1Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
1Aga enne paasapühi, kui Jeesus teadis, et tema tund on tulnud minna sellest maailmast ära Isa juurde, siis tema, kes oli armastanud omi selles maailmas, armastas neid lõpuni.
2Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
2Ja õhtusöömaajal olles, kui kurat oli juba pannud Juudas Iskarioti, Siimona poja südamesse, et ta tema reedaks,
3Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
3ja kui Jeesus teadis, et Isa on andnud tema kätte kõik ning et ta on pärit Jumala juurest ja läheb tagasi Jumala juurde,
4Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
4tõusis ta õhtusöömaajalt üles, pani oma kuue ära, võttis rätiku ning sidus selle endale vööle.
5Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
5Seejärel kallas ta vett vaagnasse ning hakkas pesema jüngrite jalgu ja kuivatama rätikuga, mis oli tal vööl.
6Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, "Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?"
6Siis tuli ta Siimon Peetruse juurde. Too ütles temale: 'Issand, kas sina tahad pesta minu jalgu?'
7Yesu akamjibu, "Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye."
7Jeesus vastas: 'Mida mina teen, seda sina praegu ei tea, aga küll sa pärast saad aru.'
8Petro akamwambia, "Wewe hutaniosha miguu kamwe!" Yesu akamjibu, "Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena."
8Peetrus ütles talle: 'Mitte mingil juhul ei pese sina mu jalgu!' Jeesus vastas talle: 'Kui mina sind ei pese, siis ei ole sul osa minuga.'
9Simoni Petro akamwambia, "Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia."
9Siimon Peetrus ütles talle: 'Issand, ära siis pese üksnes mu jalgu, vaid ka käsi ja pead.'
10Yesu akamwambia, "Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote."
10Jeesus ütles talle: 'Puhtaks pestul ei ole vaja pesta muud kui jalgu, sest ta on üleni puhas. Ka teie olete puhtad, kuid mitte kõik.'
11(Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: "Ninyi mmetakata, lakini si nyote.")
11Ta ju teadis, kes tema reedab, seepärast ta ütleski: 'Teie ei ole kõik puhtad.'
12Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, "Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
12Kui ta nüüd nende jalad oli pesnud ja oma kuue võtnud ning jälle lauda asunud, ütles ta neile: 'Kas te saate aru, mida ma olen teile teinud?
13Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
13Te hüüate mind 'Õpetaja' ja 'Issand', ja seda te ütlete õigesti, sest see ma olen.
14Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
14Kui nüüd mina, Issand ja Õpetaja, olen teie jalgu pesnud, siis tuleb teilgi pesta üksteise jalgu,
15Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
15sest ma olen teile andnud eeskuju, et teiegi teeksite nõnda, nagu mina olen teile teinud.
16Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
16Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, ei ole teener suurem kui ta isand ega saadik suurem kui see, kes tema on saatnud.
17Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
17Kui te seda teate, siis olete õndsad, kui nõnda ka teete.
18"Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
18Ma ei ütle seda teie kõikide kohta. Mina tean, keda ma olen valinud. Kuid Kiri peab minema täide: 'See, kes minu leiba sööb, on pöördunud minu vastu.'
19Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
19Ma ütlen teile seda juba praegu, enne kui see sünnib, et kui see sünnib, te usuksite, et mina olen see.
20Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma."
20Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, kes võtab vastu selle, kelle mina saadan, see võtab vastu minu, aga kes võtab vastu minu, see võtab vastu tema, kes on minu saatnud.'
21Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!"
21Seda öelnud, võpatas Jeesus vaimus ja tunnistas: 'Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, üks teie seast reedab minu.'
22Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
22Jüngrid vaatasid nõutuses üksteisele otsa ega osanud arvata, kelle kohta ta seda ütleb.
23Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
23Üks ta jüngritest, see, keda Jeesus armastas, oli tema kõrval lauas.
24Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: "Mwulize anasema juu ya nani."
24Siimon Peetrus noogutas nüüd peaga selle poole, öeldes: 'Küsi temalt, kes see on, kellest ta räägib?'
25Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, "Bwana, ni nani?"
25See jünger nõjatus siis Jeesuse rinnale ja ütles talle: 'Issand, kes see on?'
26Yesu akajibu, "Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye." Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
26Siis vastas Jeesus: 'Seesama, kelle jaoks ma kastan palakese ja annan talle.' Siis ta kastis palakese ja andis Juudas Iskariotile, Siimona pojale.
27Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, "Unachotaka kufanya, kifanye haraka!"
27Ja palakese järel läks saatan temasse. Jeesus ütles talle nüüd: 'Mida sa teed, tee kiiresti!'
28Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
28Lauasistujatest ei taibanud aga keegi, mille kohta Jeesus talle nii ütles,
29Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
29sest mõned arvasid, kuna Juudas oli kukruhoidja, et Jeesus ütles talle: 'Osta, mida vajame pühadeks!' või et ta käskis anda midagi vaestele.
30Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
30Kui siis Juudas oli võtnud palakese vastu, lahkus ta kohe. Aga oli öö.
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, "Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
31Kui nüüd Juudas oli lahkunud, ütles Jeesus: 'Nüüd on Inimese Poeg kirgastatud ja Jumal on temas kirgastatud.
32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
32Kui Jumal on temas kirgastatud, siis kirgastab Jumal temas ka ennast ja ta kirgastab teda just nüüd.
33"Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
33Lapsed, ma olen teiega veel pisut aega. Te hakkate mind otsima, ja nagu ma ütlesin juutidele: 'Kuhu mina lähen, sinna ei saa teie tulla', nii ütlen ma praegu ka teile.
34Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
34Ma annan teile uue käsu: armastage üksteist! Nõnda nagu mina teid olen armastanud, armastage teiegi üksteist!
35Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu."
35Sellest tunnevad kõik, et te olete minu jüngrid, kui te üksteist armastate.'
36Simoni Petro akamwuliza, "Bwana, unakwenda wapi?" Yesu akajibu, "Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye."
36Siimon Peetrus küsis temalt: 'Issand, kuhu sa lähed?' Jeesus vastas: 'Kuhu mina lähen, sinna ei saa sina mulle praegu järgneda, aga sa järgned hiljem.'
37Petro akamwambia "Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!"
37Peetrus ütles talle: 'Issand, miks ma siis praegu ei saa sulle järgneda? Ma annan oma elu sinu eest.'
38Yesu akajibu, "Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!"
38Jeesus vastas: 'Kas sina annad oma elu minu eest? Tõesti, tõesti, ma ütlen sulle, kukk ei laula enne, kui sina oled mind juba kolm korda salanud.