Swahili: New Testament

American Standard Version

Mark

5

1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
1And they came to the other side of the sea, into the country of the Gerasenes.
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
2And when he was come out of the boat, straightway there met him out of the tombs a man with an unclean spirit,
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
3who had his dwelling in the tombs: and no man could any more bind him, no, not with a chain;
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
4because that he had been often bound with fetters and chains, and the chains had been rent asunder by him, and the fetters broken in pieces: and no man had strength to tame him.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
5And always, night and day, in the tombs and in the mountains, he was crying out, and cutting himself with stones.
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
6And when he saw Jesus from afar, he ran and worshipped him;
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
7and crying out with a loud voice, he saith, What have I to do with thee, Jesus, thou Son of the Most High God? I adjure thee by God, torment me not.
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
8For he said unto him, Come forth, thou unclean spirit, out of the man.
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
9And he asked him, What is thy name? And he saith unto him, My name is Legion; for we are many.
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
10And he besought him much that he would not send them away out of the country.
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
11Now there was there on the mountain side a great herd of swine feeding.
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
12And they besought him, saying, Send us into the swine, that we may enter into them.
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
13And he gave them leave. And the unclean spirits came out, and entered into the swine: and the herd rushed down the steep into the sea, [in number] about two thousand; and they were drowned in the sea.
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
14And they that fed them fled, and told it in the city, and in the country. And they came to see what it was that had come to pass.
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
15And they come to Jesus, and behold him that was possessed with demons sitting, clothed and in his right mind, [even] him that had the legion: and they were afraid.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
16And they that saw it declared unto them how it befell him that was possessed with demons, and concerning the swine.
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
17And they began to beseech him to depart from their borders.
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
18And as he was entering into the boat, he that had been possessed with demons besought him that he might be with him.
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
19And he suffered him not, but saith unto him, Go to thy house unto thy friends, and tell them how great things the Lord hath done for thee, and [how] he had mercy on thee.
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
20And he went his way, and began to publish in Decapolis how great things Jesus had done for him: and all men marvelled.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
21And when Jesus had crossed over again in the boat unto the other side, a great multitude was gathered unto him; and he was by the sea.
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
22And there cometh one of the rulers of the synagogue, Jairus by name; and seeing him, he falleth at his feet,
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
23and beseecheth him much, saying, My little daughter is at the point of death: [I pray thee], that thou come and lay thy hands on her, that she may be made whole, and live.
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
24And he went with him; and a great multitude followed him, and they thronged him.
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
25And a woman, who had an issue of blood twelve years,
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
26and had suffered many things of many physicians, and had spent all that she had, and was nothing bettered, but rather grew worse,
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
27having heard the things concerning Jesus, came in the crowd behind, and touched his garment.
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
28For she said, If I touch but his garments, I shall be made whole.
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
29And straightway the fountain of her blood was dried up; and she felt in her body that she was healed of her plague.
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
30And straightway Jesus, perceiving in himself that the power [proceeding] from him had gone forth, turned him about in the crowd, and said, Who touched my garments?
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
31And his disciples said unto him, Thou seest the multitude thronging thee, and sayest thou, Who touched me?
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
32And he looked round about to see her that had done this thing.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
33But the woman fearing and trembling, knowing what had been done to her, came and fell down before him, and told him all the truth.
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
34And he said unto her, Daughter, thy faith hath made thee whole; go in peace, and be whole of thy plague.
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
35While he yet spake, they come from the ruler of the synagogue's [house] saying, Thy daughter is dead: why troublest thou the Teacher any further?
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
36But Jesus, not heeding the word spoken, saith unto the ruler of the synagogue, Fear not, only believe.
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
37And he suffered no man to follow with him, save Peter, and James, and John the brother of James.
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
38And they come to the house of the ruler of the synagogue; and he beholdeth a tumult, and [many] weeping and wailing greatly.
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
39And when he was entered in, he saith unto them, Why make ye a tumult, and weep? the child is not dead, but sleepeth.
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
40And they laughed him to scorn. But he, having put them all forth, taketh the father of the child and her mother and them that were with him, and goeth in where the child was.
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
41And taking the child by the hand, he saith unto her, Talitha cumi; which is, being interpreted, Damsel, I say unto thee, Arise.
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
42And straightway the damsel rose up, and walked; for she was twelve years old. And they were amazed straightway with a great amazement.
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.
43And he charged them much that no man should know this: and he commanded that [something] should be given her to eat.