Swahili: New Testament

French 1910

Colossians

3

1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
1Si donc vous êtes ressuscités avec Christ, cherchez les choses d'en haut, où Christ est assis à la droite de Dieu.
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
2Affectionnez-vous aux choses d'en haut, et non à celles qui sont sur la terre.
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
3Car vous êtes morts, et votre vie est cachée avec Christ en Dieu.
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
4Quand Christ, votre vie, paraîtra, alors vous paraîtrez aussi avec lui dans la gloire.
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
5Faites donc mourir les membres qui sont sur la terre, l'impudicité, l'impureté, les passions, les mauvais désirs, et la cupidité, qui est une idolâtrie.
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
6C'est à cause de ces choses que la colère de Dieu vient sur les fils de la rébellion,
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
7parmi lesquels vous marchiez autrefois, lorsque vous viviez dans ces péchés.
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
8Mais maintenant, renoncez à toutes ces choses, à la colère, à l'animosité, à la méchanceté, à la calomnie, aux paroles déshonnêtes qui pourraient sortir de votre bouche.
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
9Ne mentez pas les uns aux autres, vous étant dépouillés du vieil homme et de ses oeuvres,
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
10et ayant revêtu l'homme nouveau, qui se renouvelle, dans la connaissance, selon l'image de celui qui l'a créé.
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
11Il n'y a ici ni Grec ni Juif, ni circoncis ni incirconcis, ni barbare ni Scythe, ni esclave ni libre; mais Christ est tout et en tous.
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
12Ainsi donc, comme des élus de Dieu, saints et bien-aimés, revêtez-vous d'entrailles de miséricorde, de bonté, d'humilité, de douceur, de patience.
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
13Supportez-vous les uns les autres, et, si l'un a sujet de se plaindre de l'autre, pardonnez-vous réciproquement. De même que Christ vous a pardonné, pardonnez-vous aussi.
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
14Mais par-dessus toutes ces choses revêtez-vous de la charité, qui est le lien de la perfection.
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
15Et que la paix de Christ, à laquelle vous avez été appelés pour former un seul corps, règne dans vos coeurs. Et soyez reconnaissants.
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
16Que la parole de Christ habite parmi vous abondamment; instruisez-vous et exhortez-vous les uns les autres en toute sagesse, par des psaumes, par des hymnes, par des cantiques spirituels, chantant à Dieu dans vos coeurs sous l'inspiration de la grâce.
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
17Et quoi que vous fassiez, en parole ou en oeuvre, faites tout au nom du Seigneur Jésus, en rendant par lui des actions de grâces à Dieu le Père.
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
18Femmes, soyez soumises à vos maris, comme il convient dans le Seigneur.
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
19Maris, aimez vos femmes, et ne vous aigrissez pas contre elles.
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
20Enfants, obéissez en toutes choses à vos parents, car cela est agréable dans le Seigneur.
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
21Pères, n'irritez pas vos enfants, de peur qu'ils ne se découragent.
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
22Serviteurs, obéissez en toutes choses à vos maîtres selon la chair, non pas seulement sous leurs yeux, comme pour plaire aux hommes, mais avec simplicité de coeur, dans la crainte du Seigneur.
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
23Tout ce que vous faites, faites-le de bon coeur, comme pour le Seigneur et non pour des hommes,
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
24sachant que vous recevrez du Seigneur l'héritage pour récompense. Servez Christ, le Seigneur.
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
25Car celui qui agit injustement recevra selon son injustice, et il n'y a point d'acception de personnes.