Swahili: New Testament

Korean

Luke

1

1Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
1우리 중에 이루어진 사실에 대하여
2Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
2처음부터 말씀의 목격자 되고 일군 된 자들의 전하여 준 그대로 내력을 저술하려고 붓을 든 사람이 많은지라
3Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
3그 모든 일을 근원부터 자세히 미루어 살핀 나도 데오빌로 각하에게 차례대로 써 보내는 것이 좋은 줄 알았노니
4ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
4이는 각하로 그 배운 바의 확실함을 알게 하려 함이로다
5Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
5유대 왕 헤롯 때에 아비야 반열에 제사장 하나가 있으니 이름은 사가랴요 그 아내는 아론의 자손이니 이름은 엘리사벳이라
6Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
6이 두 사람이 하나님 앞에 의인이니 주의 모든 계명과 규례대로 흠이 없이 행하더라
7Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
7엘리사벳이 수태를 못하므로 저희가 무자하고 두 사람의 나이 많더라
8Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
8마침 사가랴가 그 반열의 차례대로 제사장의 직무를 하나님 앞에 행할새
9Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
9제사장의 전례를 따라 제비를 뽑아 주의 성소에 들어가 분향하고
10Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
10모든 백성은 그 분향하는 시간에 밖에서 기도하더니
11Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
11주의 사자가 저에게 나타나 향단 우편에 선지라
12Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
12사가랴가 보고 놀라며 무서워하니
13Lakini malaika akamwambia, "Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
13천사가 일러 가로되 `사가랴여 무서워 말라 너의 간구함이 들린지라 네 아내 엘리사벳이 네게 아들을 낳아 주리니 그 이름을 요한이라 하라
14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
14너도 기뻐하고 즐거워할 것이요 많은 사람도 그의 남을 기뻐하리니
15Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
15이는 저가 주 앞에 큰 자가 되며 포도주나 소주를 마시지 아니하며 모태로부터 성령의 충만함을 입어
16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
16이스라엘 자손을 주 곧 저희 하나님께로 많이 돌아오게 하겠음이니라
17Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake."
17저가 또 엘리야의 심령과 능력으로 주 앞에 앞서 가서 아비의 마음을 자식에게 거스리는 자를 의인의 슬기에 돌아오게 하고 주를 위하여 세운 백성을 예비하리라'
18Zakariya akamwambia huyo malaika, "Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu."
18사가랴가 천사에게 이르되 `내가 이것을 어떻게 알리요 내가 늙고 아내도 나이 많으니이다'
19Malaika akamjibu, "Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
19천사가 대답하여 가로되 `나는 하나님 앞에 섰는 가브리엘이라 이 좋은 소식을 전하여 네게 말하라고 보내심을 입었노라
20Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia."
20보라 이 일의 되는 날까지 네가 벙어리가 되어 능히 말을 못하리니 이는 내 말을 네가 믿지 아니함이어니와 때가 이르면 내 말이 이루리라' 하더라
21Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
21백성들이 사가랴를 기다리며 그의 성소 안에서 지체함을 기이히 여기더니
22Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
22그가 나와서 저희에게 말을 못하니 백성들이 그 성소 안에서 이상은 본 줄 알았더라 그가 형용으로 뜻을 표시하며 그냥 벙어리 대로 있더니
23Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
23그 직무의 날이 다 되매 집으로 돌아가니라
24Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
24이 후에 그 아내 엘리사벳이 수태하고 다섯 달 동안 숨어 있으며 가로되
25"Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu."
25`주께서 나를 돌아 보시는 날에 인간에 내 부끄러움을 없게 하시려고 이렇게 행하심이라' 하더라
26Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
26여섯째 달에 천사 가브리엘이 하나님의 보내심을 받들어 갈릴리 나사렛이란 동네에 가서
27kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
27다윗의 자손 요셉이라 하는 사람과 정혼한 처녀에게 이르니 그 처녀의 이름은 마리아라
28Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."
28그에게 들어가 가로되 `은혜를 받은 자여 ! 평안할지어다 ! 주께서 너와 함께 하시도다' 하니
29Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
29처녀가 그 말을 듣고 놀라 이런 인사가 어찌함인고 생각하매
30Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
30천사가 일러 가로되 `마리아여 무서워말라 네가 하나님께 은혜를 얻었느니라
31Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
31보라 네가 수태하여 아들을 낳으리니 그 이름을 예수라 하라
32Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
32저가 큰 자가 되고 지극히 높은신 이의 아들이라 일컬을 것이요 주 하나님께서 그 조상 다윗의 위를 저에게 주시리니
33Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho."
33영원히 야곱의 집에 왕노릇하실 것이며 그 나라가 무궁하리라'
34Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?"
34마리아가 천사에게 말하되 `나는 사내를 알지 못하니 어찌 이 일이 있으리이까 ?'
35Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
35천사가 대답하여 가로되 `성령이 네게 임하시고 지극히 높으신 이의 능력이 너를 덮으시리니 이러므로 나실 바 거룩한 자는 하나님의 아들이라 일컬으리라
36Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
36보라 네 친족 엘리사벳도 늙어서 아들을 배었느니라 본래 수태하지 못한다 하던 이가 이미 여섯 달이 되었나니
37Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu."
37대저 하나님의 모든 말씀은 능치 못하심이 없느니라 !'
38Maria akasema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema." Kisha yule malaika akaenda zake.
38마리아가 가로되 `주의 계집종이오니 말씀대로 내게 이루어지이다 !' 하매 천사가 떠나가니라
39Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
39이 때에 마리아가 일어나 빨리 산중에 가서 유대 한 동네에 이르러
40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
40사가랴의 집에 들어가 엘리사벳에게 문안하니
41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
41엘리사벳이 마리아의 문안함을 들으매 아이가 복 중에서 뛰노는지라 엘리사벳이 성령의 충만함을 입어
42akasema kwa sauti kubwa, "Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
42큰 소리로 불러 가로되 `여자 중에 네가 복이 있으며 네 태중의 아이도 복이 있도다
43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
43내 주의 모친이 내게 나아오니 이 어찌 된 일인고
44Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
44보라 네 문안하는 소리가 내 귀에 들릴 때에 아이가 내 복중에서 기쁨으로 뛰놀았도다
45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia."
45믿은 여자에게 복이 있도다 주께서 그에게 하신 말씀이 반드시 이루리라'
46Naye Maria akasema,
46마리아가 가로되 내 영혼이 주를 찬양하며
47"Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
47`내 마음이 하나님 내 구주를 기뻐하였음은
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
48그 계집종의 비천함을 돌아 보셨음이라 보라 이제 후로는 만세에 나를 복이 있다 일컬으리로다
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
49능하신 이가 큰 일을 내게 행하셨으니 그 이름이 거룩하시며
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
50긍휼하심이 두려워하는 자에게 대대로 이르는도다
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
51그의 팔로 힘을 보이사 마음의 생각이 교만한 자들을 흩으셨고
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
52권세있는 자를 그 위에서 내리치셨으며 비천한 자를 높이셨고
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
53주리는 자를 좋은 것으로 배불리셨으며 부자를 공수로 보내셨도다
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
54그 종 이스라엘을 도우사 긍휼히 여기시고 기억하시되
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele."
55우리 조상에게 말씀하신 것과 같이 아브라함과 및 그 자손에게 영원히 하시리로다' 하니라
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
56마리아가 석 달쯤 함께 있다가 집으로 돌아 가니라
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
57엘리사벳이 해산할 기한이 차서 아들을 낳으니
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
58이웃과 친족이 주께서 저를 크게 긍휼히 여기심을 듣고 함께 즐거워 하더라
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
59팔일이 되매 아이를 할례하러 와서 그 부친의 이름을 따라 사가랴라 하고자 하더니
60Lakini mama yake akasema, "La, sivyo, bali ataitwa Yohane."
60그 모친이 대답하여 가로되 `아니라 요한이라 할 것이라' 하매
61Wakamwambia, "Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?"
61저희가 가로되 `네 친족 중에 이 이름으로 이름한 이가 없다' 하고
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
62그 부친께 형용하여 무엇으로 이름하려 하는가 물으니
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: "Yohane ndilo jina lake." Wote wakastaajabu.
63저가 서판을 달라 하여 그 이름은 요한이라 쓰매 다 기이히 여기더라
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
64이에 그 입이 곧 열리고 혀가 풀리며 말을 하여 하나님을 찬송하니
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
65그 근처에 사는 자가 다 두려워하고 이 모든 말이 온 유대 산중에 두루 퍼지매
66Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: "Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?" Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
66듣는 사람이 다 이 말을 마음에 두며 가로되 `이 아이가 장차 어찌 될꼬 ?' 하니 이는 주의 손이 저와 함께 하심이러라
67Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
67그 부친 사가랴가 성령의 충만함을 입어 예언하여 가로되
68"Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
68`찬송하리로다 주 이스라엘의 하나님이여 그 백성을 돌아보사 속량하시며
69Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
69우리를 위하여 구원의 뿔을 그 종 다윗의 집에 일으키셨으니
70Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,
70이것은 주께서 예로부터 거룩한 선지자의 입으로 말씀하신 바와 같이
71kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
71우리 원수에게서와 우리를 미워하는 모든 자의 손에서 구원하시는 구원이라
72Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
72우리 조상을 긍휼히 여기시며 그 거룩한 언약을 기억하셨으니
73Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
73곧 우리 조상 아브라함에게 맹세하신 맹세라
74tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
74우리로 원수의 손에서 건지심을 입고
75kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
75종신토록 주의 앞에서 성결과 의로 두려움이 없이 섬기게 하리라 하셨도다
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
76이 아이여 네가 지극히 높으신 이의 선지자라 일컬음을 받고 주앞에 앞서 가서 그 길을 예비하여
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
77주의 백성에게 그 죄 사함으로 말미암는 구원을 알게 하리니
78Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
78이는 우리 하나님의 긍휼을 인함이라 이로써 돋는 해가 위로부터 우리에게 임하여
79na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."
79어두움과 죽음의 그늘에 앉은 자에게 비취고 우리 발을 평강의 길로 인도하시리로다' 하니라
80Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
80아이가 자라며 심령이 강하여지며 이스라엘에게 나타나는 날까지 빈 들에 있으니라