1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
1Siate dunque imitatori di Dio, come figliuoli suoi diletti;
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
2camminate nell’amore come anche Cristo vi ha amati e ha dato se stesso per noi in offerta e sacrificio a Dio, qual profumo d’odor soave.
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
3Ma come si conviene a dei santi, né fornicazione, né alcuna impurità, né avarizia, sia neppur nominata fra voi;
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
4né disonestà, né buffonerie, né facezie scurrili, che son cose sconvenienti; ma piuttosto, rendimento di grazie.
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
5Poiché voi sapete molto bene che niun fornicatore o impuro, o avaro (che è un idolatra), ha eredità nel regno di Cristo e di Dio.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
6Niuno vi seduca con vani ragionamenti; poiché è per queste cose che l’ira di Dio viene sugli uomini ribelli.
7Basi, msishirikiane nao.
7Non siate dunque loro compagni;
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
8perché già eravate tenebre, ma ora siete luce nel Signore. Conducetevi come figliuoli di luce
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
9(poiché il frutto della luce consiste in tutto ciò che è bontà e giustizia e verità),
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
10esaminando che cosa sia accetto al Signore.
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
11E non partecipate alle opere infruttuose delle tenebre; anzi, piuttosto riprendetele;
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
12poiché egli è disonesto pur di dire le cose che si fanno da costoro in occulto.
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
13Ma tutte le cose, quando sono riprese dalla luce, diventano manifeste; poiché tutto ciò che è manifesto, è luce.
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
14Perciò dice: Risvegliati, o tu che dormi, e risorgi da’ morti, e Cristo t’inonderà di luce.
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
15Guardate dunque con diligenza come vi conducete; non da stolti, ma da savi;
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
16approfittando delle occasioni, perché i giorni sono malvagi.
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
17Perciò non siate disavveduti, ma intendete bene quale sia la volontà del Signore.
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
18E non v’inebriate di vino; esso porta alla dissolutezza; ma siate ripieni dello Spirito,
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
19parlandovi con salmi ed inni e canzoni spirituali, cantando e salmeggiando col cuor vostro al Signore;
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
20rendendo del continuo grazie d’ogni cosa a Dio e Padre, nel nome del Signor nostro Gesù Cristo;
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
21sottoponendovi gli uni agli altri nel timore di Cristo.
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
22Mogli, siate soggette ai vostri mariti, come al Signore;
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
23poiché il marito è capo della moglie, come anche Cristo è capo della Chiesa, egli, che è il Salvatore del corpo.
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
24Ma come la Chiesa è soggetta a Cristo, così debbono anche le mogli esser soggette a’ loro mariti in ogni cosa.
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
25Mariti, amate le vostre mogli, come anche Cristo ha amato la Chiesa e ha dato se stesso per lei,
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
26affin di santificarla, dopo averla purificata col lavacro dell’acqua mediante la Parola,
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
27affin di far egli stesso comparire dinanzi a sé questa Chiesa, gloriosa, senza macchia, senza ruga o cosa alcuna simile, ma santa ed irreprensibile.
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
28Allo stesso modo anche i mariti debbono amare le loro mogli, come i loro propri corpi. Chi ama sua moglie ama se stesso.
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
29Poiché niuno ebbe mai in odio la sua carne; anzi la nutre e la cura teneramente, come anche Cristo fa per la Chiesa,
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
30poiché noi siamo membra del suo corpo.
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
31Perciò l’uomo lascerà suo padre e sua madre e s’unirà a sua moglie, e i due diverranno una stessa carne.
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
32Questo mistero è grande; dico questo, riguardo a Cristo ed alla Chiesa.
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
33Ma d’altronde, anche fra voi, ciascuno individualmente così ami sua moglie, come ama se stesso; e altresì la moglie rispetti il marito.