Swahili: New Testament

Estonian

Ephesians

5

1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
1Võtke nüüd Jumal eeskujuks nagu armastatud lapsed,
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
2ja käige armastuses, nõnda nagu Kristus meid on armastanud ja on iseenese loovutanud meie eest anniks ja ohvriks, magusaks lõhnaks Jumalale.
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
3Aga hoorusest ja kogu rüvedusest ja ahnusest ärgu olgu teie seas juttugi, nõnda nagu on kohane pühadele.
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
4Samuti riivatus ja rumalad sõnad ja sündsusetu lõõpimine ei sobi teile, vaid selle asemel olgu tänu.
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
5Seda teadke kindlasti, et ühelgi hoorajal ega kõlvatul ega ahnitsejal - tähendab ebajumalateenreil - ei ole pärandit Kristuse ja Jumala riigis.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
6Ärgu ükski petku teid tühjade sõnadega, sest niisuguste asjade pärast tuleb Jumala viha sõnakuulmatute laste peale!
7Basi, msishirikiane nao.
7Ärge siis saage nende kaaslasteks!
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
8Sest varem te olite pimedus, nüüd aga olete valgus Issandas. Käige nagu valguse lapsed -
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
9valguse vili on ju igasuguses headuses ja õigluses ja tões -,
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
10uurige, mis on Issandale meelepärane,
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
11ja ärge hakake pimeduse viljatute tegude kaasosaliseks, vaid pigem paljastage neid!
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
12Sest mida nad salajas teevad, seda on nimetadagi häbi.
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
13Aga kõik valguse poolt paljastatu saab avalikuks;
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
14sest kõik, mis saab avalikuks, on valguse käes. Seepärast on öeldud: 'Ärka üles, kes sa magad, ja tõuse üles surnuist, siis särab sulle Kristus!'
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
15Vaadake siis hoolega, kuidas te elate: mitte nagu arutud, vaid nagu targad,
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
16kasutades aega õigesti, sest päevad on kurjad.
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
17Seepärast ärge olge rumalad, vaid mõistke, mis on Issanda tahtmine.
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
18Ja ärge joovastuge veinist, millest tuleb liiderlikkus, vaid saage täis Vaimu,
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
19lauldes omavahel psalme, hümne ja vaimulikke laule, lauldes ja pilli mängides kogu oma südamega Issandale,
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
20tänades alati Jumalat ja Isa meie Issanda Jeesuse Kristuse nimel.
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
21Alistuge üksteisele Kristuse kartuses,
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
22naised oma meestele otsekui Issandale,
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
23sest mees on naise pea, nagu Kristus on koguduse pea, olles ise ihu päästja.
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
24Nagu kogudus alistub Kristusele, nõnda alistugu ka naised meestele kõigis asjus.
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
25Mehed, armastage naisi, otsekui Kristus on armastanud kogudust ja loovutanud iseenese tema eest,
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
26et teda pühitseda, olles ta puhastanud vees pesemisega sõna läbi,
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
27et kogudust iseenda ette seada kirkana, nii et tal ei oleks plekki ega kortsu ega muud sellesarnast, vaid et ta oleks püha ja laitmatu.
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
28Nõnda peavad mehedki armastama oma naisi nagu iseenese ihu. Kes oma naist armastab, armastab iseennast.
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
29Keegi pole ju kunagi vihanud iseenese ihu, vastupidi, ta toidab ja hellitab seda nii nagu Kristus kogudust,
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
30sest me oleme tema ihu liikmed.
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
31'Seepärast jätab mees maha oma isa ja ema ning hoiab oma naise poole, ja need kaks saavad üheks.'
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
32See saladus on suur: ma räägin Kristusest ja kogudusest.
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
33Igal juhul armastagu ka igaüks teie seast oma naist nii nagu iseennast, aga naine kartku meest!