1Wakati huo umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena, na hawakuwa na chakula. Basi, Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia,
1Onih se dana opet skupio silan svijet. Budući da nisu imali što jesti, dozva Isus učenike pa im reče:
2"Nawahurumia watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu, wala hawana chakula.
2"Žao mi je naroda jer su već tri dana uza me i nemaju što jesti.
3Nikiwaacha waende nyumbani wakiwa na njaa watazimia njiani, maana baadhi yao wametoka mbali."
3Ako ih otpravim gladne njihovim kućama, klonut će putom. A neki su od njih došli iz daleka."
4Wanafunzi wake wakamwuliza, "Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?"
4Učenici mu odgovore: "Otkuda bi ih tko ovdje u pustinji mogao nahraniti kruhom?"
5Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi?" Nao wakamjibu, "Saba."
5On ih zapita: "Koliko kruhova imate?" Oni odgovore: "Sedam."
6Basi, akawaamuru watu wakae chini. Akaitwaa ile mikate saba, akamshukuru Mungu, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu, nao wakawagawia.
6Nato zapovjedi mnoštvu da posjeda po zemlji. I uze sedam kruhova, zahvali, razlomi i davaše svojim učenicima da posluže. I poslužiše mnoštvu.
7Walikuwa pia na visamaki vichache. Yesu akavibariki, akaamuru vigawiwe watu vilevile.
7A imali su i malo ribica. Blagoslovi i njih te reče da i to posluže.
8Watu wakala, wakashiba. Wakaokota mabaki yaliyosalia wakajaza makapu saba.
8I jeli su i nasitili se. A od preteklih ulomaka odniješe sedam košara.
9Nao waliokula walikuwa watu wapatao elfu nne. Yesu akawaaga,
9Bilo ih je oko četiri tisuće. Tada ih otpusti,
10na mara akapanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda wilaya ya Dalmanutha.
10a sam sa svojim učenicima odmah uđe u lađu i ode u kraj dalmanutski.
11Mafarisayo walikuja, wakaanza kujadiliana na Yesu. Kwa kumjaribu, wakamtaka awafanyie ishara kuonyesha anayo idhini kutoka mbinguni.
11Tada istupiše farizeji i počeše raspravljati s njime. Iskušavajući ga, zatraže od njega znak s neba.
12Yesu akahuzunika rohoni, akasema, "Mbona kizazi hiki kinataka ishara? Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakitapewa ishara yoyote!"
12On uzdahnu iz sve duše i reče: "Zašto ovaj naraštaj traži znak? Zaista, kažem vam, ovome se naraštaju neće dati znak."
13Basi, akawaacha, akapanda tena mashua, akaanza safari kwenda ng'ambo ya pili ya ziwa.
13Tada ih ostavi, ponovno uđe u lađu pa otiđe prijeko.
14Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate; walikuwa na mkate mmoja tu katika mashua.
14A zaboraviše ponijeti kruha; imali su samo jedan kruh sa sobom na lađi.
15Yesu akawaonya, "Angalieni sana! Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode."
15Nato ih Isus opomenu: "Pazite, čuvajte se kvasca farizejskog i kvasca Herodova!"
16Wanafunzi wakaanza kujadiliana wao kwa wao, "Anasema hivyo kwa kuwa hatuna mikate."
16Oni, zamišljeni, među sobom govorahu: "Kruha nemamo."
17Yesu alitambua hayo, akawaambia, "Mbona mnajadiliana juu ya kutokuwa na mikate? Je, bado hamjafahamu, wala hamjaelewa? Je, mioyo yenu imeshupaa?
17Zamijetio to Isus pa im reče: "Zašto ste zamišljeni što kruha nemate? Zar još ne shvaćate i ne razumijete? Zar vam je srce stvrdnuto?
18Je, Mnayo macho na hamwoni? Mnayo masikio na hamsikii? Je, hamkumbuki
18Oči imate, a ne vidite; uši imate, a ne čujete? Zar se ne sjećate?
19wakati ule nilipoimega ile mikate mitano na kuwapa watu elfu tano? Mlikusanya vikapu vingapi vya mabaki ya makombo?" Wakamjibu, "Kumi na viwili."
19Kad sam ono razlomio pet kruhova na pet tisuća, koliko punih košara ulomaka odnijeste?" Kažu mu: "Dvanaest."
20"Na nilipoimega ile mikate saba na kuwapa watu elfu nne, mlikusanya makapu mangapi ya makombo?" Wakamjibu, "Saba."
