1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
1And he entered into a boat, and crossed over, and came into his own city.
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
2And behold, they brought to him a man sick of the palsy, lying on a bed: and Jesus seeing their faith said unto the sick of the palsy, Son, be of good cheer; thy sins are forgiven.
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
3And behold, certain of the scribes said within themselves, This man blasphemeth.
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
4And Jesus knowing their thoughts said, Wherefore think ye evil in your hearts?
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
5For which is easier, to say, Thy sins are forgiven; or to say, Arise, and walk?
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
6But that ye may know that the Son of man hath authority on earth to forgive sins (then saith he to the sick of the palsy), Arise, and take up thy bed, and go up unto thy house.
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
7And he arose, and departed to his house.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
8But when the multitudes saw it, they were afraid, and glorified God, who had given such authority unto men.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
9And as Jesus passed by from thence, he saw a man, called Matthew, sitting at the place of toll: and he saith unto him, Follow me. And he arose, and followed him.
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
10And it came to pass, as he sat at meat in the house, behold, many publicans and sinners came and sat down with Jesus and his disciples.
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
11And when the Pharisees saw it, they said unto his disciples, Why eateth your Teacher with the publicans and sinners?
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
12But when he heard it, he said, They that are whole have no need of a physician, but they that are sick.
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
13But go ye and learn what [this] meaneth, I desire mercy, and not sacrifice, for I came not to call the righteous, but sinners.
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
14Then come to him the disciples of John, saying, Why do we and the Pharisees fast oft, but thy disciples fast not?
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
15And Jesus said unto them, Can the sons of the bridechamber mourn, as long as the bridegroom is with them? but the days will come, when the bridegroom shall be taken away from them, and then will they fast.
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
16And no man putteth a piece of undressed cloth upon an old garment; for that which should fill it up taketh from the garment, and a worse rent is made.
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
17Neither do [men] put new wine into old wine-skins: else the skins burst, and the wine is spilled, and the skins perish: but they put new wine into fresh wine-skins, and both are preserved.
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
18While he spake these things unto them, behold, there came a ruler, and worshipped him, saying, My daughter is even now dead: but come and lay thy hand upon her, and she shall live.
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
19And Jesus arose, and followed him, and [so did] his disciples.
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
20And behold, a woman, who had an issue of blood twelve years, came behind him, and touched the border of his garment:
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
21for she said within herself, If I do but touch his garment, I shall be made whole.
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
22But Jesus turning and seeing her said, Daughter, be of good cheer; thy faith hath made thee whole. And the woman was made whole from that hour.
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
23And when Jesus came into the ruler's house, and saw the flute-players, and the crowd making a tumult,
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
24he said, Give place: for the damsel is not dead, but sleepeth. And they laughed him to scorn.
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
25But when the crowd was put forth, he entered in, and took her by the hand; and the damsel arose.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
26And the fame hereof went forth into all that land.
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
27And as Jesus passed by from thence, two blind men followed him, crying out, and saying, Have mercy on us, thou son of David.
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
28And when he was come into the house, the blind men came to him: and Jesus saith unto them, Believe ye that I am able to do this? They say unto him, Yea, Lord.
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
29Then touched he their eyes, saying, According to your faith be it done unto you.
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
30And their eyes were opened. And Jesus strictly charged them, saying, See that no man know it.
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
31But they went forth, and spread abroad his fame in all that land.
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
32And as they went forth, behold, there was brought to him a dumb man possessed with a demon.
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
33And when the demon was cast out, the dumb man spake: and the multitudes marvelled, saying, It was never so seen in Israel.
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
34But the Pharisees said, By the prince of the demons casteth he out demons.
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
35And Jesus went about all the cities and the villages, teaching in their synagogues, and preaching the gospel of the kingdom, and healing all manner of disease and all manner of sickness.
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
36But when he saw the multitudes, he was moved with compassion for them, because they were distressed and scattered, as sheep not having a shepherd.
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
37Then saith he unto his disciples, The harvest indeed is plenteous, but the laborers are few.
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."
38Pray ye therefore the Lord of the harvest, that he send forth laborers into his harvest.