1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
1Lapsed, olge kuulekad oma vanemaile Issandas, sest see on õige!
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
2'Austa oma isa ja ema,' see on esimene käsusõna tõotusega,
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
3'et su käsi käiks hästi ja sa elaksid kaua maa peal!'
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
4Ja teie, isad, ärge ärritage oma lapsi vihale, vaid kasvatage neid juhatamise ja manitsemisega Issanda tahte järgi!
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
5Orjad, olge oma maistele isandatele kuulekad nagu Kristusele kartuse ja värinaga siiras südames,
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
6mitte silmapetteks otsekui inimeste ees lipitsemiseks, vaid nagu Kristuse sulased, kes kõigest hingest teevad Jumala tahtmist,
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
7teenides heal meelel otsekui Issandat ja mitte nagu inimesi,
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
8teades, et igaüks, kui ta on teinud midagi head, saab selle eest tasu Issanda käest, olgu ta ori või vaba.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
9Ja teie, isandad, tehke sedasama neile ning jätke maha ähvardamine, teades, et nii neil kui teil on Isand taevas ning tema juures ei ole mingit erapoolikust.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
10Viimaks veel: saage vägevaks Issandas ja tema tugevuse jõus!
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
11Pange ülle Jumala sõjavarustus, et te suudaksite seista kuradi salanõude vastu!
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
12Meil ei tule ju võidelda inimestega, vaid meelevaldade ja võimudega, selle pimeduse maailma valitsejatega, kurjade taevaaluste vaimudega.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
13Seepärast võtke kätte kõik Jumala sõjavarustus, et te suudaksite vastu panna kurjal päeval ja jääda püsima, kui te olete kõik teinud.
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
14Seiske nüüd ja teie niuded olgu vöötatud tõega ja teil olgu seljas õiguse soomusrüü
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
15ja teie jalgades olgu valmidus minna kuulutama rõõmusõnumit rahust!
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
16Kõigepealt aga võtke kätte usukilp, millega te võite kustutada kõik kurja põlevad nooled!
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
17Võtke ka päästekiiver ja vaimumõõk, see on Jumala sõna!
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
18Ja palve ja anumisega palvetage igal ajal Vaimus ning selleks valvake kogu püsivusega ja eestpalvetega kõigi pühade eest
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
19ja minugi eest, et mulle antaks arukust, kui ma avan suu, julgelt teada anda evangeeliumi saladust,
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
20mille käskjalana ma olengi ahelais, et ma selles julgust saades hakkaksin rääkima nii, nagu ma pean.
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
21Et teiegi saaksite teada, kuidas mu käsi käib ja mida ma teen, siis jutustab seda teile Tühhikos, armas vend ja ustav abiline Issandas.
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
22Ma saadan tema teie juurde just sellepärast, et te saaksite teada, kuidas on lugu meiega, ja et ta julgustaks teie südameid.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
23Rahu vendadele ja armastust koos usuga Jumalalt Isalt ja Issandalt Jeesuselt Kristuselt!
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.
24Arm olgu nende kõikidega, kes armastavad meie Issandat Jeesust Kristust kadumatuses!