Swahili: New Testament

American Standard Version

Luke

22

1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
1Now the feast of unleavened bread drew nigh, which is called the Passover.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
2And the chief priests and the scribes sought how they might put him to death; for they feared the people.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
3And Satan entered into Judas who was called Iscariot, being of the number of the twelve.
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
4And he went away, and communed with the chief priests and captains, how he might deliver him unto them.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
5And they were glad, and covenanted to give him money.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
6And he consented, and sought opportunity to deliver him unto them in the absence of the multitude.
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
7And the day of unleavened bread came, on which the passover must be sacrificed.
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
8And he sent Peter and John, saying, Go and make ready for us the passover, that we may eat.
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
9And they said unto him, Where wilt thou that we make ready?
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
10And he said unto them, Behold, when ye are entered into the city, there shall meet you a man bearing a pitcher of water; follow him into the house whereinto he goeth.
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
11And ye shall say unto the master of the house, The Teacher saith unto thee, Where is the guestchamber, where I shall eat the passover with my disciples?
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
12And he will show you a large upper room furnished: there make ready.
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
13And they went, and found as he had said unto them: and they made ready the passover.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
14And when the hour was come, he sat down, and the apostles with him.
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
15And he said unto them, With desire I have desired to eat this passover with you before I suffer:
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
16for I say unto you, I shall not eat it, until it be fulfilled in the kingdom of God.
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
17And he received a cup, and when he had given thanks, he said, Take this, and divide it among yourselves:
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
18for I say unto you, I shall not drink from henceforth of the fruit of the vine, until the kingdom of God shall come.
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
19And he took bread, and when he had given thanks, he brake it, and gave to them, saying, This is my body which is given for you: this do in remembrance of me.
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
20And the cup in like manner after supper, saying, This cup is the new covenant in my blood, [even] that which is poured out for you.
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
21But behold, the hand of him that betrayeth me is with me on the table.
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
22For the Son of man indeed goeth, as it hath been determined: but woe unto that man through whom he is betrayed!
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
23And they began to question among themselves, which of them it was that should do this thing.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
24And there arose also a contention among them, which of them was accounted to be greatest.
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
25And he said unto them, The kings of the Gentiles have lordship over them; and they that have authority over them are called Benefactors.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
26But ye [shall] not [be] so: but he that is the greater among you, let him become as the younger; and he that is chief, as he that doth serve.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
27For which is greater, he that sitteth at meat, or he that serveth? is not he that sitteth at meat? but I am in the midst of you as he that serveth.
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
28But ye are they that have continued with me in my temptations;
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
29and I appoint unto you a kingdom, even as my Father appointed unto me,
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
30that ye may eat and drink at my table in my kingdom; and ye shall sit on thrones judging the twelve tribes of Israel.
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
31Simon, Simon, behold, Satan asked to have you, that he might sift you as wheat:
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
32but I made supplication for thee, that thy faith fail not; and do thou, when once thou hast turned again, establish thy brethren.
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
33And he said unto him, Lord, with thee I am ready to go both to prison and to death.
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
34And he said, I tell thee, Peter, the cock shall not crow this day, until thou shalt thrice deny that thou knowest me.
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
35And he said unto them, When I sent you forth without purse, and wallet, and shoes, lacked ye anything? And they said, Nothing.
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
36And he said unto them, But now, he that hath a purse, let him take it, and likewise a wallet; and he that hath none, let him sell his cloak, and buy a sword.
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
37For I say unto you, that this which is written must be fulfilled in me, And he was reckoned with transgressors: for that which concerneth me hath fulfilment.
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
38And they said, Lord, behold, here are two swords. And he said unto them, It is enough.
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
39And he came out, and went, as his custom was, unto the mount of Olives; and the disciples also followed him.
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
40And when he was at the place, he said unto them, Pray that ye enter not into temptation.
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
41And he was parted from them about a stone's cast; and he kneeled down and prayed,
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
42saying, Father, if thou be willing, remove this cup from me: nevertheless not my will, but thine, be done.
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
43And there appeared unto him an angel from heaven, strengthening him.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
44And being in an agony he prayed more earnestly; and his sweat became as it were great drops of blood falling down upon the ground.
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
45And when he rose up from his prayer, he came unto the disciples, and found them sleeping for sorrow,
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
46and said unto them, Why sleep ye? rise and pray, that ye enter not into temptation.
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
47While he yet spake, behold, a multitude, and he that was called Judas, one of the twelve, went before them; and he drew near unto Jesus to kiss him.
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
48But Jesus said unto him, Judas, betrayest thou the Son of man with a kiss?
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
49And when they that were about him saw what would follow, they said, Lord, shall we smite with the sword?
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
50And a certain one of them smote the servant of the high priest, and struck off his right ear.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
51But Jesus answered and said, Suffer ye [them] thus far. And he touched his ear, and healed him.
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
52And Jesus said unto the chief priests, and captains of the temple, and elders, that were come against him, Are ye come out, as against a robber, with swords and staves?
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
53When I was daily with you in the temple, ye stretched not forth your hands against me: but this is your hour, and the power of darkness.
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
54And they seized him, and led him [away], and brought him into the high priest's house. But Peter followed afar off.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
55And when they had kindled a fire in the midst of the court, and had sat down together, Peter sat in the midst of them.
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
56And a certain maid seeing him as he sat in the light [of the fire], and looking stedfastly upon him, said, This man also was with him.
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
57But he denied, saying, Woman, I know him not.
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
58And after a little while another saw him, and said, Thou also art [one] of them. But Peter said, Man, I am not.
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
59And after the space of about one hour another confidently affirmed, saying, Of a truth this man also was with him; for he is a Galilaean.
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
60But Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he yet spake, the cock crew.
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
61And the Lord turned, and looked upon Peter. And Peter remembered the word of the Lord, how that he said unto him, Before the cock crow this day thou shalt deny me thrice.
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
62And he went out, and wept bitterly.
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
63And the men that held [Jesus] mocked him, and beat him.
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
64And they blindfolded him, and asked him, saying, Prophesy: who is he that struck thee?
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
65And many other things spake they against him, reviling him.
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
66And as soon as it was day, the assembly of the elders of the people was gathered together, both chief priests and scribes; and they led him away into their council, saying,
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
67If thou art the Christ, tell us. But he said unto them, If I tell you, ye will not believe:
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
68and if I ask [you], ye will not answer.
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
69But from henceforth shall the Son of man be seated at the right hand of the power of God.
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
70And they all said, Art thou then the Son of God? And he said unto them, Ye say that I am.
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."
71And they said, What further need have we of witness? for we ourselves have heard from his own mouth.