20"A kada razlomih sedam na četiri tisuće, koliko punih košara ulomaka odnijeste?" Odgovore: "Sedam."
21Basi, akawaambia, "Na bado hamjaelewa?"
21A on će njima: "I još ne razumijete?"
22Yesu alifika Bethsaida pamoja na wanafunzi wake. Huko watu wakamletea kipofu mmoja, wakamwomba amguse.
22Dođu u Betsaidu, dovedu mu slijepca pa ga zamole da ga se dotakne.
23Yesu akamshika mkono huyo kipofu, akampeleka nje ya kijiji. Akamtemea mate machoni, akamwekea mikono, akamwuliza, "Je, unaweza kuona kitu?"
23On uhvati slijepca za ruku, izvede ga iz sela, pljunu mu u oči, stavi na nj ruke i zapita ga: "Vidiš li što?"
24Huyo kipofu akatazama, akasema, "Ninawaona watu wanaoonekana kama miti inayotembea."
24Slijepac upilji pogled i reče: "Opažam ljude; vidim nešto kao drveće ... hodaju."
25Kisha Yesu akamwekea tena mikono machoni, naye akakaza macho, uwezo wake wa kuona ukamrudia, akaona kila kitu sawasawa.
25Tada mu Isus opet stavi ruke na oči i slijepac progleda i ozdravi te je mogao sve jasno na daleko vidjeti.
26Yesu akamwambia aende zake nyumbani na kumwamuru, "Usirudi kijijini!"
26Tada ga posla kući i reče mu: "Ne ulazi u selo."
27Kisha Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika vijiji vya Kaisarea Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu aliwauliza wanafunzi wake, "Watu wanasema mimi ni nani?"
27I krenu Isus i njegovi učenici u sela Cezareje Filipove. Putem on upita učenike: "Što govore ljudi, tko sam ja?"
28Wakamjibu, "Wengine wanasema wewe ni Yohane Mbatizaji, wengine Eliya na wengine mmojawapo wa manabii."
28Oni mu rekoše: "Da si Ivan Krstitelj, drugi da si Ilija, treći opet da si neki od proroka."
29Naye akawauliza, "Na ninyi je, mnasema mimi ni nani?" Petro akamjibu, "Wewe ndiwe Kristo."
29On njih upita: "A vi, što vi kažete, tko sam ja?" Petar prihvati i reče: "Ti si Pomazanik - Krist!"
30Kisha Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
30I zaprijeti im da nikomu ne kazuju o njemu.
31Yesu alianza kuwafundisha wanafunzi wake: "Ni lazima Mwana wa Mtu apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Atauawa na baada ya siku tatu atafufuka."
31I poče ih poučavati kako Sin Čovječji treba da mnogo pretrpi, da ga starješine, glavari svećenički i pismoznanci odbace, da bude ubijen i nakon tri dana da ustane.
32Yesu aliwaambia jambo hilo waziwazi. Basi, Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea.
32Otvoreno im to govoraše. Petar ga uze u stranu i poče odvraćati.
33Lakini Yesu akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro akisema, "Ondoka mbele yangu, Shetani! Fikira zako si za kimungu ila ni za kibinadamu!"
33A on se okrenu, pogleda svoje učenike pa zaprijeti Petru: "Nosi se od mene, sotono, jer ti nije na pameti što je Božje, nego što je ljudsko!"
34Kisha akauita umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
34Tada dozva narod i učenike pa im reče: "Hoće li tko za mnom, neka se odrekne samoga sebe, neka uzme svoj križ i neka ide za mnom.
35Maana mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza, lakini mtu atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema, atayaokoa.
35Tko hoće život svoj spasiti, izgubit će ga; a tko izgubi život svoj poradi mene i evanđelja, spasit će ga.
36Je, kuna faida gani mtu kuupata ulimwengu wote na kuyapoteza maisha yake?
36Ta što koristi čovjeku steći sav svijet, a životu svojemu nauditi?
37Ama mtu atatoa kitu gani badala ya maisha yake?
37Ta što da čovjek dadne u zamjenu za život svoj?
38Mtu yeyote katika kizazi hiki kiovu na kisichomjali Mungu anayenionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu."
38Doista, tko se zastidi mene i mojih riječi u ovom preljubničkom i grešničkom naraštaju - njega će se stidjeti i Sin Čovječji kada dođe u slavi Oca svoga zajedno sa svetim anđelima."