1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
1Pärast seda läks Jeesus teisele poole Galilea ehk Tibeeriase järve.
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
2Ja temaga läks kaasa suur rahvahulk, sest nad olid näinud tunnustähti, mida ta haigetele tegi.
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
3Aga Jeesus läks mäele ning istus sinna koos oma jüngritega.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
4Ent paasa, juutide püha, oli ligi.
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
5Kui nüüd Jeesus oma silmad üles tõstis ja nägi palju rahvast enese juurde tulevat, siis ta ütles Filippusele: 'Kust me ostame leiba, et need saaksid süüa?'
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
6Aga seda ta ütles teda proovile pannes, sest ta teadis küll, mida ta kavatseb teha.
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
7Filippus vastas talle: 'Isegi kahesaja teenari eest ostetud leibadest ei jätku neile, et igaüks pisutki saaks.'
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
8Andreas, üks ta jüngritest, Siimon Peetruse vend, ütles talle:
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
9'Siin on üks poiss, kellel on viis odraleiba ja kaks kalakest. Kuid mis sellest saab nii paljudele?'
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
10Jeesus ütles: 'Pange inimesed istuma!' Seal paigas oli palju rohtu. Siis istusid nad maha, seal oli arvult umbes viis tuhat meest.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
11Jeesus võttis nüüd leivad, tänas Jumalat ja andis neile, kes maas istusid, samuti ka kalakestest, niipalju kui nad tahtsid.
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
12Aga kui nende kõhud olid täis saanud, ütles Jeesus oma jüngritele: 'Koguge ülejäänud palakesed kokku, et midagi ei läheks raisku!'
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
13Siis kogusid nad viiest odraleivast kokku kaksteist korvitäit palakesi, mis oli sööjatest üle jäänud.
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
14Kui nüüd rahvas nägi tunnustähte, mille Jeesus oli teinud, ütlesid nad: 'Tema on tõesti see prohvet, kes peab tulema maailma.'
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
15Nüüd sai Jeesus aru, et nad tahavad tulla ja teda vägisi kuningaks teha, ja ta tõmbus mägedesse üksindusse.
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
16Aga õhtu jõudes läksid Jeesuse jüngrid alla järve äärde
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
17ja astusid paati ning sõitsid teisele poole järve Kapernauma. Oli juba läinud pimedaks, ja Jeesus ei olnud ikka veel tulnud nende juurde.
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
18Ka puhus tugev tuul ja pani järvel tõusma kõrged lained.
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
19Nad olid nüüd sõudnud umbes kolm-neli miili, kui nägid Jeesust järvel kõndivat ja paadi lähedale jõudvat, ja nad lõid kartma.
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
20Aga Jeesus ütles neile: 'See olen mina, ärge kartke!'
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
21Siis nad tahtsid ta paati võtta, aga kohe jõudiski paat kaldale, kuhu nad olid tahtnud sõita.
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
22Järgmisel päeval nägi järve kaldal seisev rahvahulk, et seal oli ainult üks paat. Nad teadsid, et Jeesus ei olnud astunud paati koos oma jüngritega, vaid ta jüngrid olid ära läinud üksi.
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
23Tibeeriasest tuli veel teisi paate selle paiga lähedale, kus nad olid söönud Issanda õnnistatud leiba.
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
24Kui siis rahvahulk nägi, et seal ei olnud ei Jeesust ega ta jüngreid, astusid nad paatidesse ning tulid Jeesust otsides Kapernauma.
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
25Ja kui nad leidsid ta teiselt poolt järve, ütlesid nad talle: 'Rabi, millal sa siia said?'
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
26Jeesus vastas neile: 'Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, te ei otsi mind mitte sellepärast, et te nägite tunnustähti, vaid et te sõite leiba ja teie kõhud said täis.
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
27Ärge nõutage rooga, mis hävib, vaid rooga, mis püsib igaveseks eluks. Seda annab teile Inimese Poeg, sest teda on Jumal Isa pitseriga kinnitanud.'
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
28Siis nad ütlesid talle: 'Mida me peame ette võtma, et teha Jumala tegusid?'
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
29Jeesus vastas: 'See ongi Jumala tegu, et te usute temasse, kelle ta on läkitanud.'
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
30Siis nad ütlesid talle: 'Mis tunnustähe sa siis teed, et me näeksime ja võiksime sind uskuda? Mida sa teed?
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
31Meie esiisad sõid kõrbes mannat, nõnda nagu on kirjutatud: Ta andis neile süüa leiba taevast.'
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
32Siis ütles Jeesus neile: 'Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, ei andnud Mooses teile leiba taevast, vaid minu Isa annab teile tõelist leiba taevast.
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
33Sest Jumala leib on see, kes tuleb taevast alla ja annab maailmale elu.'
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
34Siis nad ütlesid talle: 'Issand, anna meile alati seda leiba!'
