1Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
1Aga pärast seda määras Issand veel seitsekümmend [kaks] ja läkitas nad kahekaupa enese eele igasse linna ja paika, kuhu ta ise tahtis minna.
2Akawaambia, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
2Ta ütles neile: 'Lõikust on palju, töötegijaid aga vähe. Paluge siis lõikuse Issandat, et ta saadaks töötegijaid välja oma lõikusele!
3Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
3Minge! Vaata, ma läkitan teid kui lambaid huntide sekka.
4Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
4Ärge kandke kukrut ega pauna ega jalatseid ja ärge teretage kedagi teel!
5Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
5Aga kui te astute kuhugi majja, ütelge esmalt: 'Rahu olgu sellele kojale!'
6Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
6Ja kui seal on rahulaps, siis hingab teie rahu tema peal, aga kui ei ole, pöördub rahu tagasi teie peale.
7Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
7Aga jääge samasse majja, sööge ja jooge, mis neil on, sest tööline on oma palka väärt! Ärge käige ühest majast teise!
8Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
8Ja kui te lähete kuhugi linna ja teid võetakse vastu, siis sööge, mida teile ette pannakse,
9Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
9ja tehke terveks sealsed haiged ja öelge neile: 'Jumala riik on teie lähedal!'
10Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
10Aga kui te lähete kuhugi linna ja teid ei võeta vastu, minge välja selle tänavaile ja öelge:
11Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
11'Ka tolmu, mis teie linnast meie jalgade külge on hakanud, pühime teile maha. Ometi teadke, et Jumala riik on lähedal!'
12Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
12Ma ütlen teile: Soodomal on sel päeval hõlpsam põli kui tollel linnal.
13"Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
13Häda sulle, Korasin! Häda sulle, Betsaida! Sest kui Tüüroses ja Siidonis oleksid sündinud need vägevad teod, mis teie juures on sündinud, küll nad oleksid ammugi kotiriides ja tuhas istudes parandanud meelt.
14Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
14Ometi on Tüürosel ja Siidonil kohtus hõlpsam põli kui teil.
15Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu."
15Ja sina, Kapernaum, kas sind ülendatakse taevani? Ei, surmavallani tõugatakse sind alla.
16Halafu akasema, "Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma."
16Kes teid kuulda võtab, see võtab kuulda mind, kes teid kõrvale lükkab, see lükkab kõrvale minu, kes aga minu kõrvale lükkab, see lükkab kõrvale mu Läkitaja.'
17Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, "Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako."
17Aga need seitsekümmend [kaks] pöördusid rõõmuga tagasi ja ütlesid: 'Issand, ka kurjad vaimud alistuvad meile sinu nime mõjul!'
18Yeye akawaambia, "Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
18Tema ütles neile: 'Ma nägin saatanat kui välku taevast maha langevat.
19Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
19Vaata, ma olen andnud teile meelevalla kõndida madude ja skorpionide peal ja vaenlase kogu väe peal ja miski ei tee teile iial kahju.
20Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni."
20Ometi ärge rõõmustage sellest, et vaimud teile alistuvad, vaid rõõmustage, et teie nimed on taevasse kirja pandud!'
21Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, "Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza."
21Selsamal tunnil juubeldas Jeesus Pühas Vaimus ja ütles: 'Ma tänan sind, Isa, taeva ja maa Issand, et sa selle oled peitnud tarkade ja mõistlike eest ja oled ilmutanud väetitele! Jah, Isa, sest nõnda on see sündinud sinu head meelt mööda.
22Kisha akasema, "Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo."
22Kõik on mu Isa üle andnud mulle ja keegi ei tunne, kes on Poeg, kui vaid Isa, ja kes on Isa, kui vaid Poeg, ja kellele Poeg seda iganes tahab ilmutada.'
23Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, "Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
23Ja omavahel olles ütles Jeesus jüngrite poole pöördudes: 'Õndsad on silmad, mis näevad seda, mida teie näete,
24Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie."
24sest ma ütlen teile, palju prohveteid ja kuningaid on tahtnud näha, mida teie näete, ega ole näinud, ja kuulda, mida teie kuulete, ega ole kuulnud.'
25Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, "Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?"
25Ja vaata, üks seadusetundja tõusis püsti Jeesust kiusama ja küsis: 'Õpetaja, mis ma pean tegema, et pärida igavest elu?'
26Yesu akamwuliza, "Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?"
26Aga Jeesus ütles talle: 'Mis Seaduses on kirjutatud? Kuidas sa loed?'
27Akamjibu, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
27Tema vastas: 'Armasta Issandat, oma Jumalat, kogu oma südamega ja kogu oma hingega ja kogu oma jõuga ja kogu oma mõistusega, ning oma ligimest kui iseennast!'
28Yesu akawaambia, "Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi."
28Siis Jeesus ütles talle: 'Sa oled õigesti vastanud, tee nii, ja sa elad!'
29Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, "Na jirani yangu ni nani?"
29Tema aga, tahtes iseennast õigustada, küsis Jeesuselt: 'Ja kes siis on mu ligimene?'
30Yesu akamjibu, "Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
30Jeesus ütles kõnelust jätkates: 'Üks inimene läks Jeruusalemmast alla Jeeriko poole ja sattus teeröövlite kätte. Kui need olid ta riided röövinud ja talle hoope andnud, läksid nad ära, jättes ta poolsurnuna maha.
31Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
31Juhtumisi tuli keegi preester sedasama teed, ja kui ta teda nägi, läks ta kaarega mööda.
32Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
32Nõndasamuti ka leviit, kui ta sattus sinna paika ja teda nägi, läks ringiga mööda.
33Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
33Aga sama teed tuli üks samaarlane. Kui ta jõudis temani ja teda nägi, hakkas tal hale
34Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
34ja ta astus ligi, sidus mehe haavad, valas nende peale õli ja veini, tõstis ta oma muula selga, viis öömajale ning kandis hoolt tema eest.
35Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi."
35Ja järgmisel hommikul võttis ta välja kaks teenarit, andis need peremehele ja ütles: 'Kanna tema eest hoolt, ja kui sa midagi veel lisaks peaksid kulutama, selle maksan mina sulle tagasi tulles.'
36Kisha Yesu akauliza, "Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?"
36Kes neist kolmest oli sinu arvates ligimene inimesele, kes oli sattunud teeröövlite kätte?'
37Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, "Ni yule aliyemwonea huruma." Yesu akamwambia, "Nenda ukafanye vivyo hivyo."
37Seadusetundja ütles: 'See, kes tema peale halastas.' Jeesus ütles talle: 'Siis mine ja tee sina nõndasamuti!'
38Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
38Aga kui nad teed käisid, astus Jeesus sisse ühte külla. Keegi naine, Marta nimi, võttis ta vastu.
39Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
39Ja sel naisel oli õde, keda hüüti Maarjaks. Maarja istus maha Issanda jalgade juurde ja kuulas tema kõnet.
40Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, "Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie."
40Marta aga oli ametis mitmesuguste toimetustega. Ja ta tuli Jeesuse juurde ning ütles: 'Issand, kas sa ei hooli sellest, et mu õde jättis mu üksinda toimetama? Ütle talle nüüd, et ta tuleks mulle appi!'
41Lakini Bwana akamjibu, "Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
41Aga Issand vastas talle: 'Marta, Marta, sa muretsed ja vaevad ennast paljude asjadega,
42Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya."
42aga tarvis on vaid üht. Maarja on ju valinud hea osa, mida ei võeta temalt ära.'