1Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
1Kaza im i prispodobu kako valja svagda moliti i nikada ne sustati:
2Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
2"U nekom gradu bio sudac. Boga se nije bojao, za ljude nije mario.
3Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
3U tom gradu bijaše i neka udovica. Dolazila k njemu i molila: 'Obrani me od mog tužitelja!'
4Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
4No on ne htjede zadugo. Napokon reče u sebi: 'Iako se Boga ne bojim nit za ljude marim, ipak,
5lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"
5jer mi udovica ova dodijava, obranit ću je da vječno ne dolazi mučiti me.'"
6Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
6Nato reče Gospodin: "Čujte što govori nepravedni sudac!
7Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
7Neće li onda Bog obraniti svoje izabrane koji dan i noć vape k njemu sve ako i odgađa stvar njihovu?
8Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"
8Kažem vam, ustat će žurno na njihovu obranu. Ali kad Sin Čovječji dođe, hoće li naći vjere na zemlji?"
9Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
9Nekima pak koji se pouzdavahu u sebe da su pravednici, a druge potcjenjivahu, reče zatim ovu prispodobu:
10"Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
10"Dva čovjeka uziđoše u Hram pomoliti se: jedan farizej, drugi carinik.
11Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
11Farizej se uspravan ovako u sebi molio: 'Bože, hvala ti što nisam kao ostali ljudi: grabežljivci, nepravednici, preljubnici ili - kao ovaj carinik.'
12Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
12Postim dvaput u tjednu, dajem desetinu od svega što steknem.'
13Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
13A carinik, stojeći izdaleka, ne usudi se ni očiju podignuti k nebu, nego se udaraše u prsa govoreći: 'Bože milostiv budi meni grešniku!'
14Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."
14Kažem vam: ovaj siđe opravdan kući svojoj, a ne onaj! Svaki koji se uzvisuje, bit će ponižen; a koji se ponizuje, bit će uzvišen."
15Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
15A donosili mu i dojenčad da ih se dotakne. Vidjevši to, učenici im branili.
16Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
16A Isus ih dozva i reče: "Pustite dječicu neka dolaze k meni i ne priječite im jer takvih je kraljevstvo Božje."
17Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."
17"Zaista, kažem vam, tko ne primi kraljevstva Božjega kao dijete, ne, u nj neće ući."
18Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"
18I upita ga neki uglednik: "Učitelju dobri, što mi je činiti da baštinim život vječni?"
19Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
19Reče mu Isus: "Što me zoveš dobrim? Nitko nije dobar, doli Bog jedini.
20Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."
20Zapovijedi znaš: Ne čini preljuba! Ne ubij! Ne ukradi! Ne svjedoči lažno! Poštuj oca svoga i majku!"
21Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
21A onaj će: "Sve sam to čuvao od mladosti."
22Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."
22Čuvši to, Isus mu reče: "Još ti jedno preostaje: sve što imaš prodaj i razdaj siromasima pa ćeš imati blago na nebu. A onda dođi i idi za mnom."
23Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
23Kad je on to čuo, ražalosti se jer bijaše silno bogat.
24Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
24Vidjevši ga, reče Isus: "Kako li je teško imućnicima u kraljevstvo Božje!
25Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
25Lakše je devi kroz uši iglene nego bogatašu u kraljevstvo Božje."
26Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"
26Koji su to čuli, rekoše: "Pa tko se onda može spasiti?"
27Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."
27A on će: "Što je nemoguće ljudima, moguće je Bogu."
28Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"
28Nato reče Petar: "Evo, mi ostavismo svoje i pođosmo za tobom."
29Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
29Isus će im: "Zaista, kažem vam, nema ga tko bi ostavio kuću, ili ženu, ili braću, ili roditelje, ili djecu poradi kraljevstva Božjega,
30atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."
30a da ne bi primio mnogostruko već u ovom vremenu, i u budućem vijeku život vječni."
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
31I uzevši sa sobom dvanaestoricu, reče im: "Evo uzlazimo u Jeruzalem i na Sinu Čovječjem ispunit će se sve što su napisali proroci:
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
32doista, bit će predan poganima, izrugan, zlostavljan i popljuvan;
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."
33i pošto ga izbičuju, ubit će ga, ali on će treći dan ustati."
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
34No oni ništa od toga ne razumješe. Te im riječi bijahu skrivene i ne shvaćahu što bijaše rečeno.
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
35A kad se približavao Jerihonu, neki slijepac sjedio kraj puta i prosio.
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"
36Čuvši gdje mnoštvo prolazi, raspitivao se što je to.
37Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."
37Rekoše mu: "Isus Nazarećanin prolazi."
38Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
38Tada povika: "Isuse, Sine Davidov, smiluj mi se!"
39Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"
39Oni ga sprijeda ušutkivali, ali on je još jače vikao: "Sine Davidov, smiluj mi se!"
40Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
40Isus se zaustavi i zapovjedi da ga dovedu k njemu. Kad se on približi, upita ga:
41"Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."
41"Što hoćeš da ti učinim?" A on će: "Gospodine, da progledam."
42Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."
42Isus će mu: "Progledaj! Vjera te tvoja spasila."
43Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.
43I umah progleda i uputi se za njim slaveći Boga. I sav narod koji to vidje dade hvalu Bogu.