1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
1Now it came to pass on a sabbath, that he was going through the grainfields; and his disciples plucked the ears, and did eat, rubbing them in their hands.
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
2But certain of the Pharisees said, Why do ye that which it is not lawful to do on the sabbath day?
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
3And Jesus answering them said, Have ye not read even this, what David did, when he was hungry, he, and they that were with him;
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
4how he entered into the house of God, and took and ate the showbread, and gave also to them that were with him; which it is not lawful to eat save for the priests alone?
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
5And he said unto them, The Son of man is lord of the sabbath.
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
6And it came to pass on another sabbath, that he entered into the synagogue and taught: and there was a man there, and his right hand was withered.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
7And the scribes and the Pharisees watched him, whether he would heal on the sabbath; that they might find how to accuse him.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
8But he knew their thoughts; and he said to the man that had his hand withered, Rise up, and stand forth in the midst. And he arose and stood forth.
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
9And Jesus said unto them, I ask you, Is it lawful on the sabbath to do good, or to do harm? to save a life, or to destroy it?
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
10And he looked round about on them all, and said unto him, Stretch forth thy hand. And he did [so]: and his hand was restored.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
11But they were filled with madness; and communed one with another what they might do to Jesus.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
12And it came to pass in these days, that he went out into the mountain to pray; and he continued all night in prayer to God.
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
13And when it was day, he called his disciples; and he chose from them twelve, whom also he named apostles:
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
14Simon, whom he also named Peter, and Andrew his brother, and James and John, and Philip and Bartholomew,
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
15and Matthew and Thomas, and James [the son] of Alphaeus, and Simon who was called the Zealot,
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
16and Judas [the son] of James, and Judas Iscariot, who became a traitor;
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
17and he came down with them, and stood on a level place, and a great multitude of his disciples, and a great number of the people from all Judaea and Jerusalem, and the sea coast of Tyre and Sidon, who came to hear him, and to be healed of their diseases;
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
18and they that were troubled with unclean spirits were healed.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
19And all the multitude sought to touch him; for power came forth from him, and healed [them] all.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
20And he lifted up his eyes on his disciples, and said, Blessed [are] ye poor: for yours is the kingdom of God.
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
21Blessed [are] ye that hunger now: for ye shall be filled. Blessed [are] ye that weep now: for ye shall laugh.
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
22Blessed are ye, when men shall hate you, and when they shall separate you [from their company], and reproach you, and cast out your name as evil, for the Son of man's sake.
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
23Rejoice in that day, and leap [for joy]: for behold, your reward is great in heaven; for in the same manner did their fathers unto the prophets.
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
24But woe unto you that are rich! for ye have received your consolation.
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
25Woe unto you, ye that are full now! for ye shall hunger. Woe [unto you], ye that laugh now! for ye shall mourn and weep.
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
26Woe [unto you], when all men shall speak well of you! for in the same manner did their fathers to the false prophets.
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
27But I say unto you that hear, Love your enemies, do good to them that hate you,
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
28bless them that curse you, pray for them that despitefully use you.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
29To him that smiteth thee on the [one] cheek offer also the other; and from him that taketh away thy cloak withhold not thy coat also.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
30Give to every one that asketh thee; and of him that taketh away thy goods ask them not again.
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
31And as ye would that men should do to you, do ye also to them likewise.
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
32And if ye love them that love you, what thank have ye? for even sinners love those that love them.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
33And if ye do good to them that do good to you, what thank have ye? for even sinners do the same.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
34And if ye lend to them of whom ye hope to receive, what thank have ye? even sinners lend to sinners, to receive again as much.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
35But love your enemies, and do [them] good, and lend, never despairing; and your reward shall be great, and ye shall be sons of the Most High: for he is kind toward the unthankful and evil.
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
36Be ye merciful, even as your Father is merciful.
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
37And judge not, and ye shall not be judged: and condemn not, and ye shall not be condemned: release, and ye shall be released:
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
38give, and it shall be given unto you; good measure, pressed down, shaken together, running over, shall they give into your bosom. For with what measure ye mete it shall be measured to you again.
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
39And he spake also a parable unto them, Can the blind guide the blind? shall they not both fall into a pit?
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
40The disciple is not above his teacher: but every one when he is perfected shall be as his teacher.
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
41And why beholdest thou the mote that is in thy brother's eye, but considerest not the beam that is in thine own eye?
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
42Or how canst thou say to thy brother, Brother, let me cast out the mote that is in thine eye, when thou thyself beholdest not the beam that is in thine own eye? Thou hypocrite, cast out first the beam out of thine own eye, and then shalt thou see clearly to cast out the mote that is in thy brother's eye.
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
43For there is no good tree that bringeth forth corrupt fruit; nor again a corrupt tree that bringeth forth good fruit.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
44For each tree is known by its own fruit. For of thorns men do not gather figs, nor of a bramble bush gather they grapes.
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
45The good man out of the good treasure of his heart bringeth forth that which is good; and the evil [man] out of the evil [treasure] bringeth forth that which is evil: for out of the abundance of the heart his mouth speaketh.
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
46And why call ye me, Lord, Lord, and do not the things which I say?
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
47Every one that cometh unto me, and heareth my words, and doeth them, I will show you to whom he is like:
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
48he is like a man building a house, who digged and went deep, and laid a foundation upon the rock: and when a flood arose, the stream brake against that house, and could not shake it: because it had been well builded.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"
49But he that heareth, and doeth not, is like a man that built a house upon the earth without a foundation; against which the stream brake, and straightway it fell in; and the ruin of that house was great.