1Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
1Aga varahommikul langetasid kõik ülempreestrid ja rahvavanemad Jeesuse kohta otsuse, et ta tuleb surmata,
2Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
2ja viisid ta aheldatult ära ning andsid maavalitseja Pilaatuse kätte.
3Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
3Kui siis tema reetja Juudas nägi, et Jeesus oli mõistetud surma, kahetses ta ja viis need kolmkümmend hõberaha ülempreestritele ja vanematele tagasi,
4Akawaambia, "Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe." Lakini wao wakasema, "Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako."
4öeldes: 'Ma olen teinud pattu, olen süütu vere ära andnud.' Nemad aga vastasid: 'Mis see meie asi on? Vaata ise!'
5Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
5Ja visanud hõberahad templisse maha, Juudas eemaldus, läks ära ja poos enese üles.
6Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, "Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu."
6Aga ülempreestrid ütlesid neid hõberahasid üles korjates: 'Neid ei tohi templivaramusse panna, sest see on vere hind.'
7Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
7Nad võtsid nõuks osta nende eest potissepa põllu matmispaigaks muulastele.
8Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
8Seepärast hüütakse seda põldu Verepõlluks tänini.
9Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: "Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
9Siis läks täide, mis prohvet Jeremija kaudu on räägitud: 'Ja nad võtsid kolmkümmend hõberaha, hinna, mille vääriliseks Iisraeli lapsed ta olid hinnanud,
10wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza."
10ja andsid need potissepa põllu eest, nii nagu Issand mind oli käskinud.'
11Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, "Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamwambia, "Wewe umesema."
11Jeesus pandi aga seisma maavalitseja ette, ja maavalitseja küsis temalt: 'Sina oled siis juutide kuningas?' Aga Jeesus lausus: 'Need on sinu sõnad.'
12Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
12Ent ülempreestrite ja vanemate kaebuste peale tema kohta ei vastanud Jeesus midagi.
13Hivyo Pilato akamwuliza, "Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?"
13Siis ütles Pilaatus talle: 'Kas sa ei kuule, mida kõike nad sinu vastu tunnistavad?'
14Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
14Tema ei vastanud talle selle peale ainsatki sõna, nõnda et maavalitseja pani seda väga imeks.
15Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
15Maavalitsejal oli aga tava vastu pühi lasta vabaks üks vang, keda rahvahulk tahtis.
16Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
16Tollal oli vangide seas Barabase-nimeline kurikuulus mees.
17Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, "Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?"
17Kui nad nüüd koos olid, küsis Pilaatus neilt: 'Kumma te tahate, et ma lasen teile vabaks, kas Barabase või Messiaks nimetatud Jeesuse?'
18Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
18Ta ju teadis, et nad olid Jeesuse kadeduse pärast tema kätte andnud.
19Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: "Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake."
19Aga kui Pilaatus istus kohtujärjel, saatis ta naine talle sõna: 'Ärgu olgu sul midagi tegemist selle õigega, sest ma olen täna öösel unenäos tema pärast palju kannatanud!'
20Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
20Ülempreestrid ja vanemad keelitasid aga rahvahulki, et need nõuaksid Barabast, Jeesuse aga laseksid hukata.
21Mkuu wa mkoa akawauliza, "Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?" Wakamjibu, "Baraba!"
21Maavalitseja küsis veel kord: 'Kumma neist kahest te tahate, et ma vabaks laseksin?' Nemad vastasid: 'Barabase!'
22Pilato akawauliza, "Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?" Wote wakasema, "Asulubiwe!"
22Pilaatus küsis neilt: 'Mis ma siis pean tegema Jeesusega, keda nimetatakse Messiaks?' Nad kõik ütlesid: 'Löödagu risti!'
23Pilato akauliza, "Kwa nini? Amefanya kosa gani?" Wao wakazidi kupaaza sauti: "Asulubiwe!"
23Aga tema lausus: 'Miks nii, mis halba on ta siis teinud?' Rahvahulk karjus aga veel valjemini: 'Löödagu risti!'
24Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, "Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe."
24Kui siis Pilaatus nägi, et ta midagi ei võinud parata, vaid lärm läks aina suuremaks, siis ta võttis vett ja pesi rahvahulga ees oma käsi, öeldes: 'Ma olen süüta selle verest! Küll te näete!'
25Watu wote wakasema, "Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!"
25Ja kogu rahvas kostis talle: 'Tema veri tulgu meie ja meie laste peale!'
26Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
26Siis ta laskis neile vabaks Barabase, Jeesust aga laskis piitsutada ja andis ta risti lüüa.
27Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
27Siis võtsid maavalitseja sõdurid Jeesuse kaasa kohtukotta ja kogusid tema kallale terve väesalga.
28Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
28Ja nad võtsid ta riidest lahti ja panid talle selga punase mantli.
29Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, "Shikamoo mfalme wa Wayahudi!"
29Ja pununud kibuvitstest pärja, panid selle talle pähe ja pilliroo ta paremasse kätte ja tema ette põlvili heites teotasid teda: 'Tervist, juutide kuningas!'
30Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
30Ja nad sülitasid ta peale ja võtsid pilliroo ning lõid talle pähe.
