Swahili: New Testament

Estonian

Luke

16

1Yesu aliwaambia wanafunzi wake: "Tajiri mmoja alikuwa na karani wake. Huyu karani alichongewa kwamba alitumia ovyo mali ya tajiri wake.
1Aga Jeesus ütles ka jüngritele: 'Oli üks rikas inimene, kellel oli mõisavalitseja, kelle peale oli talle kaevatud, nagu pillaks see tema vara.
2Yule tajiri akamwita akamwambia: Ni mambo gani haya ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya mapato na matumizi ya mali yangu, kwa maana huwezi kuwa karani tena.
2Ja mees kutsus mõisavalitseja ja ütles talle: 'Mis see on, mis ma sinu kohta kuulen? Anna aru oma valitsemisest, sest sa ei või enam valitseda!'
3Yule karani akafikiri: Bwana wangu amenifukuza kazi ya ukarani; nitafanya nini? Kwenda kulima siwezi; kwenda kuombaomba kama maskini ni aibu.
3Aga mõisavalitseja mõtles endamisi: 'Mis ma pean tegema, kui isand võtab valitsemise minu käest ära? Maad kaevata ma ei jaksa, kerjata häbenen.
4Naam, najua la kufanya, ili nitakapofukuzwa kazi, watu waweze kunikaribisha nyumbani kwao.
4Küll ma tean, mida ma teen, et inimesed võtaksid mind vastu oma kodadesse, kui mind tagandatakse valitsemast!'
5Basi, akawaita wadeni wa bwana wake, mmoja mmoja, akamwambia yule wa kwanza: Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?
5Ja ta laskis enda juurde kutsuda üksteise järel oma isanda võlglased. Esimesele ta ütles: 'Kui palju sa võlgned mu isandale?'
6Yeye akamjibu: Mapipa mia ya mafuta ya zeituni. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, keti haraka, andika hamsini.
6See ütles: 'Sada vaati õli.' Tema aga ütles talle: 'Võta oma võlatäht, istu ja kirjuta kähku viiskümmend!'
7Kisha akamwuliza mdeni mwingine: Wewe unadaiwa kiasi gani? Yeye akamjibu: Magunia mia ya ngano. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, andika themanini.
7Seejärel ta küsis teiselt: 'Aga kui palju sina võlgned?' See ütles: 'Sada tündrit nisu.' Sellele ütles valitseja: 'Võta oma võlatäht ja kirjuta kaheksakümmend!'
8"Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga."
8Ja isand kiitis ülekohtust mõisavalitsejat, et ta oli käitunud arukalt, sest selle ajastu lapsed on omasuguste suhtes arukamad kui valguse lapsed.
9Naye Yesu akaendelea kusema, "Nami nawaambieni, jifanyieni marafiki kutokana na mali ya dunia, ili zitakapowaishieni, mweze kupokewa nao katika makao ya milele.
9Minagi ütlen teile: Tehke endile sõpru ülekohtuse mammonaga, et kui see saab otsa, teid võetaks igavestesse telkidesse.
10Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, atakuwa mwaminifu katika mambo makubwa; na yeyote asiye mwaminifu katika mambo madogo, hatakuwa mwaminifu katika mambo makubwa.
10Kes on ustav pisimas, see on ustav ka paljus, ja kes on ülekohtune pisimas, see on ülekohtune ka paljus.
11Kama basi, ninyi si hamjawa waaminifu mali mbaya za dunia, ni nani atakayewakabidhi zile mali za kweli?
11Kui te nüüd ülekohtuses mammonas ei ole olnud ustavad, kes võib teie kätte usaldada tõelist?
12Na kama hamjakuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewakabidhi mali yenu wenyewe?
12Ja kui te võõra varaga ei ole olnud ustavad, kes annaks teile kätte teie oma?
13"Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au ataambatana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali."
13Ükski sulane ei või teenida kahte isandat, ikka on nii, et ta vihkab üht ja armastab teist või et ta pooldab üht ja põlgab teist. Te ei saa orjata Jumalat ja mammonat!'
14Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, kwa vile wao walikuwa wanapenda sana fedha, wakamdharau Yesu.
14Aga seda kõike kuulsid ka variserid, kes olid rahaahned, ja nad irvitasid Jeesuse üle.
15Hapo akawaambia, "Ninyi mnajifanya wema mbele ya watu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana kile kinachoonekana kuwa kitukufu mbele ya watu, Mungu anakiona kuwa takataka.
