1Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu.
1Paulus, Kristuse Jeesuse sulane, kutsutud apostel, välja valitud kuulutama Jumala evangeeliumi,
2Hapo kale, Mungu aliwaahidia watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
2mida Jumal on muiste oma prohvetite kaudu pühades kirjades tõotanud
3Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye mintarafu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi;
3oma Pojast - kes liha poolest on sündinud Taaveti soost,
4mintarafu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka wafu.
4ent pühaduse Vaimu poolest määratud oma surnuist ülestõusmise järel Jumala Pojaks väes - Jeesusest Kristusest, meie Issandast,
5Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii.
5kelle käest ma olen saanud armu ja apostliameti, et äratada kuulekust usule tema nime auks kõikide rahvaste seas,
6Ninyi ni miongoni mwa watu hao; mmeitwa muwe watu wake Yesu Kristo.
6kelle seas teiegi olete Jeesuse Kristuse kutsutud -
7Basi, ninawaandikia ninyi nyote mlioko Roma ambao Mungu anawapenda, akawateua muwe watu wake. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
7kõigile Roomas olevaile Jumala armastatuile, kutsutud pühadele: Armu teile ja rahu Jumalalt, meie Isalt, ja Issandalt Jeesuselt Kristuselt!
8Awali ya yote, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inasikika duniani kote.
8Esmalt ma tänan oma Jumalat Jeesuse Kristuse läbi teie kõikide pärast, sest teie usust räägitakse kogu maailmas.
9Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni
9Jumal, keda ma oma vaimus teenin, kuulutades evangeeliumi tema Pojast, on ju minu tunnistaja, kuidas ma lakkamatult meenutan teid
10daima katika sala zangu. Namwomba Mungu akipenda, anipatie nafasi nzuri ya kuja kwenu sasa.
10alati oma palveis, kui ma anun, et ehk ometi õnnestuks mul Jumala tahtmisel kord tulla teie juurde.
11Kwa maana ninatamani sana kuwaoneni ili nipate kuwagawieni zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.
11Ma ju igatsen teid näha, et ma võiksin teile jagada mõnda vaimulikku andi teie kinnituseks,
12Ndiyo kusema, tutaimarishana: imani yenu itaniimarisha mimi, na yangu itawaimarisha ninyi.
12see aga tähendab: teie keskel leida üheskoos julgustust mõlemapoolse usu, teie ja minu oma varal.
13Ndugu zangu, nataka mjue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembeleeni, lakini mpaka sasa nimezuiwa. Ningependa kupata mafanikio mema kati yenu kama nilivyopata kati ya watu wa mataifa mengine.
13Ma ei taha ju, vennad, et teil jääks teadmata: ma olen sageli püüdnud teie juurde tulla, et mul oleks mingit vilja ka teie seas, nagu mul seda on muude rahvaste seas, ent tänini on mulle tulnud ikka mõni takistus.
14Ninalo jukumu kwa watu wote, waliostaarabika na wasiostaarabika, wenye elimu na wasio na elimu.
14Ma olen nii kreeklaste kui umbkeelsete, nii tarkade kui rumalate võlglane.
15Ndiyo maana ninatamani pia kuihubiri Habari Njema kwenu ninyi mlioko huko Roma.
15Seepärast olen valmis ka teile, Roomas asuvaile, kuulutama evangeeliumi.
16Sioni aibu kutangaza Habari Njema; yenyewe ni nguvu ya Mungu inayowaokoa wote wanaoamini: Wayahudi kwanza, na wasio Wayahudi pia.
16Sest ma ei häbene evangeeliumi, see on ju Jumala vägi päästeks igaühele, kes usub, juudile esmalt ja siis kreeklasele.
17Kwa maana Habari Njema inaonyesha wazi jinsi Mungu anavyowakubali watu kuwa waadilifu; jambo hili hufanyika kwa imani, tangu mwanzo mpaka mwisho. Kama ilivyoandikwa: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
17Sest Jumala õigus on ilmunud evangeeliumis usust usku, nii nagu on kirjutatud: 'Aga õige jääb usust elama.'
18Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa binadamu ambao kwa njia zao mbaya wanaupinga ukweli usijulikane.
18Jah, Jumala viha ilmub taevast inimeste igasuguse jumalakartmatuse ja ülekohtu vastu, nende vastu, kes tõde hoiavad ülekohtu kammitsais,
19Kwa maana, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao; maana Mungu mwenyewe ameyadhirisha.
19sest et see, mida teatakse Jumalast, on nende keskel avalik, Jumal on seda neile avaldanud.
20Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea!
20Tema nähtamatu olemus, tema jäädav vägi ja jumalikkus on ju maailma loomisest peale nähtav, kui mõeldakse tema tehtule, nii et nad ei saa endid vabandada,
21Ingawa wanajua kuna Mungu, lakini hawampi heshima anayostahili, wala hawamshukuru. Badala yake, fikira zao zimekuwa batili na akili zao tupu zimejaa giza.
21sest et Jumalat tundes nad ei ole ülistanud ega tänanud teda kui Jumalat, vaid on oma arvamustega jooksnud tühja ning nende mõistmatu süda on jäänud pimedaks.
22Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu.
22Väites endid targad olevat, on nad läinud rumalaks
23Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.
23ja on kadumatu Jumala kirkuse vahetanud kaduva inimese ja lindude ja neljajalgsete ja roomajate kujutistega.
24Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao.
24Seepärast ongi Jumal andnud nemad nende südame himudes rüvedusse, et nad oma ihu ise häbistaksid.
25Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina.
25Nad on Jumala tõe vahetanud vale vastu ning austanud ja teeninud loodut Looja asemel, kes olgu kiidetud igavesti. Aamen.
26Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile.
26Seepärast on Jumal nad andnud häbitute kirgede kätte: nende naised on ju vahetanud loomuliku vahekorra loomuvastasega,
27Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
27nõndasamuti ka mehed, loobudes loomulikust vahekorrast naisega, on oma tungis süttinud üksteise vastu - mees on teinud mehega nurjatust - ja on seega iseenestes saanud kätte paratamatu palga oma eksimuse eest.
28Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya.
28Ja nii nagu nad ei ole hoolinud Jumala tunnetusest, nõnda on Jumal nad andnud kõlbmatu mõtteviisi kätte, tegema seda, mis on väär;
29Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya,
29nad on tulvil igasugust ülekohut, kurjust, ahnust ja tigedust, täis kadedust, tapmist, riidu, kavalust, kiuslikkust, nad on keelekandjad,
30na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao;
30laimajad, Jumala vihkajad, julmurid, ülbed, kelkijad, halva peale leidlikud, vanematele sõnakuulmatud,
31hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine.
31mõistmatud, truudusetud, leppimatud, halastamatud,
32Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.
32kes küll teavad Jumala käsku - et need, kes selliseid asju teevad, on surma väärt -, kuid ei tee seda mitte üksnes ise, vaid tunnevad head meelt neist, kes nii teevad.