1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
1Jedne je subote prolazio kroz usjeve. Učenici su njegovi trgali klasje, trli ga rukama i jeli.
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
2A neki farizeji rekoše: "Zašto činite što subotom nije dopušteno?"
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
3Odgovori im Isus: "Zar niste čitali što učini David kad ogladnje on i njegovi pratioci?
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
4Kako uđe u Dom Božji, uze, pojede i svojim pratiocima dade prinesene kruhove kojih ne smije jesti nitko, nego samo svećenici?"
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
5I govoraše im: "Sin Čovječji gospodar je subote!"
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
6Druge subote uđe u sinagogu i stane naučavati. Bio je ondje čovjek kome desnica bijaše usahla.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
7Pismoznanci i farizeji vrebahu na nj da li subotom liječi kako bi našli u čemu da ga optuže.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
8A on je znao njihove namjere pa reče čovjeku s usahlom rukom: "Ustani i stani na sredinu!" On usta i stade.
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
9A Isus im reče: "Pitam ja vas: je li subotom dopušteno činiti dobro ili činiti zlo? Život spasiti ili upropastiti?"
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
10Sve ih ošinu pogledom pa reče čovjeku: "Ispruži ruku!" On učini tako - i ruka mu zdrava.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
11A oni se, izbezumljeni, počnu dogovarati što da poduzmu protiv Isusa.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
12Onih dana iziđe na goru da se pomoli. I provede noć moleći se Bogu.
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
13Kad se razdanilo, dozva k sebi učenike te između njih izabra dvanaestoricu, koje prozva apostolima:
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
14Šimuna, koga prozva Petrom, i Andriju, brata njegova, i Jakova, i Ivana, i Filipa, i Bartolomeja,
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
15i Mateja, i Tomu, i Jakova Alfejeva, i Šimuna zvanoga Revnitelj,
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
16i Judu Jakovljeva, i Judu Iškariotskoga, koji posta izdajica.
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
17Isus siđe s njima i zaustavi se na ravnu. I silno mnoštvo njegovih učenika i silno mnoštvo naroda iz cijele Judeje i Jeruzalema, iz primorja tirskog i sidonskog
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
18nagrnuše da ga slušaju i da ozdrave od svojih bolesti. I ozdravljali su oni koje su mučili nečisti dusi.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
19Sve je to mnoštvo tražilo da ga se dotakne jer je snaga izlazila iz njega i sve ozdravljala.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
20On podigne oči prema učenicima i govoraše: "Blago vama, siromasi: vaše je kraljevstvo Božje!
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
21Blago vama koji sada gladujete: vi ćete se nasititi! Blago vama koji sada plačete: vi ćete se smijati!
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
22Blago vama kad vas zamrze ljudi i kad vas izopće i pogrde te izbace ime vaše kao zločinačko zbog Sina Čovječjega!
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
23Radujte se u dan onaj i poskakujte: evo, plaća vaša velika je na nebu. Ta jednako su činili prorocima oci njihovi!"
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
24"Ali jao vama, bogataši: imate svoju utjehu!
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
25Jao vama koji ste sada siti: gladovat ćete! Jao vama koji se sada smijete: jadikovat ćete i plakati!
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
26Jao vama kad vas svi budu hvalili! Ta tako su činili lažnim prorocima oci njihovi."
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
27"Nego, velim vama koji slušate: Ljubite svoje neprijatelje, dobro činite svojim mrziteljima,
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
28blagoslivljajte one koji vas proklinju, molite za one koji vas zlostavljaju."
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
29"Onomu tko te udari po jednom obrazu pruži i drugi, i onomu tko ti otima gornju haljinu ne krati ni donje.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
30Svakomu tko od tebe ište daji, a od onoga tko tvoje otima ne potražuj."
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
31"I kako želite da ljudi vama čine, tako činite i vi njima."
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
32"Ako ljubite one koji vas ljube, kakvo li vam uzdarje? Ta i grešnici ljube ljubitelje svoje.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
33Jednako tako, ako dobro činite svojim dobročiniteljima, kakvo li vam uzdarje? I grešnici to isto čine.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
34Ako pozajmljujete samo onima od kojih se nadate dobiti, kakvo li vam uzdarje? I grešnici grešnicima pozajmljuju da im se jednako vrati."
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
35"Nego, ljubite neprijatelje svoje. Činite dobro i pozajmljujte ne nadajuć se odatle ničemu. I bit će vam plaća velika, i bit ćete sinovi Svevišnjega jer je on dobrostiv i prema nezahvalnicima i prema opakima."
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
36"Budite milosrdni kao što je Otac vaš milosrdan."
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
37"Ne sudite i nećete biti suđeni. Ne osuđujte i nećete biti osuđeni. Praštajte i oprostit će vam se.
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
38Dajite i dat će vam se: mjera dobra, nabijena, natresena, preobilna dat će se u krilo vaše jer mjerom kojom mjerite vama će se zauzvrat mjeriti."
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
39A kaza im i prispodobu: "Može li slijepac slijepca voditi? Neće li obojica u jamu upasti?
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
40Nije učenik nad učiteljem. Pa i tko je posve doučen, bit će samo kao njegov učitelj."
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
41"Što gledaš trun u oku brata svojega, a brvna u oku svome ne opažaš?
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
42Kako možeš kazati bratu svomu: 'Brate, de da izvadim trun koji ti je u oku', a sam u svom oku brvna ne vidiš? Licemjere! Izvadi najprije brvno iz oka svoga pa ćeš onda dobro vidjeti izvaditi trun što je u oku bratovu."
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
43"Nema dobra stabla koje bi rađalo nevaljalim plodom niti stabla nevaljala koje bi rađalo dobrim plodom.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
44Ta svako se stablo po svom plodu poznaje. S trnja se ne beru smokve niti se s gloga grožđe trga."
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
45"Dobar čovjek iz dobra blaga srca svojega iznosi dobro, a zao iz zla iznosi zlo. Ta iz obilja srca usta mu govore."
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
46"Što me zovete 'Gospodine, Gospodine!', a ne činite što zapovijedam?
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
47Tko god dolazi k meni te sluša moje riječi i vrši ih, pokazat ću vam kome je sličan:
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
48sličan je čovjeku koji gradi kuću pa iskopa u dubinu i postavi temelj na kamen. A kad bude poplava, nahrupi bujica na tu kuću, ali je ne može uzdrmati jer je dobro sagrađena.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"
49A koji čuje i ne izvrši, sličan je čovjeku koji sagradi kuću na tlu bez temelja; nahrupi na nju bujica i umah se sruši te bude od te kuće razvalina velika."