1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
1Viimaks veel, vennad, palvetage meie eest, et Issanda sõna leviks ja kirgastuks nõnda nagu teiegi juures
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
2ning et meid kistaks välja üleannetute ja kurjade inimeste käest. Sest usku ei ole kõikidel.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
3Aga ustav on Issand, kes teid kinnitab ja kurja eest hoiab.
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
4Me oleme ju Issandas veendunud teie suhtes, et te olete teinud ja teete, mida me käsime.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
5Issand aga suunaku teie südamed Jumala armastuse ja Kristuse kannatlikkuse poole!
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
6Aga meie käsime teid, vennad, meie Issanda Jeesuse Kristuse nimel vältida kõiki vendi, kes logelevad ja ei ela mitte pärimuse järgi, mille nad on meilt saanud.
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
7Te teate ju ise, kuidas te peate meid võtma eeskujuks, sest meie ei ole teie keskel logelnud
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
8ega ole kellegi juures leiba muidu söönud, vaid oleme vaeva nähes ja rühmates töötanud nii ööd kui päevad, et me ei koormaks kedagi teie seast.
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
9Mitte et meil poleks seda meelevalda, vaid me tahaksime anda teile head eeskuju.
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
10Sest ka siis, kui olime teie juures, käskisime teid: 'Kes ei taha töötada, ärgu ka söögu!'
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
11Me kuuleme ju, et mõned teie keskel elavad korratult ja ei tööta, vaid janditavad.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
12Niisuguseid me käsime ja manitseme Issandas Jeesuses Kristuses, et nad vaikselt töötades sööksid oma leiba.
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
13Teie aga, vennad, ärge tüdige head tehes!
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
14Aga kui mõni ei kuula, mida me oleme ütelnud selles kirjas, siis pange teda tähele ja ärge suhelge temaga, et ta hakkaks häbenema.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
15Kuid ärge pidage teda vaenlaseks, vaid noomige teda kui venda.
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
16Aga rahu Issand ise andku teile rahu alati ja igal viisil. Issand olgu teie kõikidega!
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
17See tervitus on minu, Pauluse käega. See on tähiseks igas kirjas - nii kirjutan mina!
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
18Meie Issanda Jeesuse Kristuse arm olgu teie kõikidega!