1Ndugu zangu, wengi wenu msiwe walimu. Kama mjuavyo, sisi walimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine.
1Ärgu püüdku paljud teie seast, mu vennad, saada õpetajaiks! Te teate ju, et meie osaks on teistest karmim kohtuotsus.
2Lakini kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu, na anaweza kutawala nafsi yake yote.
2Me kõik eksime paljus. Kui keegi ei eksi kõnes, siis on ta täiuslik ja suudab ohjeldada ka kogu ihu.
3Sisi huwatia farasi lijamu kinywani mwao ili watutii; na kwa njia hiyo twaweza kuwaongoza kokote tunakotaka.
3Kui me paneme aga hobusele suitsed suhu, et ta oleks meile kuulekas, siis me juhime kogu hobust.
4Meli nazo pia, ingawa ni kubwa sana, na husukumwa na upepo mkali, huweza kugeuzwa kwa usukani mdogo sana, zikaelekea kokote nahodha anakotaka.
4Ennäe, ka suuri ja rajutuulte aetud laevu juhitakse väikese tüüriga sinna, kuhu tüürimees tahab.
5Vivyo hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana. Moto mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa.
5Nõnda on ka keel väike ihuliige, aga kiitleb suurte asjade üle. Ennäe kui väike tuli süütab suure metsa!
6Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe.
6Ka keel on tuli. Keel, see ebaõigluse maailm, on seatud meie ihuliikmete hulka nii, et see rüvetab kogu ihu ja süütab põlema eluratta, nagu ta ise on süüdatud põrgust.
7Binadamu anaweza kuwafuga wanyama, na amefaulu kufuga viumbe vyote--wanyama wa mwituni, ndege, nyoka na viumbe vya baharini.
7Jah, igasuguste loomade ja lindude, roomajate ja mereelajate loomust suudab taltsutada ja ongi taltsutanud inimese loomus,
8Lakini hakuna mtu aliyeweza kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu inayoua.
8aga ükski inimene ei suuda taltsutada keelt, seda kärsitut pahategijat, mis on tulvil surmavat mürki.
9Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huohuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
9Sellesamaga me õnnistame Issandat ja Isa, ja sellesamaga me neame inimesi, kes on sündinud Jumala sarnasteks.
10Maneno ya laana na ya kusifia hutoka katika kinywa kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo.
10Ühest ja samast suust tuleb õnnistamine ja needmine. Nii ei tohi olla, mu vennad!
11Je, chemchemi moja yaweza kutoa maji matamu na maji machungu pamoja?
11Kas allikast keeb ühest ja samast soonest magedat ja kibedat vett?!
12Ndugu zangu, je, mti wa mtini waweza kuzaa zeituni? Au, mzabibu waweza kuzaa tini? Chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
12Mu vennad, ega viigipuu saa kanda õlimarju ega viinapuu viigimarju?! Nii ei saa ka soolase vee allikas anda magedat vett.
13Je, ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu? Basi, aonyeshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na hekima.
13Kes teie seas on tark ja arusaaja? Las ta näitab hea käitumisega oma tegusid tarkuse tasaduses.
14Lakini ikiwa mioyo yenu imejaa wivu, chuki na ubinafsi, basi, msijisifu na kusema uongo dhidi ya ukweli.
14Kui teie südames on aga kibedat kadedust ja riiakust, siis ärge hoobelge ega valetage tõe vastu!
15Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani.
15See pole ülalt tulev tarkus, vaid maine, hingelik, deemonlik.
16Maana popote palipo na wivu na ubinafsi hapo pana fujo na kila aina ya uovu.
16Sest kus on kadedust ja riiakust, seal on kärsitust ja igasuguseid halbu tegusid.
17Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki.
17Aga ülalt pärinev tarkus on esmalt puhas, siis rahumeelne, leebe, kuulekas, tulvil halastust ja häid vilju, erapooletu, teeskluseta.
18Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.
18Rahutegijaile külvatakse rahus õiguse vilja.