Swahili: New Testament

American Standard Version

Luke

4

1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
1And Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led in the Spirit in the wilderness
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
2during forty days, being tempted of the devil. And he did eat nothing in those days: and when they were completed, he hungered.
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
3And the devil said unto him, if thou art the Son of God, command this stone that it become bread.
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
4And Jesus answered unto him, It is written, Man shall not live by bread alone.
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
5And he led him up, and showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
6And the devil said unto him, To thee will I give all this authority, and the glory of them: for it hath been delivered unto me; and to whomsoever I will I give it.
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
7If thou therefore wilt worship before me, it shall all be thine.
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
8And Jesus answered and said unto him, It is written, Thou shalt worship the Lord thy God, and him only shalt thou serve.
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
9And he led him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said unto him, If thou art the Son of God, cast thyself down from hence:
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
10for it is written, He shall give his angels charge concerning thee, to guard thee:
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
11and, On their hands they shall bear thee up, Lest haply thou dash thy foot against a stone.
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
12And Jesus answering said unto him, It is said, Thou shalt not make trial of the Lord thy God.
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
13And when the devil had completed every temptation, he departed from him for a season.
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
14And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee: and a fame went out concerning him through all the region round about.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
15And he taught in their synagogues, being glorified of all.
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
16And he came to Nazareth, where he had been brought up: and he entered, as his custom was, into the synagogue on the sabbath day, and stood up to read.
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
17And there was delivered unto him the book of the prophet Isaiah. And he opened the book, and found the place where it was written,
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
18The Spirit of the Lord is upon me, Because he anointed me to preach good tidings to the poor: He hath sent me to proclaim release to the captives, And recovering of sight to the blind, To set at liberty them that are bruised,
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
19To proclaim the acceptable year of the Lord.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
20And he closed the book, and gave it back to the attendant, and sat down: and the eyes of all in the synagogue were fastened on him.
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
21And he began to say unto them, To-day hath this scripture been fulfilled in your ears.
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
22And all bare him witness, and wondered at the words of grace which proceeded out of his mouth: and they said, Is not this Joseph's son?
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
23And he said unto them, Doubtless ye will say unto me this parable, Physician, heal thyself: whatsoever we have heard done at Capernaum, do also here in thine own country.
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
24And he said, Verily I say unto you, No prophet is acceptable in his own country.
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
25But of a truth I say unto you, There were many widows in Israel in the days of Elijah, when the heaven was shut up three years and six months, when there came a great famine over all the land;
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
26and unto none of them was Elijah sent, but only to Zarephath, in the land of Sidon, unto a woman that was a widow.
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
27And there were many lepers in Israel in the time of Elisha the prophet; and none of them was cleansed, but only Naaman the Syrian.
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
28And they were all filled with wrath in the synagogue, as they heard these things;
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
29and they rose up, and cast him forth out of the city, and led him unto the brow of the hill whereon their city was built, that they might throw him down headlong.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
30But he passing through the midst of them went his way.
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
31And he came down to Capernaum, a city of Galilee. And he was teaching them on the sabbath day:
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
32and they were astonished at his teaching; for his word was with authority.
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
33And in the synagogue there was a man, that had a spirit of an unclean demon; and he cried out with a loud voice,
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
34Ah! what have we to do with thee, Jesus thou Nazarene? art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
35And Jesus rebuked him, saying, Hold thy peace, and come out of him. And when the demon had thrown him down in the midst, he came out of him, having done him no hurt.
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
36And amazement came upon all, and they spake together, one with another, saying, What is this word? for with authority and power he commandeth the unclean spirits, and they come out.
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
37And there went forth a rumor concerning him into every place of the region round about.
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
38And he rose up from the synagogue, and entered into the house of Simon. And Simon's wife's mother was holden with a great fever; and they besought him for her.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
39And he stood over her, and rebuked the fever; and it left her: and immediately she rose up and ministered unto them.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
40And when the sun was setting, all they that had any sick with divers diseases brought them unto him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
41And demons also came out from many, crying out, and saying, Thou art the Son of God. And rebuking them, he suffered them not to speak, because they knew that he was the Christ.
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
42And when it was day, he came out and went into a desert place: and the multitudes sought after him, and came unto him, and would have stayed him, that he should not go from them.
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
43But he said unto them, I must preach the good tidings of the kingdom of God to the other cities also: for therefore was I sent.
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.
44And he was preaching in the synagogues of Galilee.