31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
31Ja kui nad olid teda küllalt teotanud, tõmbasid nad tal mantli seljast ja riietasid Jeesuse ta oma rõivastesse ja viisid ta ära ristilöömiseks.
32Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
32Välja minnes leidsid nad Küreene mehe, nimega Siimon, seda nad sundisid kandma Jeesuse risti.
33Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la kichwa,"
33Ja kui nad jõudsid paika, mida hüütakse Kolgataks - see tähendab Pealuu paigaks -,
34wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
34andsid nad Jeesusele juua sapiga segatud veini. Kui ta seda oli maitsnud, siis ta ei tahtnud juua.
35Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35Aga kui nad tema olid risti löönud, jagasid nad liisku heites ta rõivad omavahel
36Wakaketi, wakawa wanamchunga.
36ja istusid maha ning valvasid teda seal.
37Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, "Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi."
37Ja nad panid ta pea kohale kirja tema süüga: 'See on Jeesus, juutide kuningas.'
38Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
38Siis nad lõid koos Jeesusega risti kaks teeröövlit, ühe ta paremale ja teise vasemale käele.
39Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
39Möödujad aga parastasid teda päid vangutades:
40"Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!"
40'Sina, kes lammutad templi ja kolme päevaga üles ehitad, päästa iseennast! Kui sa oled Jumala Poeg, siis astu ristilt alla!'
41Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
41Nõndasamuti teotasid teda ka ülempreestrid koos kirjatundjate ja vanematega:
42"Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
42'Teisi on ta päästnud, iseennast ei suuda päästa. On ta Iisraeli kuningas, astugu nüüd ristilt alla ja me usume temasse!
43Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka."
43Ta on lootnud Jumala peale, eks tema päästku ta, kui ta teda tahab, ta ju ütleb, et ta on Jumala Poeg.'
44Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
44Just niisamuti teotasid teda ka koos temaga ristilöödud teeröövlid.
45Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
45Keskpäeval aga tuli pimedus üle kogu maa kuni kella kolmeni pärast lõunat.
46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eli, Eli, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
46Kella kolme paiku aga kisendas Jeesus valju häälega: 'Elii, elii, lemaa sabahtani?' - see tähendab: 'Mu Jumal, mu Jumal, miks sa mu maha jätsid?'
47Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, "Anamwita Eliya."
47Aga mõned sealseisjaist laususid seda kuuldes: 'See hüüab Eelijat appi!'
48Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
48Ja kohe jooksis üks nende seast ja võttis äädikaga immutatud käsna, pistis selle roo otsa ja pakkus talle juua.
49Wengine wakasema, "Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa."
49Aga teised rääkisid: 'Noh olgu, eks me näe, kas Eelija tuleb teda päästma!'
50Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
50Jeesus aga, kisendades taas valju häälega, heitis hinge.
51Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
51Ja ennäe, templi vahevaip kärises ülalt alla kaheks ja maa värises ja kaljud murdusid
52makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
52ja hauakambrid avanesid ja ärkas üles palju magama uinunud pühade ihusid
53nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
53ja need tulid hauakambritest välja ja läksid pärast tema surnuist ülesäratamist pühasse linna ja paljud said seda näha.
54Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu."
54Aga kui väeülem ja need, kes koos temaga Jeesust valvasid, nägid maavärisemist ja seda, mis sündis, lõid nad väga kartma ja ütlesid: 'Tõesti, see oli Jumala Poeg!'
55Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
55Aga seal oli toimuvat eemalt vaatamas palju naisi, kes olid Jeesusele järgnenud Galileast alates teda teenides,
56Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
56nende seas Maarja Magdaleena ja Jaakobuse ja Joosepi ema Maarja ning Sebedeuse poegade ema.
57Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
57Aga õhtu jõudes tuli rikas mees Arimaatiast, nimega Joosep, kes oli ka Jeesuse jünger.
58Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
58See läks Pilaatuse juurde ja palus enesele Jeesuse ihu. Siis Pilaatus käskis selle anda.
59Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
59Ja Joosep võttis ihu, mässis selle puhtasse linasse
60akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
60ja pani oma uude kaljusse raiutud hauakambrisse, ning veeretanud haua ukse ette suure kivi, läks ära.
61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
61Aga Maarja Magdaleena ja teine Maarja olid ka seal, nad istusid haua vastas.
62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
62Järgmisel päeval, see oli pühade valmistuspäevale järgnev hingamispäev, tulid ülempreestrid ja variserid Pilaatuse juurde kokku
63Wakasema, "Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
63ja ütlesid: 'Isand, meile tuleb meelde, et see eksitaja ütles, kui ta alles elas: 'Mina ärkan kolme päeva pärast üles.'
64Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali."
64Käsi nüüd hauda kolmanda päevani valve all pidada, et jüngrid ei tuleks ja teda ära ei varastaks ega ütleks rahvale, et ta on üles äratatud surnuist, sest nii oleks viimane pettus hullem kui esimene.'
65Pilato akawaambia, "Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo."
65Pilaatus lausus neile: 'Siin on teile valvesalk. Minge ning pidage valvet, nii nagu oskate!'
66Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
66Nemad läksid ja võtsid haua valve alla ja koos valvesalgaga pitseerisid kivi.