15Ja ta ütles neile: 'Teie olete need, kes end õigena näitavad inimeste silmis. Aga Jumal tunneb teie südant, sest mis inimeste seas on kõrge, see on Jumala ees jäledus.
16"Sheria na maandishi ya manabii vilikuweko mpaka wakati wa Yohane mbatizaji. Tangu hapo, Ufalme wa Mungu unahubiriwa, na kila mmoja anauingia kwa nguvu.
16Moosese Seadus ja Prohvetid ulatuvad Johanneseni. Sellest ajast peale kuulutatakse evangeeliumi Jumala riigist ja igaüks tungib väevõimul sinna sisse.
17Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita, kuliko hata herufi moja ya Sheria kufutwa.
17Aga hõlpsamini kaovad taevas ja maa kui üksainus kriipsuke Seadusest.
18"Yeyote anayemwacha mke wake na kuoa mwingine, anazini; na yeyote anayemwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
18Igaüks, kes ajab minema oma naise ja võtab teise, rikub abielu, ja kes võtab minemaaetud naise, rikub abielu.
19"Palikuwa na mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa anavaa mavazi ya bei kubwa sana ya rangi ya zambarau, na ya kitani safi, na kufanya sherehe kila siku.
19Oli üks rikas inimene ja tal oli kombeks rõivastuda purpurisse ja peenlinasesse, pidutsedes päevast päeva rõõmsasti.
20Kulikuwa pia na maskini mmoja jina lake Lazaro, aliyekuwa amejaa vidonda na alikuwa analazwa mlangoni pa nyumba ya huyo tajiri.
20Aga üks vaene, Laatsarus nimi, oli maas tema värava ees, täis paiseid,
21Lazaro alitamani kula makombo yaliyoanguka kutoka meza ya tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kulamba vidonda vyake!
21ja püüdis oma kõhtu täita leivaraasukestega, mis rikka laualt kukkusid. Kuid koeradki tulid ja lakkusid tema paiseid.
22"Ikatokea kwamba huyo maskini akafa, malaika wakamchukua, wakamweka karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa.
22Siis sündis, et vaene suri, ja inglid kandsid ta Aabrahami sülle. Aga ka rikas suri ja maeti maha.
23Huyo tajiri, alikuwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye.
23Ja põrgus piineldes tõstis ta oma silmad üles ja nägi Aabrahami kaugelt ja Laatsarust tema süles.
24Basi, akaita kwa sauti: Baba Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno katika moto huu.
24Ja ta hüüdis: 'Isa Aabraham, halasta minu peale ja saada Laatsarus, et ta kastaks oma sõrmeotsa vette ja jahutaks mu keelt, sest ma tunnen suurt valu selles leegis!'
25Lakini Abrahamu akamjibu: Kumbuka mwanangu, kwamba ulipokea mema yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe unateswa.
25Aga Aabraham ütles: 'Laps, tuleta meelde, et sa oled oma hea põlve elus kätte saanud, ja nõndasamuti Laatsarus halva. Nüüd lohutatakse teda siin, sina aga tunned valu.
26Licha ya hayo, kati yetu na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja kwenu kutoka huku wasiweze, wala wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze.
26Ja pealegi on meie ja teie vahele seatud suur kuristik, et need, kes tahavad siit teie juurde minna, ei saa, ega tulda ka sealt meie juurde.'
27Huyo aliyekuwa tajiri akasema: Basi baba, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu,
27Aga tema ütles: 'Ma palun siis sind, isa, et sa saadaksid Laatsaruse mu isakotta,
28maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso.
28sest mul on viis venda, et ta hoiataks neid, et nemadki ei satuks siia piinapaika!'
29Lakini Abrahamu akamwambia: Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao.
29Kuid Aabraham ütles: 'Neil on Mooses ja Prohvetid, kuulaku nad neid!'
30Lakini yeye akasema: Sivyo baba Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka wafu na kuwaendea, watatubu.
30Ent tema ütles: 'Ei sugugi, isa Aabraham, vaid kui keegi surnuist nende juurde läheks, siis nad parandaksid meelt!'
31Naye Abrahamu akasema: Kama hawawasikilizi Mose na manabii, hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka wafu."
31Aabraham aga ütles talle: 'Kui nad ei kuula Moosest ja Prohveteid, ei neid veena siis ka see, kui keegi surnuist üles tõuseks!''