Swahili: New Testament

American Standard Version

Romans

3

1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
1What advantage then hath the Jew? or what is the profit of circumcision?
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
2Much every way: first of all, that they were intrusted with the oracles of God.
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
3For what if some were without faith? shall their want of faith make of none effect the faithfulness of God?
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
4God forbid: yea, let God be found true, but every man a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy words, And mightest prevail when thou comest into judgment.
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
5But if our righteousness commendeth the righteousness of God, what shall we say? Is God unrighteous who visiteth with wrath? (I speak after the manner of men.)
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
6God forbid: for then how shall God judge the world?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
7But if the truth of God through my lie abounded unto his glory, why am I also still judged as a sinner?
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
8and why not (as we are slanderously reported, and as some affirm that we say), Let us do evil, that good may come? whose condemnation is just.
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
9What then? are we better than they? No, in no wise: for we before laid to the charge both of Jews and Greeks, that they are all under sin;
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
10as it is written, There is none righteous, no, not one;
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
11There is none that understandeth, There is none that seeketh after God;
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
12They have all turned aside, they are together become unprofitable; There is none that doeth good, no, not, so much as one:
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
13Their throat is an open sepulchre; With their tongues they have used deceit: The poison of asps is under their lips:
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
14Whose mouth is full of cursing and bitterness:
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
15Their feet are swift to shed blood;
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
16Destruction and misery are in their ways;
17njia ya amani hawaijui.
17And the way of peace have they not known:
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
18There is no fear of God before their eyes.
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
19Now we know that what things soever the law saith, it speaketh to them that are under the law; that every mouth may be stopped, and all the world may be brought under the judgment of God:
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
20because by the works of the law shall no flesh be justified in his sight; for through the law [cometh] the knowledge of sin.
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
21But now apart from the law a righteousness of God hath been manifested, being witnessed by the law and the prophets, being witnessed by the law and the prophets;
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
22even the righteousness of God through faith in Jesus Christ unto all them that believe; for there is no distinction;
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
23for all have sinned, and fall short of the glory of God;
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
24being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus:
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
25whom God set forth [to be] a propitiation, through faith, in his blood, to show his righteousness because of the passing over of the sins done aforetime, in the forbearance of God;
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
26for the showing, [I say], of his righteousness at this present season: that he might himself be just, and the justifier of him that hath faith in Jesus.
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
27Where then is the glorying? It is excluded. By what manner of law? of works? Nay: but by a law of faith.
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
28We reckon therefore that a man is justified by faith apart from the works of the law.
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
29Or is God [the God] of Jews only? is he not [the God] of Gentiles also? Yea, of Gentiles also:
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
30if so be that God is one, and he shall justify the circumcision by faith, and the uncircumcision through faith.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.
31Do we then make the law of none effect through faith? God forbid: nay, we establish the law.