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
35Jeesus ütles neile: 'Mina olen eluleib. Kes minu juurde tuleb, see ei nälgi iialgi, ja kes minusse usub, see ei janune enam iialgi.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
36Kuid ma olen teile öelnud, et kuigi te olete mind näinud, ei usu te ikkagi.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
37Kõik, mis Isa mulle annab, tuleb minu juurde, ning kes minu juurde tuleb, seda ma ei aja välja.
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
38Ma ei ole ju taevast alla tulnud oma tahtmist tegema, vaid tema tahtmist, kes minu on saatnud.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
39Aga tema tahtmine, kes minu on saatnud, on see, et ma ei kaotaks midagi sellest, mis mulle on antud, vaid et ma ärataksin nad üles viimsel päeval.
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
40See ongi mu Isa tahtmine, et igaühel, kes näeb Poega ning temasse usub, oleks igavene elu, ja viimsel päeval mina äratan ta üles.'
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
41Siis nurisesid juudid Jeesuse üle, et ta ütles: 'Mina olen taevast alla tulnud leib.'
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
42Ja nad laususid: 'Eks see ole Jeesus, Joosepi poeg, kelle isa ja ema me tunneme? Kuidas ta siis nüüd ütleb, et ta on alla tulnud taevast?'
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
43Jeesus vastas neile: 'Ärge nurisege endamisi!
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
44Ükski ei saa tulla minu juurde, kui teda ei tõmba Isa, kes on minu läkitanud, ja mina äratan ta üles viimsel päeval.
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
45Prohvetites on kirjutatud: Siis on nad kõik Jumalalt õppinud. Igaüks, kes Isa on kuulnud ja temalt õppinud, tuleb minu juurde.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
46Mitte keegi ei ole näinud Isa peale selle, kes on Jumala juurest; see on näinud Isa.
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
47Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, kes usub, sellel on igavene elu.
48Mimi ni mkate wa uzima.
48Mina olen eluleib.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
49Teie esiisad sõid kõrbes mannat, ja surid.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
50See on leib, mis taevast alla tuleb, et inimene sellest sööks ega sureks.
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
51Mina olen taevast alla tulnud elav leib. Kui keegi sööb seda leiba, siis ta elab igavesti; ja leib, mille mina annan, on minu liha; ma annan selle maailma elu eest.'
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
52Sellest tõusis juutide keskel suur tüli. Nad küsisid: 'Kuidas saab tema anda meile süüa oma liha?'
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
53Jeesus ütles neile: 'Tõesti, tõesti, ma ütlen teile, kui te ei söö Inimese Poja liha ega joo tema verd, ei ole teie sees elu.
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
54Kes minu liha sööb ning minu verd joob, sellel on igavene elu ja mina äratan ta üles viimsel päeval,
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
55sest minu liha on tõeline roog ja minu veri on tõeline jook.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
56Kes minu liha sööb ning minu verd joob, see jääb minusse ja mina temasse.
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
57Nii nagu elav Isa minu on läkitanud ja mina elan Isa läbi, nii elab ka see, kes mind sööb, minu läbi.
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
58See ongi leib, mis on alla tulnud taevast. See ei ole niisugune leib, mida teie esiisad sõid, ja surid. Aga kes seda leiba sööb, elab igavesti.'
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
59Seda ütles Jeesus Kapernauma sünagoogis õpetades.
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
60Siis paljud tema jüngrid ütlesid seda kuuldes: 'See sõna on ränk, kes suudab seda kuulda?'
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
61Aga Jeesus, kes sisimas teadis, et ta jüngrid selle pärast nurisevad, ütles neile: 'Kas see ärritab teid?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
62Aga mis on veel siis, kui te näete Inimese Poega üles minevat sinna, kus ta oli enne?
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
63Vaim on see, kes elustab, lihast ei ole mingit kasu. Sõnad, mis ma teile olen rääkinud, on vaim ja elu.
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
64Kuid teie seas on mõned, kes ei usu.' Jeesus teadis ju algusest peale, kes on need, kes ei usu, ja kes on see, kes tema reedab.
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
65Ja ta ütles: 'Seepärast ma olengi teile öelnud, et keegi ei saa tulla minu juurde, kui talle ei ole seda andnud Isa.'
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
66Seepeale lahkusid paljud ta jüngritest tema juurest ega käinud enam koos temaga.
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
67Siis ütles Jeesus neile kaheteistkümnele: 'Kas teiegi tahate ära minna?'
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
68Siimon Peetrus vastas talle: 'Issand, kelle juurde me peaksime minema? Sinul on igavese elu sõnad,
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
69ja me oleme uskunud ning ära tundnud, et sina oled Jumala Püha.'
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
70Jeesus vastas neile: 'Eks ma ole teid kahtteistkümmend välja valinud, ent üks teie seast on kurat.'
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.
71Aga seda ta ütles Juudas Iskarioti kohta, sest see kavatses teda reeta, üks neist kaheteistkümnest.