Swahili: New Testament

American Standard Version

Revelation

9

1Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu.
1And the fifth angel sounded, and I saw a star from heaven fallen unto the earth: and there was given to him the key of the pit of the abyss.
2Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu.
2And he opened the pit of the abyss; and there went up a smoke out of the pit, as the smoke of a great furnace; and the sun and the air were darkened by reason of the smoke of the pit.
3Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
3And out of the smoke came forth locusts upon the earth; and power was given them, as the scorpions of the earth have power.
4Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
4And it was said unto them that they should not hurt the grass of the earth, neither any green thing, neither any tree, but only such men as have not the seal of God on their foreheads.
5Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
5And it was given them that they should not kill them, but that they should be tormented five months: and their torment was as the torment of a scorpion, when it striketh a man.
6Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
6And in those days men shall seek death, and shall in no wise find it; and they shall desire to die, and death fleeth from them.
7Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
7And the shapes of the locusts were like unto horses prepared for war; and upon their heads as it were crowns like unto gold, and their faces were as men's faces.
8Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
8And they had hair as the hair of women, and their teeth were as [teeth] of lions.
9Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
9And they had breastplates, as it were breastplates of iron; and the sound of their wings was as the sound of chariots, of many horses rushing to war.
10Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
10And they have tails like unto scorpions, and stings; and in their tails is their power to hurt men five months.
11Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi.
11They have over them as king the angel of the abyss: his name in Hebrew is Abaddon, and in the Greek [tongue] he hath the name Apollyon.
12Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
12The first Woe is past: behold, there come yet two Woes hereafter.
13Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
13And the sixth angel sounded, and I heard a voice from the horns of the golden altar which is before God,
14Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, "Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!"
14one saying to the sixth angel that had one trumpet, Loose the four angels that are bound at the great river Euphrates.
15Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
15And the four angels were loosed, that had been prepared for the hour and day and month and year, that they should kill the third part of men.
16Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
16And the number of the armies of the horsemen was twice ten thousand times ten thousand: I heard the number of them.
17Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
17And thus I saw the horses in the vision, and them that sat on them, having breastplates [as] of fire and of hyacinth and of brimstone: and the heads of lions; and out of their mouths proceedeth fire and smoke and brimstone.
18Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
18By these three plagues was the third part of men killed, by the fire and the smoke and the brimstone, which proceeded out of their mouths.
19maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
19For the power of the horses is in their mouth, and in their tails: for their tails are like unto serpents, and have heads; and with them they hurt.
20Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
20And the rest of mankind, who were not killed with these plagues, repented not of the works of their hands, that they should not worship demons, and the idols of gold, and of silver, and of brass, and of stone, and of wood; which can neither see, nor hear, nor walk:
21Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.
21and they repented not of their murders, nor of their sorceries, nor of their fornication, nor of their thefts.