Swahili: New Testament

Croatian

Matthew

14

1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
1U ono vrijeme doču Herod tetrarh za Isusa
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
2pa reče svojim slugama: "To je Ivan Krstitelj! On uskrsnu od mrtvih i zato čudesne sile djeluju u njemu."
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
3Herod doista bijaše uhitio Ivana te ga svezana bacio u tamnicu zbog Herodijade, žene brata svoga Filipa.
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
4Jer Ivan mu govoraše: "Ne smiješ je imati!"
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
5Htjede ga ubiti, ali se bojao naroda jer su ga smatrali prorokom.
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
6Na Herodov rođendan zaplesa kći Herodijadina pred svima i svidje se Herodu.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
7Zato se zakle dati joj što god zaište.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
8A ona nagovorena od matere: "Daj mi, reče, ovdje na pladnju glavu Ivana Krstitelja."
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
9Ražalosti se kralj, ali zbog zakletve i sustolnika zapovjedi da se dade.
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
10Posla odrubiti glavu Ivanu u tamnici.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
11I doniješe glavu njegovu na pladnju, dadoše djevojci, a ona je odnije materi.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
12A učenici njegovi dođu, uzmu njegovo tijelo i pokopaju ga pa odu i jave Isusu.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
13Kad je Isus to čuo, povuče se odande lađom na samotno mjesto, u osamu. Dočuo to narod pa pohrli pješice za njim iz gradova.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
14Kad on iziđe, vidje silan svijet, sažali mu se nad njim te izliječi njegove bolesnike.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
15Uvečer mu pristupe učenici pa mu reknu: "Pust je ovo kraj i već je kasno. Otpusti dakle svijet: neka odu po selima kupiti hrane."
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
16A Isus im reče: "Ne treba da idu, dajte im vi jesti."
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
17Oni mu kažu: "Nemamo ovdje ništa osim pet kruhova i dvije ribe."
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
18A on će im: "Donesite mi ih ovamo."
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
19I zapovjedi da mnoštvo posjeda po travi. On uze pet kruhova i dvije ribe, pogleda na nebo, izreče blagoslov pa razlomi i dade kruhove učenicima, a učenici mnoštvu.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
20I jeli su svi i nasitili se. Od preteklih ulomaka nakupiše dvanaest punih košara.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
21A blagovalo je oko pet tisuća muškaraca, osim žena i djece.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
22I odmah prisili učenike da uđu u lađu i da se prebace prijeko dok on otpusti mnoštvo.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
23A pošto otpusti mnoštvo, uziđe na goru, nasamo, da se pomoli. Uvečer bijaše ondje sam.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
24Lađa se već mnogo stadija bila ostisla od kraja, šibana valovima. Bijaše protivan vjetar.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
25O četvrtoj noćnoj straži dođe on k njima hodeći po moru.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
26A učenici ugledavši ga kako hodi po moru, prestrašeni rekoše: "Utvara!" I od straha kriknuše.
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
27Isus im odmah progovori: "Hrabro samo! Ja sam! Ne bojte se!"
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
28Petar prihvati i reče: "Gospodine, ako si ti, zapovjedi mi da dođem k tebi po vodi!"
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
29A on mu reče: "Dođi!" I Petar siđe s lađe te, hodeći po vodi, pođe k Isusu.
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
30Ali kad spazi vjetar, poplaši se, počne tonuti te krikne: "Gospodine, spasi me!"
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
31Isus odmah pruži ruku, dohvati ga i kaže mu: "Malovjerni, zašto si posumnjao?"
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
32Kad uđoše u lađu, utihnu vjetar.
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
33A oni na lađi poklone mu se ničice govoreći: "Uistinu, ti si Sin Božji!"
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
34Pošto preploviše, dođu na kraj, u Genezaret.
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
35I ljudi ga onoga kraja prepoznaju pa razglase po svoj onoj okolici. I donošahu mu sve bolesnike
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.
36te ga moljahu da se samo dotaknu skuta njegove haljine. I koji bi se dotakli, ozdravili bi.