Swahili: New Testament

Croatian

Matthew

20

1"Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
1"Kraljevstvo je nebesko kao kad domaćin rano ujutro izađe najmiti radnike u svoj vinograd.
2Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
2Pogodi se s radnicima po denar na dan i pošalje ih u svoj vinograd.
3Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
3Izađe i o trećoj uri i vidje druge gdje stoje na trgu besposleni
4Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
4pa i njima reče: 'Idite i vi u moj vinograd pa što bude pravo, dat ću vam.'
5Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
5I oni odoše. Izađe opet o šestoj i devetoj uri te učini isto tako.
6Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
6A kad izađe o jedanaestoj uri, nađe druge gdje stoje i reče im: 'Zašto ovdje stojite vazdan besposleni?'
7Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
7Kažu mu: 'Jer nas nitko ne najmi.' Reče im: 'Idite i vi u vinograd.'"
8"Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
8"Uvečer kaže gospodar vinograda svojemu upravitelju: 'Pozovi radnike i podaj im plaću počevši od posljednjih pa sve do prvih.'
9Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
9Dođu tako oni od jedanaeste ure i prime po denar.
10Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
10Pa kada dođu oni prvi, pomisle da će primiti više, ali i oni prime po denar.
11Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
11A kad primiše, počeše mrmljati protiv domaćina:
12Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
12'Ovi posljednji jednu su uru radili i izjednačio si ih s nama, koji smo podnosili svu tegobu dana i žegu.'"
13"Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
13"Nato on odgovori jednomu od njih: 'Prijatelju, ne činim ti krivo. Nisi li se pogodio sa mnom po denar?
14Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
14Uzmi svoje pa idi. A ja hoću i ovomu posljednjemu dati kao i tebi.
15Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?"
15Nije li mi slobodno činiti sa svojim što hoću? Ili zar je oko tvoje zlo što sam ja dobar?'"
16Yesu akamaliza kwa kusema, "Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho."
16"Tako će posljednji biti prvi, a prvi posljednji."
17Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
17Dok je Isus uzlazio u Jeruzalem, uze dvanaestoricu nasamo te im putem reče:
18"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
18"Evo, uzlazimo u Jeruzalem i Sin Čovječji bit će predan glavarima svećeničkim i pismoznancima. Osudit će ga na smrt
19Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa."
19i predati poganima da ga izrugaju, izbičuju i razapnu, ali on će treći dan uskrsnuti."
20Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
20Tada mu pristupi mati sinova Zebedejevih zajedno sa sinovima, pade ničice da od njega nešto zaište.
21Yesu akamwuliza, "Unataka nini?" Huyo mama akamwambia, "Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto."
21A on će joj: "Što želiš?" Kaže mu: "Reci da ova moja dva sina u tvome kraljevstvu sjednu uza te, jedan tebi zdesna, drugi slijeva."
22Yesu akajibu, "Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?" Wakamjibu, "Tunaweza."
22Isus odgovori: "Ne znate što ištete. Možete li piti čašu koju ću ja piti?" Kažu mu: "Možemo!"
23Yesu akawaambia, "Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu."
23A on im reče: "Čašu ćete moju doduše piti, ali sjesti meni zdesna ili slijeva - to nisam ja vlastan dati, to je onih kojima je pripravio moj Otac."
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
24Kada su to čula ostala desetorica, razgnjeve se na dva brata.
25Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
25Zato ih Isus dozva i reče: "Znate da vladari gospoduju svojim narodima i velikaši njihovi drže ih pod vlašću.
26Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
26Neće tako biti među vama! Naprotiv, tko hoće da među vama bude najveći, neka vam bude poslužitelj.
27na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
27I tko god hoće da među vama bude prvi, neka vam bude sluga."
28Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
28"Tako i Sin Čovječji nije došao da bude služen, nego da služi i život svoj dade kao otkupninu za mnoge."
29Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
29Kad su izlazili iz Jerihona, pođe za njim silan svijet.
30Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
30I gle, dva slijepca sjeđahu kraj puta. Čuvši da Isus prolazi, povikaše: "Gospodine, smiluj nam se, Sine Davidov!"
31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
31Mnoštvo ih ušutkivalo, ali oni još jače viknuše: "Gospodine, smiluj nam se, Sine Davidov!"
32Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
32Isus se zaustavi, dozove ih i reče: "Što hoćete da vam učinim?"
33Wakamjibu, "Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe."
33Kažu mu: "Gospodine, da nam se otvore oči."
34Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.
34Isus se ganut dotače njihovim očiju i oni odmah progledaše. I pođoše za njim.