1Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
1Kad je Isus sišao s gore, pohrli za njim silan svijet.
2Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, "Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!"
2I gle, pristupi neki gubavac, pokloni mu se do zemlje i reče: "Gospodine, ako hoćeš, možeš me očistiti."
3Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka! Takasika." Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
3Isus pruži ruku i dotakne ga se govoreći: "Hoću, očisti se!" I odmah se očisti od gube.
4Kisha Yesu akamwambia, "Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona."
4Kaže mu Isus: "Pazi, nikomu ne kazuj, nego idi, pokaži se svećeniku i prinesi dar što ga propisa Mojsije, njima za svjedočanstvo."
5Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
5Kad uđe u Kafarnaum, pristupi mu satnik pa ga zamoli:
6akisema, "Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana."
6"Gospodine, sluga mi leži kod kuće uzet, u strašnim mukama."
7Yesu akamwambia, "Nitakuja kumponya."
7Kaže mu: "Ja ću doći izliječiti ga."
8Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
8Odgovori satnik: "Gospodine, nisam dostojan da uđeš pod krov moj, nego samo reci riječ i izliječen će biti sluga moj.
9Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya."
9Ta i ja, premda sam čovjek pod vlašću, imam pod sobom vojnike pa reknem jednomu: 'Idi!' - i ode, drugomu: 'Dođi!' - i dođe, a sluzi svomu: 'Učini to' - i učini."
10Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, "Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
10Čuvši to, zadivi se Isus i reče onima koji su išli za njim: "Zaista, kažem vam, ni u koga u Izraelu ne nađoh tolike vjere.
11Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
11A kažem vam: Mnogi će s istoka i zapada doći i sjesti za stol s Abrahamom, Izakom i Jakovom u kraljevstvu nebeskom,
12Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno."
12a sinovi će kraljevstva biti izbačeni van u tamu. Ondje će biti plač i škrgut zubi."
13Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, "Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini." Na mtumishi wake akapona saa ileile.
13I reče Isus satniku: "Idi, neka ti bude kako si vjerovao!" I ozdravi sluga u taj čas.
14Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
14Ušavši u kuću Petrovu, Isus ugleda njegovu punicu koja ležaše u ognjici.
15Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
15Dotače joj se ruke i pusti je ognjica. Ona ustade i posluživaše mu.
16Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
16A uvečer mu doniješe mnoge opsjednute. On izagna duhove riječju i sve bolesnike ozdravi -
17Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: "Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu."
17da se ispuni što je rečeno po Izaiji proroku: On slabosti naše uze i boli ponese.
18Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
18Kad Isus vidje mnoštvo oko sebe, zapovjedi da se prijeđe prijeko.
19Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, "Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako."
19I pristupi jedan pismoznanac te mu reče: "Učitelju, za tobom ću kamo god ti pošao."
20Yesu akamjibu, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
20Kaže mu Isus: "Lisice imaju jazbine i ptice nebeske gnijezda, a Sin Čovječji nema gdje bi glavu naslonio."
21Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, "Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu."
21Drugi mu od učenika reče: "Gospodine, dopusti mi da prije odem i pokopam svoga oca."
22Lakini Yesu akamwambia, "Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao."
22Isus mu kaže: "Hajde za mnom i pusti neka mrtvi pokapaju svoje mrtve."
23Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
23Kad uđe u lađu, pođoše za njim njegovi učenici.
24Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
24I gle, žestok vihor nasta na moru tako da lađu prekrivahu valovi. A on je spavao.
25Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, "Bwana, tuokoe, tunaangamia!"
25Oni pristupiše i probudiše ga govoreći: "Gospodine, spasi, pogibosmo!"
26Yesu akawaambia, "Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?" Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
26Kaže im: "Što ste plašljivi, malovjerni?" Tada ustade i zaprijeti vjetrovima i moru te nasta velika utiha.
27Watu wakashangaa, wakasema, "Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!"
27A ljudi su u čudu pitali: "Tko je taj da mu se i vjetrovi i more pokoravaju?"
28Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
28I kada dođe prijeko, u gadarski kraj, eto mu u susret dvaju opsjednutih: izlazili su iz grobnica, silno goropadni, te nitko nije mogao proći onim putem.
29Nao wakaanza kupiga kelele, "Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?"
29I gle, povikaše: "Što ti imaš s nama, Sine Božji? Došao si ovamo prije vremena mučiti nas?"
30Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
30A podalje od njih paslo je veliko krdo svinja.
31Basi, hao pepo wakamsihi, "Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale."
31Zlodusi ga zaklinjahu: "Ako nas istjeraš, pošalji nas u ovo krdo svinja."
32Yesu akawaambia, "Haya, nendeni." Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
32On im reče: "Idite!" Oni iziđoše i uđoše u svinje. I gle, sve krdo jurnu niz obronak u more i podavi se u vodama.
33Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
33A svinjari pobjegoše, odoše u grad te razglasiše sve, napose o opsjednutima.
34Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.
34I gle, sav grad iziđe u susret Isusu. Kad ga ugledaše, zamole ga da ode iz njihova kraja.