1Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
1Siis Jeesus kõneles rahvale ja oma jüngritele:
2"Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
2'Moosese asemele on istunud kirjatundjad ja variserid.
3Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
3Kõike nüüd, mida nad iganes teile ütlevad, seda tehke ja pidage, aga ärge tehke nende tegusid mööda, sest nad räägivad küll, aga ise ei tee!
4Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
4Nad seovad kokku ränki ja vaevukantavaid koormaid ja panevad need inimeste õlgadele, ise aga ei taha sõrmeotsagagi neid liigutada.
5Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
5Kõiki oma tegusid teevad nad selleks, et inimesed neid vaataksid. Nad teevad oma palvepaelad laiemaks ja palvetupsud suuremaks.
6Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
6Nad armastavad esimesi kohti võõruspidudel ja esimesi istmeid sünagoogides
7Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
7ja teretamisi turgudel ja seda, et inimesed hüüaksid neid rabiks.
8Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
8Teie ärge laske endid hüüda rabiks, sest ainult üks on teie Õpetaja, teie kõik olete aga vennad!
9Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
9Ja ärge hüüdke kedagi maa peal oma isaks, sest ainult üks on teie Isa, see taevane!
10Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
10Ärge laske end ka kellelgi hüüda juhatajaks, sest ainult üks on teie Juhataja - Kristus!
11Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
11Aga suurim teie seast olgu teie teenija!
12Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
12Kes ennast ise ülendab, seda alandatakse, ja kes ennast ise alandab, seda ülendatakse.
13"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
13Aga häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad, et te lukustate taevariigi inimeste eest! Ise te ei lähe sinna sisse ega lase sisse ka neid, kes tahaksid minna.
14Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
14[Häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad, et te neelate alla lesknaiste majad ja silmakirjaks venitate palvetused pikaks! Seepärast te saate seda rängema kohtuotsuse.]
15"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe.
15Häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad! Te rändate läbi mered ja mandrid, et pöörata kas või üks oma usku, ja kui see sünnib, siis te teete temast põrgulise, kahevõrra niisuguse, kui te ise olete.
16"Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
16Häda teile, te sõgedad teejuhid, kes te ütlete: 'Kes iganes vannub templi juures, selle vanne ei loe midagi, kes aga iganes vannub templi kulla juures, see on kohustatud vannet täitma.'
17Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
17Te rumalad ja sõgedad! Kumb on suurem, kas kuld või tempel, mis kulla pühitseb?
18Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
18Te ütlete: 'Kes iganes vannub altari juures, selle vanne ei loe midagi, aga kes iganes vannub altaril oleva ohvrianni juures, see on kohustatud vannet täitma.'
19Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
19Teie sõgedad, kumb siis on suurem, kas ohvriand või altar, mis ohvrianni pühitseb?
20Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
20Niisiis, kes vannub altari juures, see vannub selle ja kõige juures, mis on altaril,
21Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
21ja kes vannub templi juures, see vannub selle ja tema juures, kes templis elab,
22Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
22ja kes vannub taeva juures, see vannub Jumala trooni ja troonil istuja juures.
23Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
23Häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad, et te maksate kümnist mündist ja tillist ja köömnest ning jätate kõrvale kaalukama osa Seadusest - õigluse ja halastuse ja ustavuse! Üht tuleb teha, kuid teist ei tohi jätta kõrvale!
24Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
24Te sõgedad teejuhid, te kurnate välja küll sääsed, aga kaamelid neelate alla.
25"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
25Häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad, sest te puhastate karika ja liua väljastpoolt, aga seest on need täis riisumist ja aplust!
26Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
26Sa sõge variser! Puhasta enne karikas seestpoolt, et see ka väljast saaks puhtaks!
27"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
27Häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad, sest te sarnanete lubjatud haudadega, mis väljastpoolt paistavad küll nägusad, aga seestpoolt on täis surnuluid ja kõiksugust roisku!
28Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
28Nõnda paistate ka teie inimestele õigetena, aga seestpoolt olete täis silmakirjatsemist ja ülekohut.
29"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
29Häda teile, kirjatundjad ja variserid, te silmakirjatsejad, sest te ehitate prohvetite hauamärke ja ehite õigete hauakambreid
30Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
30ja ütlete: 'Kui meie oleksime elanud oma esiisade päevil, siis meie küll ei oleks olnud nende kaasosalised prohvetite vere valamisel.'
31Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
31Nõnda te tunnistate ise eneste kohta, et teie olete prohvetite tapjate pojad.
32Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
32Täitke siis teiegi oma vanemate mõõt!
33Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu?
33Te maod, te rästikute sugu, kuidas te võiksite põgeneda ära põrgu kohtust?
34Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
34Seepärast, vaata, mina läkitan teie juurde prohveteid ja tarku ja kirjatundjaid ning osa te tapate ja lööte risti ning osa te piitsutate oma sünagoogides ja jälitate neid linnast linna,
35Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
35et teie peale tuleks kõik õige veri, mis on valatud maa peal õige Aabeli verest kuni Berekja poja Sakarja vereni, kelle te tapsite templi ja altari vahel.
36Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
36Tõesti, ma ütlen teile, see kõik tuleb selle sugupõlve peale!
37"Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
37Jeruusalemm, Jeruusalemm, kes sa tapad prohveteid ja viskad kividega surnuks need, kes su juurde on läkitatud! Kui palju kordi olen ma tahtnud su lapsi koguda, otsekui kana kogub oma pesakonna tiibade alla, ent teie ei ole tahtnud!
38Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
38Vaata, teie koda jäetakse maha,
39Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."
39sest ma ütlen teile, et teie ei näe mind nüüdsest enam, kuni te ütlete: Õnnistatud olgu, kes tuleb Issanda nimel!'