1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
1Or quanto ai tempi ed ai momenti, fratelli, non avete bisogno che vi se ne scriva;
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
2perché voi stessi sapete molto bene che il giorno del Signore verrà come viene un ladro nella notte.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
3Quando diranno: Pace e sicurezza, allora di subito una improvvisa ruina verrà loro addosso, come le doglie alla donna incinta; e non scamperanno affatto.
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
4Ma voi, fratelli, non siete nelle tenebre, sì che quel giorno abbia a cogliervi a guisa di ladro;
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
5poiché voi tutti siete figliuoli di luce e figliuoli del giorno; noi non siamo della notte né delle tenebre;
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
6non dormiamo dunque come gli altri, ma vegliamo e siamo sobri.
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
7Poiché quelli che dormono, dormono di notte; e quelli che s’inebriano, s’inebriano di notte;
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
8ma noi, che siamo del giorno, siamo sobri, avendo rivestito la corazza della fede e dell’amore, e preso per elmo la speranza della salvezza.
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
9Poiché Iddio non ci ha destinati ad ira, ma ad ottener salvezza per mezzo del Signor nostro Gesù Cristo,
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
10il quale è morto per noi affinché, sia che vegliamo sia che dormiamo, viviamo insieme con lui.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
11Perciò, consolatevi gli uni gli altri, ed edificatevi l’un l’altro, come d’altronde già fate.
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
12Or, fratelli, vi preghiamo di avere in considerazione coloro che faticano fra voi, che vi son preposti nel Signore e vi ammoniscono,
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
13e di tenerli in grande stima ed amarli a motivo dell’opera loro. Vivete in pace fra voi.
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
14V’esortiamo, fratelli, ad ammonire i disordinati, a confortare gli scoraggiati, a sostenere i deboli, ad esser longanimi verso tutti.
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
15Guardate che nessuno renda ad alcuno male per male; anzi procacciate sempre il bene gli uni degli altri, e quello di tutti.
16Furahini daima,
16Siate sempre allegri;
17salini kila wakati
17non cessate mai di pregare;
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
18in ogni cosa rendete grazie, poiché tale è la volontà di Dio in Cristo Gesù verso di voi.
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
19Non spegnete lo Spirito;
20msidharau unabii.
20non disprezzate le profezie;
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
21ma esaminate ogni cosa e ritenete il bene;
22na epukeni kila aina ya uovu.
22astenetevi da ogni specie di male.
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
23Or l’Iddio della pace vi santifichi Egli stesso completamente; e l’intero essere vostro, lo spirito, l’anima ed il corpo, sia conservato irreprensibile, per la venuta del Signor nostro Gesù Cristo.
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
24Fedele è Colui che vi chiama, ed Egli farà anche questo.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
25Fratelli, pregate per noi.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
26Salutate tutti i fratelli con un santo bacio.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
27Io vi scongiuro per il Signore a far sì che questa epistola sia letta a tutti i fratelli.
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
28La grazia del Signor nostro Gesù Cristo sia con voi.