1Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
1Seetõttu mina, Paulus, olen Kristuse Jeesuse vang teie, paganate heaks.
2Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
2Jah, küllap te olete kuulnud Jumala armu majapidamisest, mis minu kätte on antud teie heaks!
3Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
3Jumal on mulle ilmutuse kaudu teatanud saladuse, nagu ma eespool lühidalt kirjutasin.
4nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
4Seda lugedes te võite mõista minu arusaamist Kristuse saladustest,
5Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
5mida muistsete põlvede aegu ei antud teada inimlastele nii, nagu see nüüd on ilmutatud tema pühadele apostlitele ja prohvetitele Vaimus:
6Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
6et paganadki on tõotuse kaaspärijad ja sama ihu liikmed ja kaasosalised Kristuses Jeesuses evangeeliumi kaudu.
7Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
7Selle evangeeliumi teenriks olen ma saanud Jumala armu kingituse kohaselt, mis mulle on antud tema väe toimel.
8Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
8Minule, kõige vähemale kõigi pühade seast, on antud see arm: kuulutada paganate seas evangeeliumi Kristuse äraarvamatust rikkusest
9tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele,
9ja valge ette tuua kõigile, mis on selle saladuse korraldus, mis on kätketud aegade algusest peale Jumalas, kes kõik on loonud.
10kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
10Nii saab nüüd Jumala mitmekülgne tarkus teatavaks koguduse kaudu taevastele valitsustele ja meelevaldadele
11Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
11ajastute ettemääramise järgi, mille ta on teinud teoks meie Issandas Kristuses Jeesuses,
12Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
12kelle sees usu läbi temasse on meil julgus ja usaldav ligipääs Jumalale.
13Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
13Seetõttu ma kutsun teid üles mitte loobuma, kui mind ahistatakse teie pärast - see on teie kirkus.
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
14Sellepärast ma põlvitan Isa ees,
15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
15kelle käest iga suguvõsa taevas ja maa peal saab nime,
16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
16et ta teile oma kirkuse rikkust mööda annaks väge saada tema Vaimu läbi tugevaks seesmise inimese poolest,
17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
17et Kristus usu kaudu elaks teie südameis ning te oleksite juurdunud ja kinnitatud armastuses,
18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
18et te suudaksite koos kõigi pühadega tunnetada, milline on armastuse laius ja pikkus ja sügavus ja kõrgus,
19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
19ning ära tunda Kristuse armastust, mis ületab iga tunnetuse, et te oleksite täidetud Jumala kogu täiusega.
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
20Aga Jumalale, kes meis tegutseva väega võib korda saata palju rohkem, kui oskame paluda või isegi mõelda,
21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.
21temale olgu kirkus koguduses ja Kristuses Jeesuses igavesest ajast igavesti kõigi sugupõlvedeni! Aamen.