Swahili: New Testament

Paite

1 Corinthians

11

1Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
1Hon enjuite hi un, kei leng Kris enjuipa ka hih mahbangin
2Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
2Huan, bangkima non theihgige jiak un leh thukhah kon hilh bang taka na vom chinten jiak un kon phat ahi.
3Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
3Ahihhangin, pasal peuhmah lutang tuh Kris ahi, numei lutang tuh pasal ahi, Kris lu tuh Pathian ahi chih na theih uh ka deih hi.
4Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
4Pasal, a lu khuh kawma thum hiam, thugen hiam peuhmahin, a lu a selphou hi.
5Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
5Ahihhangin, numei, a lu khuhloua thum hiam, thugen hiam peuhmahin a lu a selphou ahi; metmai toh kibangleltak ahi ngala.
6Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
6Numei a lu khuh loua a om ngal leh met vanglak hen. Ahihhangin, numei adinga sam met hiam mei maihiam a zumhuai leh, kikhuh hen.
7Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
7Pasal jaw Pathian batpih leh thupina a hih jiakin a lu a khuh ding hi lou himhim ahi; numei bel pasal thupina ahi a.
8Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
8Pasal jaw numei akipana pawt ahi keia; numei bel pasal akipana pawt ahi jaw hi:
9Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
9Pasal numei adia siam leng ahi sam kei; numei bel pasal adia siam ahi ajaw:
10Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
10Huai ahihjiakin, angelte jiakin numeiin pasal thuneih chiamtehna a khuk ding ahi.
11Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
11Himahleh, Toupa thilgel dan ah, numei pasal louin a om theikeia, pasal leng numei louin a om thei sam kei hi.
12Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
12Numei pasal akipana pawt ahi bangmahin pasal leng numei laka piang ahi ngal a; ahihhangin, bangkim Pathiana kipana pawt vek ahi.
13Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
13Noumau kingaihtuah dih ua, numeiin a lu khuh loua Pathian kianga thum a kilawm hiam?
14Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
14Pasal in sam sau a neih leh, amah adingin a zumhuai ahi chih na lungtang pianpih un leng a honthei sak kei ahia?
15lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
15Numeiin bel sam sau a neih leh amah dingin thupina ahi jaw; a sam khuhna dinga piak ahi ngala.
16Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
16Abang abang hitaleh, kuapeuh a selkhah leh, huchibang dan himhim i neikei uh, Pathian saptuam pawlten leng a nei sam kei hi.
17Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
17Ahihhangin, nou hiai thu ka hon hilhna ah kon phat theikei, na hoih semna ding lam uh hi louin, na siat semna ding lam jaw ua na kikhop nak jiak un.
18Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
18Amasapenin, saptuamte-a na kikhop un, na lak uah kilangkhenna a om nak chih ka za ngala; gin leng ka gingta sim sam hi.
19maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
19Na lak ua a taktakte a lat theihna ding un, na lak ua gin tuamna leng a om sam him ding ahi.
20Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
20Huchibangin, na kikhop un, Toupa nitakan nek theihna vual ahi kei:
21Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
21Michihin nanek un noumau nitakan na ne masa jel ngal ua; huchiin, mi khat gil a kiala, adangin a kham ngala.
22Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
22Bangchidan ahia? Nek leh dawnna ding, in na neikei ua hia? Ahihkeileh, Pathian saptuamte na musit ua, bangmah neiloute na selphou ua hia? Na kiang uah bang ka genta dia? Kon phat dia hia? Hiai lam thu ah ka honphat theikei hi.
23Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
23Ka thu honhilh sawn Toupa kianga kipana ka muh ahi a, huchia Toupa Jesun matsaka a om jana, tanghou a laka,
24akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: "Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
24Kipahthu a gen khita a balkhapa, Hiai ka pumpi nou adia piak ahi, Keimah theihgigena in hiai hih jel un, a chih.
25Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: "Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka."
25Huchimahbanga, nitakan nek khita nou leng a laka, Hiai nou ka sisana thukhun thak ahi, Na dawn teng un keimah theihgigena in hiai hih jel un, a chih.
26Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
26Huai tanghou na nek ua, nou na dawn teng un, a hongpai nawn masiah, Toupa sihna na phuangjak jel uh ahi ngala.
27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
27Huaijiakin, kuapeuh kilawm loutaka tanghou ne hiam, Toupa nou dawn hiam tuh, Toupa pumpi leh sisan tungah siamlouh a tang ding hi.
28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
28Huchiin, mi amah kienchian jaw hen, huchibangin tanghou tuh nein nou tuh dawn hen.
29maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
29A ne leh dawnin, Toupa pumpi ngentel taka a ngaihtuah keileh, amah tunga vaihawmna dingin a nein a dawn jel ahi ngala.
30Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
30Hiaijiakin, na lak ua mi tampi na hat kei ua, na jawngkhal uhi, duaisan leng na ihmu kei uhi.
31Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
31Ahihhangin, ngentel takin eimah kingaihtuah jel lehang vaihawm saka om nak lou ding i hi uhi.
32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
32Himahleh, vaihawm saka i omin leng, khovel toh siamlouhtanga i om louhna dingin, Toupa taihilhin i om jel ahi.
33Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
33Huaijiakin, ka unaute aw, ne dinga na kikhop in kingak chiat un.Na kikhop uh vaihawmna na thuak pih louhna ding un, kuapeuhin a gil a kial leh a in lamah ne hen. Huan, thu dang jaw ka hong peuhpeuh chiangin kon hilh ding hi.
34Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.
34Na kikhop uh vaihawmna na thuak pih louhna ding un, kuapeuhin a gil a kial leh a in lamah ne hen. Huan, thu dang jaw ka hong peuhpeuh chiangin kon hilh ding hi.