Swahili: New Testament

Croatian

Matthew

17

1Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu.
1Nakon šest dana uze Isus sa sobom Petra, Jakova i Ivana, brata njegova, te ih povede na goru visoku, u osamu,
2Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
2i preobrazi se pred njima. I zasja mu lice kao sunce, a haljine mu postadoše bijele kao svjetlost.
3Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
3I gle: ukazaše im se Mojsije i Ilija te razgovarahu s njime.
4Hapo Petro akamwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
4A Petar prihvati i reče Isusu: "Gospodine, dobro nam je ovdje biti. Ako hoćeš, načinit ću ovdje tri sjenice, tebi jednu, Mojsiju jednu i Iliji jednu."
5Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni."
5Dok je on još govorio, gle, svijetao ih oblak zasjeni, a glas iz oblaka govoraše: "Ovo je Sin moj, Ljubljeni! U njemu mi sva milina! Slušajte ga!"
6Wanafunzi waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
6Čuvši glas, učenici padoše licem na zemlju i silno se prestrašiše.
7Yesu akawaendea, akawagusa, akasema, "Simameni, msiogope!"
7Pristupi k njima Isus, dotakne ih i reče: "Ustanite, ne bojte se!"
8Walipoinua macho yao hawakumwona mtu, ila Yesu peke yake.
8Podigoše oči, ali ne vidješe nikoga doli Isusa sama.
9Basi, walipokuwa wanashuka mlimani, Yesu akawaonya: "Msimwambie mtu mambo mliyoyaona mpaka Mwana wa Mtu atakapofufuliwa kutoka wafu."
9Dok su silazili s gore, zapovjedi im Isus: "Nikomu ne kazujte viđenje dok Sin Čovječji od mrtvih ne uskrsne."
10Kisha wanafunzi wakamwuliza, "Mbona walimu wa Sheria wanasema ati ni lazima kwanza Eliya aje?"
10Upitaše ga učenici: "Što dakle pismoznanci govore da prije treba da dođe Ilija?"
11Yesu akawajibu, "Kweli, Eliya atakuja kutayarisha mambo yote.
11On im odgovori: "Ilija će doduše doći i sve obnoviti.
12Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja nao hawakumtambua, bali walimtendea jinsi walivyotaka. Mwana wa Mtu atateswa vivyo hivyo mikononi mwao."
12No velim vam: Ilija je već došao, ali ga ne upoznaše, već učiniše s njim što im se prohtjelo. Tako je i Sinu Čovječjemu trpjeti od njih."
13Hapo hao wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohane mbatizaji.
13Tada razumješe učenici da im to reče o Ivanu Krstitelju.
14Walipojiunga tena na ule umati wa watu, mtu mmoja alimwendea Yesu, akampigia magoti,
14Kada dođoše k mnoštvu, pristupi mu čovjek, padne pred njim na koljena
15akasema, "Mheshimiwa, mwonee huruma mwanangu kwa kuwa ana kifafa, tena anateseka sana; mara nyingi yeye huanguka motoni na majini.
15i reče: "Gospodine, smiluj se sinu mojemu jer je mjesečar i zlo mu je. Često doista pada u oganj i često u vodu.
16Nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumponya."
16Dovedoh ga tvojim učenicima i ne mogoše ga izliječiti."
17Yesu akajibu, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia ninyi mpaka lini? Mleteni hapa huyo mtoto."
17A Isus odgovori: "O rode nevjerni i opaki! Dokle mi je biti s vama! Dokle li vas podnositi! Dovedite mi ga ovamo!"
18Basi, Yesu akamkemea huyo pepo, naye akamtoka, na yule mtoto akapona wakati huohuo.
18I zaprijeti Isus zloduhu te on iziđe iz njega. I ozdravi dječak toga časa.
19Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha, wakamwuliza, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo?"
19Tada učenici pristupiše nasamo k Isusu i rekoše: "Zašto ga mi ne mogosmo izagnati?"
20Yesu akawajibu, "Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, hata iwe ndogo kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: Toka hapa uende pale, nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu."
20Kaže im: "Zbog vaše malovjernosti. Zaista, kažem vam, ako imadnete vjere koliko je zrno gorušičino te reknete ovoj gori: 'Premjesti se odavde onamo!', premjestit će se i ništa vam neće biti nemoguće."
21"Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga."
21#
22Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.
22A kad su se skupili u Galileji, reče im Isus: "Sin Čovječji ima biti predan ljudima u ruke
23Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa." Wanafunzi wakahuzunika mno.
23i ubit će ga, ali on će treći dan uskrsnuti." I ožalostiše se silno.
24Walipofika Kafarnaumu watu wenye kukusanya fedha ya zaka ya Hekalu walimwendea Petro, wakamwuliza, "Je, mwalimu wenu hulipa fedha ya zaka?"
24Kad stigoše u Kafarnaum, pristupe Petru oni što ubiru dvodrahme pa mu rekoše: "Učitelj vaš ne plaća dvodrahme?"
25Petro akajibu, "Naam, hulipa." Basi, Petro alipoingia ndani ya nyumba, kabla hata hajasema neno, Yesu akamwuliza, "Simoni, wewe unaonaje? Wafalme wa dunia hukusanya ushuru au kodi kutoka kwa kina nani? Kutoka kwa wananchi ama kutoka kwa wageni?"
25"Plaća", odgovori. A kad on uđe u kuću, pretekne ga Isus: "Što ti se čini, Šimune? Kraljevi zemaljski od koga ubiru carinu ili porez? Od svojih sinova ili od tuđih?"
26Petro akajibu, "Kutoka kwa wageni." Yesu akamwambia, "Haya basi, wananchi hawahusiki.
26Kad on odgovori: "Od tuđih!", reče mu Isus: "Sinovi su, dakle, oslobođeni.
27Lakini kusudi tusiwakwaze, nenda ziwani ukatupe ndoana; chukua samaki wa kwanza atakayenaswa, fungua kinywa chake, na ndani utakuta fedha taslimu ya zaka. Ichukue ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako."
27Ali da ih ne sablaznimo, pođi k moru, baci udicu i prvu ribu koja naiđe uzmi, otvori joj usta i naći ćeš stater. Uzmi ga pa im ga podaj za me i za se."