
3Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
3And he sought to see Jesus who he was; and could not for the crowd, because he was little of stature.
4Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
4And he ran on before, and climbed up into a sycomore tree to see him: for he was to pass that way.
5Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako."
5And when Jesus came to the place, he looked up, and said unto him, Zacchaeus, make haste, and come down; for to-day I must abide at thy house.
6Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
6And he made haste, and came down, and received him joyfully.
7Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, "Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi."
7And when they saw it, they all murmured, saying, He is gone in to lodge with a man that is a sinner.
8Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, "Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne."
8And Zacchaeus stood, and said unto the Lord, Behold, Lord, the half of my goods I give to the poor; and if I have wrongfully exacted aught of any man, I restore fourfold.
9Yesu akamwambia, "Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
9And Jesus said unto him, To-day is salvation come to this house, forasmuch as he also is a son of Abraham.
10Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea."
10For the Son of man came to seek and to save that which was lost.
11Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
11And as they heard these things, he added and spake a parable, because he was nigh to Jerusalem, and [because] they supposed that the kingdom of God was immediately to appear.
12Hivyo akawaambia, "Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
12He said therefore, A certain nobleman went into a far country, to receive for himself a kingdom, and to return.
13Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
13And he called ten servants of his, and gave them ten pounds, and said unto them, Trade ye [herewith] till I come.
14Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
14But his citizens hated him, and sent an ambassage after him, saying, We will not that this man reign over us.
15"Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
15And it came to pass, when he was come back again, having received the kingdom, that he commanded these servants, unto whom he had given the money, to be called to him, that he might know what they had gained by trading.
16Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
16And the first came before him, saying, Lord, thy pound hath made ten pounds more.
17Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
17And he said unto him, Well done, thou good servant: because thou wast found faithful in a very little, have thou authority over ten cities.
18Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
18And the second came, saying, Thy pound, Lord, hath made five pounds.
19Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
19And he said unto him also, Be thou also over five cities.
20"Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
20And another came, saying, Lord, behold, [here is] thy pound, which I kept laid up in a napkin:
21kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
21for I feared thee, because thou art an austere man: thou takest up that which thou layedst not down, and reapest that which thou didst not sow.
22Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
22He saith unto him, Out of thine own mouth will I judge thee, thou wicked servant. Thou knewest that I am an austere man, taking up that which I laid not down, and reaping that which I did not sow;
23Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
23then wherefore gavest thou not my money into the bank, and I at my coming should have required it with interest?
24Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
24And he said unto them that stood by, Take away from him the pound, and give it unto him that hath the ten pounds.
25Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
25And they said unto him, Lord, he hath ten pounds.
26Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
26I say unto you, that unto every one that hath shall be given; but from him that hath not, even that which he hath shall be taken away from him.
27Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu."
27But these mine enemies, that would not that I should reign over them, bring hither, and slay them before me.
28Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
28And when he had thus spoken, he went on before, going up to Jerusalem.
29Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
29And it came to pass, when he drew nigh unto Bethphage and Bethany, at the mount that is called Olivet, he sent two of the disciples,
30akawaambia: "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
30saying, Go your way into the village over against [you]; in which as ye enter ye shall find a colt tied, whereon no man ever yet sat: loose him, and bring him.
31Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye."
31And if any one ask you, Why do ye loose him? thus shall ye say, The Lord hath need of him.
32Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
32And they that were sent went away, and found even as he had said unto them.
33Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, "Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?"
33And as they were loosing the colt, the owners thereof said unto them, Why loose ye the colt?
34Nao wakawajibu, "Bwana anamhitaji."
34And they said, The Lord hath need of him.
35Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
35And they brought him to Jesus: and they threw their garments upon the colt, and set Jesus thereon.
36Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
36And as he went, they spread their garments in the way.
37Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
37And as he was now drawing nigh, [even] at the descent of the mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works which they had seen;
38wakawa wanasema: "Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!"
38saying, Blessed [is] the King that cometh in the name of the Lord: peace in heaven, and glory in the highest.
39Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, "Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!"
39And some of the Pharisees from the multitude said unto him, Teacher, rebuke thy disciples.
40Yesu akawajibu, "Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti."
40And he answered and said, I tell you that, if these shall hold their peace, the stones will cry out.
41Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
41And when he drew nigh, he saw the city and wept over it,
42akisema: "Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
42saying, If thou hadst known in this day, even thou, the things which belong unto peace! but now they are hid from thine eyes.
43Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
43For the days shall come upon thee, when thine enemies shall cast up a bank about thee, and compass thee round, and keep thee in on every side,
44Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa."
44and shall dash thee to the ground, and thy children within thee; and they shall not leave in thee one stone upon another; because thou knewest not the time of thy visitation.
45Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
45And he entered into the temple, and began to cast out them that sold,
46akisema, "Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi."
46saying unto them, It is written, And my house shall be a house of prayer: but ye have made it a den of robbers.
47Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
47And he was teaching daily in the temple. But the chief priests and the scribes and the principal men of the people sought to destroy him:
48lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.
48and they could not find what they might do; for the people all hung upon him, listening.