1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
1Mis on siis juudil erilist või mis kasu on ümberlõikamisest?
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
2Jah, on palju ja mitmel moel. Esmalt juba see, et juutide kätte on usaldatud Jumala sõnumid.
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
3Mis siis nüüd? Kui mõned pole olnud ustavad, ega siis nende ebaustavus tühista Jumala ustavust?
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
4Mitte sugugi! Kindel on, et Jumal on tõemeelne, aga iga inimene valelik, nagu on kirjutatud: '...selleks, et sind tunnistataks õigeks su sõnades ja sa võidaksid, kui sinuga käidaks kohut.'
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
5Kui aga meie ülekohus toob esile Jumala õigluse, mida me siis peame ütlema? Kas Jumal pole siis ebaõiglane, kui ta meid nuhtleb vihas? Ma räägin inimlikul pinnal.
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
6Mitte sugugi! Kuidas siis muidu saaks Jumal kohut mõista maailma üle?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
7Kui aga Jumala tõde minu valetamise tõttu saab üha rohkem temale kirkuseks, miks siis minu üle veel kohut mõistetakse, nagu oleksin ma patune?
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
8Ja miks siis ei ole nõnda, nagu mõned mind teotades räägivad, et mina ütlevat: 'Tehkem kurja, et sellest tuleks head!' Niisuguste nuhtlus on õige.
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
9Kuidas siis nüüd? On siis meil, juutidel, eeliseid? Ei ainsatki! Me oleme juba esitanud süüdistuse, et nii juudid kui kreeklased on kõik patu võimu all,
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
10nõnda nagu on kirjutatud: 'Ei ole õiget, ei ühtainsatki,
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
11ei ole mõistjat, ei ole Jumala otsijat.
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
12Nad kõik on kaldunud kõrvale, üheskoos kõlbmatuks muutunud, ei ole, kes teeb head, ei ühtainsatki.
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
13Nende kurk on lahtine haud, nende keeled kavaldavad, nende huulte all on maomürk.
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
14Nende suu on täis sajatamist ja kibedust,
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
15nende jalad on nobedad valama verd,
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
16nende teedel on purustus ja viletsus
17njia ya amani hawaijui.
17ja rahu teed nad ei tunne,
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
18ei ole Jumala kartust nende silme ees.'
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
19Aga me teame, et mida Seadus iganes ütleb, seda ütleb ta neile, kes on Seaduse all, et iga suu suletaks ja kogu maailm oleks Jumala ees süüalune;
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
20seepärast et Seaduse tegude tõttu ei mõisteta kedagi õigeks tema ees, sest Seaduse kaudu tuleb patutundmine.
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
21Nüüd aga on ilma Seaduseta saanud avalikuks Jumala õigus, millest tunnistavad Moosese Seadus ja Prohvetid,
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
22see Jumala õigus, mis tuleb Jeesusesse Kristusesse uskumise kaudu kõigile, kes usuvad. Siin ei ole erinevust,
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
23sest kõik on pattu teinud ja ilma jäänud Jumala kirkusest
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
24ning mõistetakse õigeks tema armust päris muidu, lunastuse kaudu, mis on Kristuses Jeesuses,
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
25kelle Jumal on seadnud tema veres lepitusohvriks usu kaudu, et näidata üles oma õigust sellega, et ta kustutas varem tehtud patud
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
26oma jumalikus sallivuses, et näidata üles oma õigust praegusel ajal, et tema ise on õige ja teeb õigeks igaühe, kes usub Jeesusesse.
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
27Kus on nüüd kiitlemine? See on välistatud. Millise seaduse läbi? Kas tegude seaduse läbi? Ei, vaid usu seaduse läbi.
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
28Me ju arvame, et inimene mõistetakse õigeks usu läbi, Seaduse tegudest sõltumata.
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
29Kas Jumal on üksnes juutide Jumal? Eks ta ole ka paganate Jumal? Jah, ta on ka paganate Jumal!
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
30Jumal on üksainus ja tema teeb usu läbi õigeks nii ümberlõigatu kui ümberlõikamatu.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.
31Kas me siis tühistame Seaduse usu läbi? Ei sugugi! Me vaid kinnitame Seadust.